DAR ES SALAAM
Na Mathayo Kijazi
Mkuu wa Idara ya Walei Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Delphinus Ngaiza, amewasihi Viongozi wa Utume wa Wanaume Katoliki (UWAKA) Taifa, kuiga mfano wa Mtakatifu Yosefu kwa kuwa wanyenyekevu, na wenye kumtanguliza Mungu katika mambo yao.
Padri Nagiza alisema hayo hivi karibuni katika homilia yake, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu, katika Mkutano wa Viongozi hao wa UWAKA, walipokutana kwa lengo la kujadili mambo mbalimbali, yatakayokiendeleza chama hicho cha kitume ngazi ya Taifa, uliofanyika katika Kiwanda cha Woiso Original Products, kilichopo Salasala jijini Dar es Salaam.