Print this page

Watakiwa kuikwepa rushwa kama ukoma

By September 18, 2023 350 0

DAR ES SALAAM

Na Esther Ngubes- TUDARCO

Wakatoliki wametakiwa kuepuka dhuluma, wizi na rushwa kwa sababu ni matendo maovu mbele ya Mungu.
Aidha, wameaswa kuacha kujihusisha na vitendo vya utoaji mimba, na wenye kushiriki vitendo hivyo vya uuaji yawapasa kufanya toba kwa Mwenyezi Mungu.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Padri wa Jimbo Katoliki la Shiyanga, Padri Dunstan Sita, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mwokozi, Sinza, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.
“Tunaalikwa kuwa na moyo mkuu, moyo hodari, na hatupaswi kuwa na deni…baadhi ya familia hususan wazazi na walezi, wanawasaidia mabinti kutoa mimba, jambo hilo ni baya na watu wanatakiwa wakatubu,” alisema Padri Sita.
Padri huyo alisema kwamba waamini wanapaswa kuwa sababu ya watu wengine ili kufikia malengo na mafanikio yao, na kuwa taa kwa kuwaonya watu wanaokosea katika ngazi za familia hadi Jumuiya.
Aliendelea kusema kwamba Kanisa lina wajibu mkubwa wa kuonya na kuwasaidia watu wanaokosea na wale wenye kwenda kinyume na maadili.
Padri Sita alisema pia kuwa dhambi ni chukizo kwa Mungu, hivyo waamini wasiwe wanatakiwa kuanza kuishi kwa mazoea, na badala yake waonyeshe upendo kwa wenzao.

Rate this item
(0 votes)
Japhet