DODOMA
Na Mwandishi wetu
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amewaasa wataalamu wa sekta za mifugo na uvuvi kupeleka na kufundisha teknolojia za sekta hizo vijijini, ili kuwapa elimu wafugaji kuhusu ufugaji wa kisasa, na hivyo kuleta tija.
Alisema hayo alipotembelea kwenye Maonesho ya Kilimo ya Kimataifa (Nane Nane) yaliyofanyika Kitaifa mkoani humo.