DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimesema kuwa hali ya uwekezaji nchini imeongezeka katika kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka huu.
Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Gilead Teri alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kueleza kwamba TIC ilisajili miradi 198 yenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 1.69 sawa na zaidi ya Shilingi trilioni tatu, itakayoajiri watu 9600 kote nchini.