Dar es Salaam
Na Mwandishi wetu
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Tanzania Forest Services Agency: TFS) umesema kwamba utaendelea kuhamasisha Watanzania kujikita katika ufugaji nyuki kwa kuzingatia maelekezo yote muhimu, na kuwa na vifungashio vyenye ubora unaokubalika.
Hayo yalisemwa na Ofisa Ufugaji Nyuki, Masoko na Leseni wa TFS, Theresia Kamote, wakati wa Maadhimisho ya Barcode Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.