MBEYA
Na Angela Kibwana
Mhashamu Godfrey Jackson Mwasekaga, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Mbeya, amesema malengo ya Kwaresima ni kufanya toba, wongofu wa ndani na uaminifu kwa neno la Mungu.
Aidha, amesema kuwa Neno la Mungu ni chakula cha kiroho, na ni taa ya kuwaongoza waamini kwenye njia ya Ukristo wao.
Askofu Mwasekaga alisema hayo wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu, aliyoadhimisha katika Parokia ya Mtakatifu Clara wa Asizi- Shewa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya.