DAR ES SALAAM
Na Mathayo Kijazi
Waamini wameonywa kuepuka kukata tamaa kutokana na majaribu wanayokutana nayo, kwani hayo ni sehemu ya maisha yao.
Kauli hiyo ilitolewa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia – Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Musa Kihoo wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima iliyofanyika parokiani hapo.