BAGAMOYO
Na Mathayo Kijazi
Baada ya mchakato wa muda mrefu hatimaye Bagamoyo Lango la Ukristo Tanzania sasa historia yake imekamilika, kutokana na kuundwa kuwa Jimbo jipya Katoliki, huku Baba Mtakatifu Fransisko akimteua Mhashamu Askofu Mteule Stephano Musomba, kuwa Askofu wa kwanza wa jimbo hilo.
Kabla ya uteuzi huo Mhashamu Musomba alikuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, aliyekuwa akisimamia Mawasiliano jimboni humo.