VATICAN CITY-Vatican
Maadhimisho ya kumtangaza Mwenyeheri Carlo Acutis kuwa Mtakatifu yamesitishwa kufuatia kifo cha Papa Fransisko.
Maadhimisho hayo yaliyokuwa yafanyike Dominika ya Aprili 27, mwaka huu yamesitishwa kusubiria kupatikana kwa Baba Mtakatifu mpya.
Kijana huyo aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 15, kwa sababu ya ugonjwa wa saratani ya damu Oktoba 12, mwaka 2006 tayari ametangazwa Mwenyeheri huko Assisi Oktoba 10, mwaka 2020.
Mwili wake umekuwa ukipumzika tangu 2019, katika Kanisa la Mtakatifu Maria Mkuu (Maria maggiore), Assisi.
Kwa njia hiyo Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican imefahamisha kwamba, Adhimisho la Ekaristi Takatifu na ibada ya kutangazwa kuwa Mtakatifu iliyopangwa kufanyika katika Maadhimisho ya Jubilei ya Vijana, imesitishwa.