Na Askofu Mstaafu Method Kilaini
Wahuni:
Wahuni walikuwa wapiganaji wakali sana, na ndio walioleta matatizo yaliyozusha uvamizi. Wahuni walikuwa watu wa Mashariki ya mbali (Mongoliani, waasia wa ngozi ya njano). Wahuni walikuwa wachungaji wakiishi Kaskazini ya Milima ya Himalaya.
Malisho yalipoisha, hawa wapanda farasi, walianza kuvamia nchi nyingine. Mwaka 200 Baada ya Kristo (BK), walikwea ukuta wakaivamia China na kusambaratisha himaya yake, na tangu hapo ikawa nyakati za giza kwa miaka 400 iliyofuata kwa China.