Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Makala

Makala (54)

Na Paul Mabuga

Jua la adhuhuri liliwaka eneo kuu la biashara na lenye shughuli nyingi katikati ya Jiji la Mwanza. Nilimpa muuza magazeti, makala ya toleo la gazeti moja la kila siku la Kiswahili, kwa mwaliko wa kimya kimya wa kumshirikisha kwa habari zinazovutia siku hiyo.
Dakika zilipita, kisha nikauliza: “Ni nini kinakuvutia?” Alionesha tangazo la EWURA, mwanga wa matumaini mbele ya matatizo ya maji yasiyoisha.
“Ni kuhusu suluhisho,” alisema.  Nilisubiri zaidi, lakini kurasa alizipita na baadaye anasema hakuna cha ziada.
Baadaye, kwenye vurugu za soko la Mlango Mmoja. Muuzaji, macho yakimtoka, alilishika gazeti kana kwamba lilikuwa adimu, lakini kumbe kwake ni la gharama kubwa. “Shilingi 1000?” alisema kwa mshangao.
“Hiyo ni chakula cha mchana cha ugali na fulu!” Gharama, sio maudhui, pengine ndio ingeuwa kichwa cha habari kwake kuliko yaliyomo kwenye gazeti.
Kisha katika safari ya kurejea maskani nikiwa nimebanwa kwenye daladala, mazungumzo na jirani yangu, kijana aliyejitambulisha kuwa msomi, yalifunua mtazamo tofauti.
 “Mitandao ya kijamii,” alisema kwa dharau, akipitia kurasa. “Matukio ya moja kwa moja kwenye TV tunaona yote kwa haraka zaidi.” Kwa hiyo Gazeti, mikononi mwake, lilionekana kama halina cha maana, maana mengi alishayapata kabla. ZAIDI KWENYE TUMAINI LETU.

Na Joseph Mihangwa

Katika mkutano wa nchi tajiri duniani (G.8), uliofanyika Gleneagles, mwaka 2005, chini ya kauli mbiu ya “Ufanye Umaskini Uwe Historia”, nchi hizo ziliahidi kuipatia Afrika  dola za Kimarekani bilioni 50 ili zijikwamue kutoka kwenye umaskini.

Mpaka sasa nchi hizo hazijatekeleza ahadi yake, badala yake Afrika inaendelea kupata fedha za mzunguko wa mikopo kwa  masharti magumu.

Masharti hayo ni pamoja na kuuza/kubinafsisha Rasilimali za Taifa, kama tulivyofanya kwa Mashirika muhimu kama Benki ya NBC, NMB na mashinikizo mengine, kama vile kuruhusu vituo vya kijeshi vya Marekani nchini [AFRICOM], kutunga sheria dhidi ya “Ugaidi”, ambacho hiki kinachoitwa “Ugaidi” kusema kweli ni harakati za wanyonge dhidi ya ubabe, ubeberu na ukoloni mamboleo wa nchi za Magharibi.

Si hivyo tu, hata ahadi na misaada inayotolewa siku zote ni chini ya kiwango/kiasi kinachotamkwa. Na kwa mujibu wa taarifa ya Shirika  moja lisilo la Kiserikali barani Ulaya, CONCORD, iliyopewa jina, “Hold the Applause” [Usishangilie], ni kwamba, zaidi ya asilimia 30 ya sehemu ya misaada inayotolewa au kuahidiwa na nchi fadhili, si misaada halisi bali ni misaada iliyobinywa na urejeshaji kubebwa na Serikali inayofadhiliwa. INAENDELEA KWENYE GAZETI TUMAINI LETU.

HISTORIA YA KANISA

Na Askofu Mstaafu Method Kilaini

Mitume na wafuasi wa Kristo toka mwanzo kilele na kitovu cha Imani yao kilikuwa kifo na ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo. Injili zote zinasimulia juu ya wiki ya mwisho ya maisha ya Bwana wetu Yesu Kristo ulimenguni au kwa naneno mengine tunachoadhimisha kama Juma Kuu ikiwa ni matukio ya  kuwaaga mitume, kushikwa, kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Hiki ndicho kilikuwa kilele cha simulizi zote. Kwa namna ya pekee tunayakuta katika Injili ya Mt. Yohana sura ya 12 hadi 20, ambayo inasimulia kwa kinaganaga juma hilo kuu. Mtakatifu Yohana alikuwa shuhuha wa matukio haya yote na hadi kifo chake aliyakumbuka kwa uwazi, yalimwachia alama kubwa katika maisha yake.
Yesu Kristo alikufa na kufufuka wakati wa maadhimisho ya Pasaka ya Wayahudi. Katika siku hizo Wayahudi humkumbuka Musa na kukombolewa kwao kutoka utumwani Misri. Huadhimisha mapatano kati ya Mungu na taifa lao la  Israel.
Pasaka, yalikuwa ni maadhimisho ya juma zima, wakikumbuka na kusimilia historia yao kuanzia baba zao walipokula chakula cha mwisho huko Misri, ikiwa ni mkate bila kutiwa chachu na mboga chungu na nyama ya kondoo, ambaye damu yake  waliipaka milango yao.

SOMA ZAIDI KATIKA TUMAINI LETU.

1. Utangulizi
Kipindi cha Kwaresima kinahusika na liturujia ya kubariki mafuta na kuweka wakfu Krisma. Askofu hana budi kuwa kuhani mkuu wa kundi lake. Maisha ya Waamini wake katika Kristo, kwa namna fulani yanatokana naye na kumtegemea yeye.
Askofu huadhimisha Misa ya Krisma, pamoja na Mapadri waliotoka sehemu mbalimbali za Jimbo Lake. Katika Misa hiyo huweka wakfu Krisma na kubariki mafuta mengine. Misa hii ya Krisma ni njia mojawapo kubwa ya kuonyesha ukamilifu wa Ukuhani wa Askofu, na ni ishara ya muungano mkubwa uliopo kati ya Askofu na Mapadri wake.
Misa ya Kubariki mafuta ya Krisma, hufanyika kabla ya Misa ya Karamu ya Mwisho ya Bwana. Misa haiadhimishwi bila mkusanyiko wa Waamini. soma kwenye Tumaini Letu

DAR ES SALAAM

Na Joseph Mihangwa

Ghafla, Afrika imenyamaza kupiga kelele juu ya paa kutangaza sera zake za maendeleo zenye sura ya ubinadamu; sera zilizojaa kurasa za Vyombo vya Habari enzi za uhuru na zama za mageuzi ya uchumi kufuatia uhuru, kwa maandishi makubwa makubwa na kwa wino wa kuangaza:
“Ujamaa” kwa Tanzania; “Zambian Humanism” kwa Zambia; The Common Man’s Charter” – Uganda na “The Guinean Revolution” kwa Guinea ya Rais Ahmed Sekou Toure.

Ujenzi wa Miundo mbinu:
Mwishoni mwa mkutano waliunda Shirika lililoitwa: ‘Inter-Regional Episcopal Board of Eastern Africa (ITEBEA)’. Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Zambia, Fr. Killian Flynn, OFM Cap alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wake wa kwanza na kuanzia mwaka 1964 akawa na ofisi ya kudumu Nairobi, Kenya.
Fr. Killian Flynn ndiye Baba wa Amecea aliyehudumu hadi mwaka 1972. Askofu Mkuu Adam Kozlowiecki, (Baadaye Kadinali) wa Lusaka, Zambia alikuwa Mwenyekiti wake wa kwanza.
Mkutano wa Pili ulikuwa huko Roma: Wakati wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikani (1962 -65) Maaskofu walipata muda wa kufahamiana zaidi na mnamo Novemba 1964 Maaskofu walikutana Roma katika Chuo cha Mt.  Anselmo.

SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Fransisko amesema kuwa mateso na mahangaiko ya mwanadamu, ni zawadi ya matumaini na uaminifu wa Mungu katika Fumbo la Pasaka, na kwamba upendo wa Mungu daima utawaandama waja wake hata wakati wa majaribu na vikwazo katika maisha yao.
Papa alitoa ujumbe huo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya 33 ya Wagonjwa Duniani mwaka 2025, iliyoadhimishwa mjini Vatican, siku ambayo ilianzishwa Mei 13 mwaka 1992, na kuadhimishwa kwa mara ya kwanza kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa Lourdes nchini Ufaransa, mnamo Februari 11 mwaka 1993.
Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa kwa ngazi ya kijimbo yaliyoadhimishwa mwaka huu wa 2025, yananogeshwa na kauli mbiu isemayo, “Na tumaini halitahayarishi, lakini hutuimarisha wakati wa majaribu,” huku Baba Mtakatifu akiwaalika watu wote wa Mungu kuwa Mahujaji wa Matumaini.

DAR ES SALAAM

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mitihani ya kuhitimisha Kidato cha Nne, Tanzania (CSEE) ilifanyika Novemba 11 hadi 29, 2024.
Matokeo yakatangazwa rasimi Januari 23, 2025 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (National Examinations Council of Tanzania: NECTA) Dk. Said Mohammed kupitia hafla na Waandishi wa Habari.
Taarifa iliyotolewa na Mtendaji Mkuu wa NECTA, ilionyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia tatu (3) kutokana na watahiniwa wengi kufaulu.
Hiyo inamaanisha kuwa kati ya watahimiwa 516,695, kati ya hao watahiniwa 477,262 wamefauli kwa madaraja: I, II, III na IV; ikiwa ni ufaulu wa asilimia 92.37 kulinganisha na matokeo ya mitihani ya 2023 yenye ufaulu wa asilimia 89.36 tu.
Kadhalika, ufaulu kwa madaraja ya I, II na III ni watahiniwa 221,952 sawa na asilimia 43, wakati mwaka 2023 walikuwa watahiniwa 197,426 sawa na asilimia 37.4 tu.
Vile vile, matokeo yameonyesha kuwa waliopata daraja la nne (iv) pamoja na waliopata alama (sufuri) wamepungua kulinganisha na matokeo ya mwaka 2023; hivyo kuashiria ongezeko la asilimia 5.6 wa ubora wa kufaulu.
Hata hivyo, Katibu Mtendaji, NECTA alibainisha kuwa kwa matokeo ya mwaka 2024, watahiniwa 67, NECTA imelazimika kufuta matokeo yao kutokana na udanganyifu wakati wakifanya mitihani.

DAR ES SALAAM

Na Alex Kachhelewa

Viongozi wa Matifa ya Afrika Mashariki (East African Community: EAC) na wale wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community: SADC), walikutana hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Mkutano Maalumu kuhusu kusaka suluhu ya mzozo wa vita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Mzozo huo ni kati ya Majeshi ya Serikali ya DRC dhidi ya Vikosi vya Waasi wa Movement For March 23- au maarufu kama M23, wanaosadikiwa kuuteka Mji wa Goma, Mashariki mwa nchi hiyo.
Katika mkutano huo ambapo Rais wa DRC Felix Tshisekedi Shilombo, yeye alishiriki kwa njia ya Mtandao, Viongozi hao walifanya maamuzi yatakayosaidia kurejesha amani  katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), iliyogubikwa na mzozo wa muda mrefu zaidi kuwahi kushuhudiwa.
Mkutano huo uliwakaribisha viongozi hao chini ya Mwenyeji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, uliohudhuriwa na wakuu wa nchi na serikali kutoka mataifa wanachama wa EAC na SADC,  ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa EAC, Rais William Ruto wa Jamhuri ya Kenya, na Mwenyekiti wa SADC, Rais Emmerson Mnangagwa wa  Jamhuri ya Zimbabwe,  hapakuwapo Rais wa Congo DRC Felix Tshisekedi, ambaye alishiriki kwa njia ya mtandao.

MOROGORO

Na Angela Kibwana

Mpendwa msomaji, katika mfululizo wa makala haya ya “Wajibu wa Kanisa kwa Watu Wenye Ulemavu katika Huduma za Kiroho,” Makala yaliyopita yalianza na kuonesha kwamba Kanisa kama Jumuiya ya Waamini wanaomwamini Kristo, msingi wake ni Kristo mwenyewe ((Waefeso 5: 29; Wakolosai, 1: 24 na Wakolosai 2:10).
Katika kulithibitisha hilo, makala hayo yalionesha namna Yesu Kristo mwenyewe alivyokasimisha majukumu yake  ya  kulihudumia Kanisa  la hapa duniani  kupitia Mtume Petro, na msingi huo huo ndiyo asili ya uwepo wa  Kanisa Katoliki ((Mathayo, 16:18).
Makala hayo yalisisitiza kwa kuwa Yesu Kristo ndiye msingi wa Kanisa, Kanisa la duniani halina budi kuyaishi maneno, matendo pamoja na kuubeba wajibu ambao Yesu Kristo aliukasimisha kwa Kanisa la hapa duniani, kama ilivyothibitishwa kupitia Biblia Takatifu na mafundisho ya mama Kanisa.
Makala hayo pia yalisisitiza kuwa Kanisa kama Jumuiya ya Waamini wanaomwamini Kristo, Waamini wake wanayo mahitaji tofauti, ambayo ndio msingi wa ustawi wao, kiroho na kimwili.
Makala hayo yakaangazia ni kwa namna gani Kanisa la hapa duniani linaweza au linayatafsiri mahitaji hayo katika utekelezaji wa majukumu yake kiroho na kimwili, pasipo kumwacha Waamini yeyote ambaye ni mwili na Kielelezo cha Kristo nje ya huduma hizo. “Waamini wenye ulemavu na mahitaji yao ya kiroho, ndio ukawa msingi wa makala hayo.”
Katika makala ya toleo hili, tunaendelea kuangazia hali ya upatikanaji wa huduma za kiroho ndani ya Kanisa Katoliki kwa watu wenye ulemavu, pasipo kuyatenga makundi mengine ya watu wenye ulemavu. Makala haya yatajikita kwa undani zaidi kwenye vikwazo vya mawasiliano kwa kundi la watu wenye ulemavu wa kuongea na kusikia, ili kuweka usawa wa kihuduma kiroho, kiafya,kijamii na kimtazamo pia.
Kutokana na takwimu za matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 nchini Tanzania, kati ya watu wote wenye ulemavu, ulemavu wa kuona,kusikia, kuongea na kutembea ni 6.5% ya Watanzania wote, ambayo ni sawa na jumla ya watu 3,154,514kuanzia umri wa miaka saba (7)na kuendelea pasipo kujali dhehebu au dini ya mhusika, kwa hiyo kutokana na hali zao watu hawa wanahitaji mipango na mikakati maalum ya kuwafikia kwa huduma za kimwili, kijamii, kiafya, kielimu na kiroho pia.
Mpendwa msomaji wa makala haya katika kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata huduma za kiroho leo hii nitaangazia wajibu huo kuanzia katika msingi wa familia na  jumuiya ndogondogo za Kikristu.
Kanisa Katoliki linajengwa kuanzia ngazi ya familia halafu jumuiya  ndogondogo za Kikristu ukiwa ni mwito wa kuwakaribisha watu wote  katika jamii ya waamini wanao mwamini Kristo kuwa Kristo ndiyo  kichwa na mwili wa kanisa
Katika waraka wa Mtakatifu Paulo kwa Wakorintho, tunakumbushwa kuwa mwili wa Kristo una viungo vingi, na kila kimoja kina thamani na nafasi yake (1 Kor. 12:12-27).
Hili ni somo muhimu linalotufundisha kuwa hakuna anayepaswa kuachwa nyuma katika mpango wa wokovu, ikiwa ni pamoja na watu wenye ulemavu kwa ujumla.
Huduma za kiroho kwa watu wenye ulemavu wa kusikia ni mwaliko wa dhati wa kuhakikisha kwamba kundi hili linaloshiriki kikamilifu katika maisha ya kiroho ya jumuiya, ikiwa ni haki yao ya kimsingi kama waamini na wana wa Mungu, ambao walibatizwa na kuwa sehemu ya familia ya Kanisa.
Kwa msingi huu, huduma hizi zinapaswa kuwekwa kama kipaumbele katika jitihada za Kanisa za kujenga jumuiya ndogondogo zinazojumuisha watu wote kuanzia ngazi ya familia bila ubaguzi unaotokana na hali zao.
Jumuiya za Kikristo, hasa ndani ya mazingira ya Parokia, zina jukumu la kutambua kuwa ulemavu wa kusikia,kutembea, kuongea au kuona, siyo kikwazo kwa imani, badala yake, ni fursa ya kuthibitisha wito wa Kanisa wa kuwa sauti ya matumaini na mshikamano kwa kundi hilo.
Maandiko Mtakatifu, mfano Warumi, 15:1, inaonesha jinsi ambavyo wana Kanisa wanavyoitwa kuwa na moyo wa huduma na kusaidia wale walio na udhaifu wa aina yoyote, ikiwemo ulemavu.”Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wa wanyonge, wala si kujipendeza wenyewe.”
Kanisa Katoliki linapofanya sensa kujua idadi ya waamini wake, kadhalika sensa hiyo inapaswa kuwajumuisha watu wenye ulemavu ili kujua idadi yao, taarifa na mahitaji yao ili yatafsiriwe katika huduma za kiroho na huduma nyingine.
Kadhalika, Kanisa lina wajibu wa kuandaa mwongozo kwa watu wenye ulemavu, ambao utaonesha namna ya kuwafikia kuanzia ngazi ya familia, jumuiya Ndogo Ndogo,Parokia na taasisi zake  kwa ujumla, ili waweze kupata huduma za kiroho, ikiwa ni pamoja na kuwalinda kwa sababu Kanisa nalo lina wajibu wa kulinda haki kwa maisha ya kila binadamu.

Page 1 of 4