Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Makala

Makala (50)

DAR ES SALAAM

Na Joseph Mihangwa

Ghafla, Afrika imenyamaza kupiga kelele juu ya paa kutangaza sera zake za maendeleo zenye sura ya ubinadamu; sera zilizojaa kurasa za Vyombo vya Habari enzi za uhuru na zama za mageuzi ya uchumi kufuatia uhuru, kwa maandishi makubwa makubwa na kwa wino wa kuangaza:
“Ujamaa” kwa Tanzania; “Zambian Humanism” kwa Zambia; The Common Man’s Charter” – Uganda na “The Guinean Revolution” kwa Guinea ya Rais Ahmed Sekou Toure.

Ujenzi wa Miundo mbinu:
Mwishoni mwa mkutano waliunda Shirika lililoitwa: ‘Inter-Regional Episcopal Board of Eastern Africa (ITEBEA)’. Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Zambia, Fr. Killian Flynn, OFM Cap alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wake wa kwanza na kuanzia mwaka 1964 akawa na ofisi ya kudumu Nairobi, Kenya.
Fr. Killian Flynn ndiye Baba wa Amecea aliyehudumu hadi mwaka 1972. Askofu Mkuu Adam Kozlowiecki, (Baadaye Kadinali) wa Lusaka, Zambia alikuwa Mwenyekiti wake wa kwanza.
Mkutano wa Pili ulikuwa huko Roma: Wakati wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikani (1962 -65) Maaskofu walipata muda wa kufahamiana zaidi na mnamo Novemba 1964 Maaskofu walikutana Roma katika Chuo cha Mt.  Anselmo.

SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Fransisko amesema kuwa mateso na mahangaiko ya mwanadamu, ni zawadi ya matumaini na uaminifu wa Mungu katika Fumbo la Pasaka, na kwamba upendo wa Mungu daima utawaandama waja wake hata wakati wa majaribu na vikwazo katika maisha yao.
Papa alitoa ujumbe huo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya 33 ya Wagonjwa Duniani mwaka 2025, iliyoadhimishwa mjini Vatican, siku ambayo ilianzishwa Mei 13 mwaka 1992, na kuadhimishwa kwa mara ya kwanza kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa Lourdes nchini Ufaransa, mnamo Februari 11 mwaka 1993.
Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa kwa ngazi ya kijimbo yaliyoadhimishwa mwaka huu wa 2025, yananogeshwa na kauli mbiu isemayo, “Na tumaini halitahayarishi, lakini hutuimarisha wakati wa majaribu,” huku Baba Mtakatifu akiwaalika watu wote wa Mungu kuwa Mahujaji wa Matumaini.

DAR ES SALAAM

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mitihani ya kuhitimisha Kidato cha Nne, Tanzania (CSEE) ilifanyika Novemba 11 hadi 29, 2024.
Matokeo yakatangazwa rasimi Januari 23, 2025 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (National Examinations Council of Tanzania: NECTA) Dk. Said Mohammed kupitia hafla na Waandishi wa Habari.
Taarifa iliyotolewa na Mtendaji Mkuu wa NECTA, ilionyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia tatu (3) kutokana na watahiniwa wengi kufaulu.
Hiyo inamaanisha kuwa kati ya watahimiwa 516,695, kati ya hao watahiniwa 477,262 wamefauli kwa madaraja: I, II, III na IV; ikiwa ni ufaulu wa asilimia 92.37 kulinganisha na matokeo ya mitihani ya 2023 yenye ufaulu wa asilimia 89.36 tu.
Kadhalika, ufaulu kwa madaraja ya I, II na III ni watahiniwa 221,952 sawa na asilimia 43, wakati mwaka 2023 walikuwa watahiniwa 197,426 sawa na asilimia 37.4 tu.
Vile vile, matokeo yameonyesha kuwa waliopata daraja la nne (iv) pamoja na waliopata alama (sufuri) wamepungua kulinganisha na matokeo ya mwaka 2023; hivyo kuashiria ongezeko la asilimia 5.6 wa ubora wa kufaulu.
Hata hivyo, Katibu Mtendaji, NECTA alibainisha kuwa kwa matokeo ya mwaka 2024, watahiniwa 67, NECTA imelazimika kufuta matokeo yao kutokana na udanganyifu wakati wakifanya mitihani.

DAR ES SALAAM

Na Alex Kachhelewa

Viongozi wa Matifa ya Afrika Mashariki (East African Community: EAC) na wale wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community: SADC), walikutana hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Mkutano Maalumu kuhusu kusaka suluhu ya mzozo wa vita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Mzozo huo ni kati ya Majeshi ya Serikali ya DRC dhidi ya Vikosi vya Waasi wa Movement For March 23- au maarufu kama M23, wanaosadikiwa kuuteka Mji wa Goma, Mashariki mwa nchi hiyo.
Katika mkutano huo ambapo Rais wa DRC Felix Tshisekedi Shilombo, yeye alishiriki kwa njia ya Mtandao, Viongozi hao walifanya maamuzi yatakayosaidia kurejesha amani  katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), iliyogubikwa na mzozo wa muda mrefu zaidi kuwahi kushuhudiwa.
Mkutano huo uliwakaribisha viongozi hao chini ya Mwenyeji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, uliohudhuriwa na wakuu wa nchi na serikali kutoka mataifa wanachama wa EAC na SADC,  ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa EAC, Rais William Ruto wa Jamhuri ya Kenya, na Mwenyekiti wa SADC, Rais Emmerson Mnangagwa wa  Jamhuri ya Zimbabwe,  hapakuwapo Rais wa Congo DRC Felix Tshisekedi, ambaye alishiriki kwa njia ya mtandao.

MOROGORO

Na Angela Kibwana

Mpendwa msomaji, katika mfululizo wa makala haya ya “Wajibu wa Kanisa kwa Watu Wenye Ulemavu katika Huduma za Kiroho,” Makala yaliyopita yalianza na kuonesha kwamba Kanisa kama Jumuiya ya Waamini wanaomwamini Kristo, msingi wake ni Kristo mwenyewe ((Waefeso 5: 29; Wakolosai, 1: 24 na Wakolosai 2:10).
Katika kulithibitisha hilo, makala hayo yalionesha namna Yesu Kristo mwenyewe alivyokasimisha majukumu yake  ya  kulihudumia Kanisa  la hapa duniani  kupitia Mtume Petro, na msingi huo huo ndiyo asili ya uwepo wa  Kanisa Katoliki ((Mathayo, 16:18).
Makala hayo yalisisitiza kwa kuwa Yesu Kristo ndiye msingi wa Kanisa, Kanisa la duniani halina budi kuyaishi maneno, matendo pamoja na kuubeba wajibu ambao Yesu Kristo aliukasimisha kwa Kanisa la hapa duniani, kama ilivyothibitishwa kupitia Biblia Takatifu na mafundisho ya mama Kanisa.
Makala hayo pia yalisisitiza kuwa Kanisa kama Jumuiya ya Waamini wanaomwamini Kristo, Waamini wake wanayo mahitaji tofauti, ambayo ndio msingi wa ustawi wao, kiroho na kimwili.
Makala hayo yakaangazia ni kwa namna gani Kanisa la hapa duniani linaweza au linayatafsiri mahitaji hayo katika utekelezaji wa majukumu yake kiroho na kimwili, pasipo kumwacha Waamini yeyote ambaye ni mwili na Kielelezo cha Kristo nje ya huduma hizo. “Waamini wenye ulemavu na mahitaji yao ya kiroho, ndio ukawa msingi wa makala hayo.”
Katika makala ya toleo hili, tunaendelea kuangazia hali ya upatikanaji wa huduma za kiroho ndani ya Kanisa Katoliki kwa watu wenye ulemavu, pasipo kuyatenga makundi mengine ya watu wenye ulemavu. Makala haya yatajikita kwa undani zaidi kwenye vikwazo vya mawasiliano kwa kundi la watu wenye ulemavu wa kuongea na kusikia, ili kuweka usawa wa kihuduma kiroho, kiafya,kijamii na kimtazamo pia.
Kutokana na takwimu za matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 nchini Tanzania, kati ya watu wote wenye ulemavu, ulemavu wa kuona,kusikia, kuongea na kutembea ni 6.5% ya Watanzania wote, ambayo ni sawa na jumla ya watu 3,154,514kuanzia umri wa miaka saba (7)na kuendelea pasipo kujali dhehebu au dini ya mhusika, kwa hiyo kutokana na hali zao watu hawa wanahitaji mipango na mikakati maalum ya kuwafikia kwa huduma za kimwili, kijamii, kiafya, kielimu na kiroho pia.
Mpendwa msomaji wa makala haya katika kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata huduma za kiroho leo hii nitaangazia wajibu huo kuanzia katika msingi wa familia na  jumuiya ndogondogo za Kikristu.
Kanisa Katoliki linajengwa kuanzia ngazi ya familia halafu jumuiya  ndogondogo za Kikristu ukiwa ni mwito wa kuwakaribisha watu wote  katika jamii ya waamini wanao mwamini Kristo kuwa Kristo ndiyo  kichwa na mwili wa kanisa
Katika waraka wa Mtakatifu Paulo kwa Wakorintho, tunakumbushwa kuwa mwili wa Kristo una viungo vingi, na kila kimoja kina thamani na nafasi yake (1 Kor. 12:12-27).
Hili ni somo muhimu linalotufundisha kuwa hakuna anayepaswa kuachwa nyuma katika mpango wa wokovu, ikiwa ni pamoja na watu wenye ulemavu kwa ujumla.
Huduma za kiroho kwa watu wenye ulemavu wa kusikia ni mwaliko wa dhati wa kuhakikisha kwamba kundi hili linaloshiriki kikamilifu katika maisha ya kiroho ya jumuiya, ikiwa ni haki yao ya kimsingi kama waamini na wana wa Mungu, ambao walibatizwa na kuwa sehemu ya familia ya Kanisa.
Kwa msingi huu, huduma hizi zinapaswa kuwekwa kama kipaumbele katika jitihada za Kanisa za kujenga jumuiya ndogondogo zinazojumuisha watu wote kuanzia ngazi ya familia bila ubaguzi unaotokana na hali zao.
Jumuiya za Kikristo, hasa ndani ya mazingira ya Parokia, zina jukumu la kutambua kuwa ulemavu wa kusikia,kutembea, kuongea au kuona, siyo kikwazo kwa imani, badala yake, ni fursa ya kuthibitisha wito wa Kanisa wa kuwa sauti ya matumaini na mshikamano kwa kundi hilo.
Maandiko Mtakatifu, mfano Warumi, 15:1, inaonesha jinsi ambavyo wana Kanisa wanavyoitwa kuwa na moyo wa huduma na kusaidia wale walio na udhaifu wa aina yoyote, ikiwemo ulemavu.”Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wa wanyonge, wala si kujipendeza wenyewe.”
Kanisa Katoliki linapofanya sensa kujua idadi ya waamini wake, kadhalika sensa hiyo inapaswa kuwajumuisha watu wenye ulemavu ili kujua idadi yao, taarifa na mahitaji yao ili yatafsiriwe katika huduma za kiroho na huduma nyingine.
Kadhalika, Kanisa lina wajibu wa kuandaa mwongozo kwa watu wenye ulemavu, ambao utaonesha namna ya kuwafikia kuanzia ngazi ya familia, jumuiya Ndogo Ndogo,Parokia na taasisi zake  kwa ujumla, ili waweze kupata huduma za kiroho, ikiwa ni pamoja na kuwalinda kwa sababu Kanisa nalo lina wajibu wa kulinda haki kwa maisha ya kila binadamu.

Mzungu hajakubali kuwa bin-Adam wote ni sawa, wala kwamba wote ni wa baba mmoja,  Adam.
Pamoja na kwamba alituletea Msahafu wa dini – Biblia wenye kusisitiza “upendo,” hiyo ni ghiliba tupu kwa sababu inawabagua wana-Adam kati ya walio wana wa Taifa teule la Mungu (Israeli), na wana wa Mataifa yasiyo teule. Huko ni kukweza ngozi nyeupe.
Kwa kutumia Mungu wa kujiundia (Yahweh) na Msahafu wa kibeberu, wanaidhinishwa kutugeuza watumwa wao, eti kwamba:
“Na wageni watakuwa watumwa wa kulisha mifugo yenu; na wana wa Mataifa watawalimia na kutunza mashamba ya mizabibu yenu”. Huo ndio ubaguzi wa ubeberu wa kimataifa ambao umedumu hadi leo.
Ubaguzi huo kwa misingi ya rangi ulioasisiwa, kusimikwa na kukomazwa Kimataifa na Mjerumani Johann Friedrich Blumenbach (1752 – 1840) unawagawa bin-Adam kwa viwango vya ubora katika makundi sita ya Watu weupe (Coucassians) kama daraja la kwanza; Wamongolia (Mongoloid) daraja la pili; Watu weusi (Ethiopoid); Wamarekani wenye asili ya Kihindi (Red Indians) na Wahimalaya (Malayans) kama daraja la mwisho kwa ubora.
Wamefika mbali kwa kudai kuwa Mwafrika si Mwana-Adam, yaani hakuzaliwa na Adam. Dhana hiyo mpya inayoitwa “Pre-Adamisma inadai kuwa Mwafrika alikuwepo kabla ya kuumbwa Adam na alikuwa kiumbe asiye na roho.
Mwasisi na Mwenezi wa dhana hiyo inayoshika kasi kipindi hiki cha utandawazi ni Mfaransa Isaac La Peyrere (1596 – 1676). Dhana hiyo inapinga usahihi wa Biblia juu ya uumbaji, ikidai kuwa kulikuwa na watu kabla ya kuumbwa kwa Adam na Hawa.
Anasema kwamba kulikuwa na uumbaji mbili za watu: uumbaji wa kwanza ulikuwa wa dunia nzima na Mwafrika kama mtu wa kwanza; na uumbaji wa pili ulihusu Wayahudi kama Taifa ambalo Adam alikuwa mkuu wake.
Anadai kuwa, Mataifa yote hayatokani na Nuhu, kwamba watu wa Mataifa (wasio wa Taifa teule) hawakutenda wala hawahusiki na dhambi ya asili kwa sababu walikuwepo kabla ya Adam, na hivyo hawakupokea “Sheria” au Maagizo ya Mungu, bali ni Adam na uzao wake pekee. Chini ya dhana hiyo Wazungu ni Wana-Adam, na Mwafrika siye.
Dhana hii ina watetezi wengi miongoni mwa Mataifa ya Ulaya: Mathew Fleming Stephenson, katika kitabu chake “Adamic Race” anasema, “Mungu alitumia mamilioni ya miaka kuumba mtu duni (Mwafrika) kabla ya kuumba mtu bora aina ya Mzungu (Caucasian) juu yake”. Wengine, kwa kutaja wanataaluma wachache tu, ni pamoja na John Harris (The Pre-Adamite Race), Isabelle Duncan (Adamites and Pre-Adamites), na wengine.
Iwe ni kwa mtizamo wa dhana ya “Pre-Adamite”, “Uumbaji” au “Mageuko” (evolution), hakuna ubishi mpaka sasa, kwamba binadamu (mtu) wa kwanza aliishi Loliondo/Ngorongoro zaidi kabla ya mwaka 10,000, Kabla ya Vizazi (KV) ambao ndio mwaka unaosemekana Adam aliumbwa.
Ustaarabu wa mtu huyu ulianza na shughuli za Kilimo, ufugaji, ibada na makazi eneo ambalo sasa linajulikana kama Nubia, au Sudan Kaskazini. Utawala wa kwanza ulianzia Ta-Seti eneo hilo; watu hawa walijulikana kama “Anu”.
Nchi waliyokalia ilijulikana kwa majina mengi, kama vile, Nubia, Kermet, Kush, Ethiopia au Egypt (Misri) na Mji Mkuu ulikuwa Kerma. Nubia imetajwa kwenye Biblia, Kitabu cha Mwanzo 2:11 kama nchi ya Havillah.
Ni Ufalme ulioundwa na watu weusi kutoka eneo la Maziwa Makuu (ANU) miaka ya 5900 Kabla ya Vizazi (KV) na maelfu ya miaka kabla ya Kristo (KK). Hapa ndipo Gharika (la Nuhu) lilipowakuta watu hawa, wakaangamia isipokuwa mtu mmoja – Nuhu na wanae watatu – Yafeti, Shem na Hamu. Hiyo ilikuwa Mwaka 5000 KK. SOMA ZAIDI KWA KUNUNUA TUMAINI LETU.

VATICAN

Na Angela Rwezaura

Kitabu hiki kinapatikana katika lugha ya Kijerumani, ambacho kinasimulia historia ya Ukristo katika dunia.
Kitabu hicho kimeeleza kwa kina kuhusu safari za Papa Fransisko alizotimiza nchini Iraq mwaka 2021, na kuhusu diplomasia ya Vatican katika nchini Iraq.
Matthias Kopp ni mwandishi na Mtaalimumgu ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Baraza la Maaskofu nchini Ujerumani.
Desemba mwaka 2024, Baba Mtakatifu Fransisko alimteua kuwa mshauri wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano.
Dibaji ya Papa Fransisko:
Kwa shukrani ya kumbukumbu ya ziara yangu ya kitume nchini Iraq, ambaye licha ya janga la Uviko 19, na mashaka ya usalama, nilitimiza ziara hiyo kunako Machi 2021 ili kueleza kwa Wakristo na watu wote wenye mapenzi mema katika Nchi hiyo, upendo wangu na mshikamano wangu.
Nchi hiyo inachukua nafasi daima na kila wakati katika moyo wangu katika sala.
Licha ya matatizo mengi ambayo Iraq inakabiliana nayo, ninatazama  Nchi hiyo kwa matumaini, kwa sababu inayo nguvu maalum.
Nguvu hiyo awali ya yote, ni watu hao hao  nchini Iraq, wale wote wanaoshiriki ujenzi wa jamii ya raia, ambao wanahamasisha demokrasia katika Nchi na ambao wanajibidiisha kwa ajili ya mazungumzo ya wazi na ya kweli kati ya dini.
Kwa njia hiyo, ziara yangu kwa Mkuu Ayatollah wa Najaf, Sayyid Ali Al-Sistani, ilikuwa muhimu na ya maana. Mkutano ule ulikuwa unataka kuwa alama kwa ulimwengu wote kwamba : kufanya vurugu katika jina la dini, ni matumizi mabaya ya dini.
Kama watu wa dini, tunawajibika kuelekeza amani, na lazima kuiishi, kufundisha na kuieneza amani hii.
Katika muktadha huo ninafikiri hata ziara yangu huko Ur, Kusini mwa Iraq, kwa maana kama wawakilishi wa dini mbali mbali, tulizungumza na kusali pamoja, chini ya maelfu na maelefu ya nyota zilizotazamwa na  baba yetu Ibrahimu alipoinua macho yake angani.
Urithi wa utajiri katika historia ya Bimillenaria del Cristianesimo kisayansi, karibu haijavumbuliwa.
Ninafikiri shule za kiteknolojia za Wakristo wa kwanza wa Mesopotamia, uwepo wa amani kwa mamia ya miaka kati ya Wakristo, na Waislamu kati ya Eufrate na Tigri, na tamaduni mbali mbali za ibada ya Kikatoliki katika kanda.
Aidha, mapambano kati ya Madhehebu ya Kikristo, katika nyakati za mateso mwanzoni mwa karne ya 20,  na visasi vingine vya kisiasa  na kwa mwendelezo wa uwepo wa Kikristo, hadi sasa.
Haya yote yanapendeza kwamba katika kazi ya Matthias Kopp, urithi huu na historia hiyo inakuja kuonesha katika muktadha wao mafunzo ya kidini, katika wingi na kwa kuzingatia fasihi nzito.
Mwandishi kwa namna ya pekee anaweka umakini katika jitihada za Kikanisa nchini Iraq na katika shughuli za Vatican,  kwa wawakilishi wake wa kidiplomasia, ambao wanamulika uhasishaji mwingi wa Mapapa kwa ajili ya Iraq na Wakristo wanaoishi ndani mwake.
Kwa njia hiyo, imezaliwa zawadi kama anavyoandika mwandishi mwenyewe, kwa Wakristo nchini Iraq, ambao ninawatia moyo kujihusisha kwa kina zaidi utajiri wao mkubwa wa kihistoria na kudumisha uhai wa urithi wao:
Kwa wakati ujao ambao hata leo hii unahatarishwa kwa sababu ya uhamiaji na ukosefu wa uhakika kisiasa.
Ninataka kueleza kwa kina na kuamini kwamba  haiwezekani kufikiria Iraq bila Wakristo, kwa sababu pamoja na Waamini wengine wote wanawakilisha kwa nguvu utambuzi maalum wa Nchi, ambao tangu karne za kwanza pamekuwa ni mahali pa kuishi, kuvumiliana na kukubaliana wao kwa wao.
Kwa hiyo, Iraq inaweza na kwa watu wake, kuonekana, katika Mashariki ya Kati na katika Ulimwengu kwamba inawezakana kuishi pamoja kwa amani, licha ya tofauti zao.

MOROGORO

Na Angela Kibwana

Katika nyumba moja huko Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro, Lucy Patrick (siyo jina lake halisi), mfanyakazi wa majumbani, anajikuta akifanya kazi kwa saa 18 kila siku, bila kupumzika.
Hajawahi kulipwa mshahara wake wa miezi mitatu, sasa, ambapo malengo yake ya awali ilikuwa ni kujiongezea kipato kusaidia familia yake na mara nyingi anakula mabaki ya chakula cha familia.
Kwa muda mrefu, sauti yake haikusikika, lakini sasa, juhudi za Chama cha Wafanyakazi Wakatoliki (CWW) zimeanza kuleta matumaini kwake baada ya kutoa mafunzo ya kuboresha mahusiano kati ya waajiri na wafanyakazi.”
Wafanyakazi wa majumbani wanakabiliwa na changamoto nyingi, zikiwemo kutolipwa mishahara inayoendana na kazi zao, kunyimwa chakula, kupigwa, na kudhulumiwa haki zao za msingi.
Aidha, wengi wao hawana mikataba ya ajira, jambo linalowafanya kukosa ulinzi wa kisheria, hivyo wanajikuta wakifanya kazi kwa mazingira magumu bila msaada wowote wa kisheria au kijamii.
Victor Mackyao, mwanasheria na mwezeshaji wa mafunzo yaliyoandaliwa na (Chama cha Wafanyakazi Majumbani: CWM), anasema kuwa wafanyakazi wa majumbani, mara nyingi hawajui sheria za ajira, wala haki zao za msingi.
Wafanyakazi wa majumbani wengi wao ukiwauliza wanasema wanakumbana na vipigo, wananyanyapaliwa, wanatengwa,wanateswa maeneo wanayoishi siyo rafiki, wanakosa fursa ya matibabu wanapougua, wengine kukosa chombo maalum cha kuwasemea” alisema Mackyao.
Alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwaelimisha wafanyakazi hao wa majumbani ili kujua nini maana ya haki, lakini pia waajiri watambue wajibu wao ni upi kwa wafanyakazi hao ili kujenga usawa katika makundi yote mawili.
Alifafanua kuwa moja ya changamoto zinazochangia wafanyakazi hao wa majumbani kukosa hali zao msingi ni kutokana na vyombo au mamlaka mbalimbali ambazo zina dhamana ya kuwasimamia haki zao, kutowafikia kwa wakati kwa sababu wafanyakazi hao wanatoka kwa waajiri tofauti na maeneo tofauti.
Alisema kuwa tangu Cwm ilipoanza kutoa mafunzo hayo wamebaini kwamba baadhi ya wafanyakazi wa majumbani wanapohojiwa, ambao wanakaa kwao nje ya mwajiri wake, baada ya kuulizwa, wamedai kwamba wanalipwa kiasi cha shilingi elfu 30 au 50, wakati sheria inamtaka alipwe kuanzia 120,000/=.
“Wafanyakazi ambao wanakaa kwa waajiri wao sheria inawataka walipwe shilingi elfu 60, lakini hawalipwi kwa mujibu wa sheria. Kwa hiyo changamoto hizo ndizo zilizotufanya tuweze kupita na kutoa elimu kwa jamii lakini tutoe rai na tuviombe vyombo vyenye mamlaka ya kushughulikia masuala ya wafanyakazi wa majumbani, waweze kutumia mbinu kama tunazotumia sisi, ili waweze kuwafikia kujua changamoto zao na kazitatua wasikae tu mijini.”
Alisema kwamba kazi za majumbani si rahisi, na sheria inakataza ajira ya watoto katika kazi hizi kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009, Sura ya 13, Hata hivyo, bado kuna ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu,
Kwa kutambua changamoto hizi, CWM jimbo la Morogoro limeanza kutoa mafunzo kwa waajiri na wafanyakazi wa majumbani katika Dekania ya Kilosa.
Kwa mujibu wa CWM, kati ya wafanyakazi 161 waliopata mafunzo, asilimia 70 hawakuwa wanajua haki zao za msingi, na wala hawajui lolote kuhusu haki yao ya kuwa na mikataba ya kazi, ili kulinda haki zao.
Lengo ni kujenga mahusiano bora kati ya waajiri na wafanyakazi wa majumbani, kwa kuhakikisha haki na wajibu vinazingatiwa pande zote mbili.
Mratibu wa CWM, Edson Yeyeye, alisema kuwa mafunzo haya yalianza mwishoni mwa mwaka 2024 katika Dekania za Kihonda, Morogoro mjini, na sasa yamefikia Kilosa. Tayari wafanyakazi 161 na waajiri 62 wamepatiwa mafunzo hayo, huku Viongozi wa Dini na serikali 27 wakiungwa mkono katika juhudi hizi.
“Lengo letu ni kuhakikisha kila mfanyakazi wa majumbani anapata elimu ya haki zake na waajiri wanajua wajibu wao,” alisema Yeyeye.
Bahati Ramadhani, mmoja wa waajiri walioshiriki mafunzo hayo, alisema, “Ni muhimu elimu hii kufika vijijini kwa sababu huko ndiko wafanyakazi wengi wa majumbani wanatoka, Wengi wanapokuja mjini, wanakosa haki zao kwa sababu hawana mikataba wala hawajui sheria”.
Maria Chalalika, mshiriki mwingine, aliongeza kuwa kunahitajika kuundwa vyombo maalum vya kushughulikia haki za wafanyakazi wa majumbani, hasa kwa wale wanaopelekwa nje ya nchi, bila kujua wanachokwenda kukifanya
Kwa upande wake, Hosea Nikodemas Mgunda, Mwenyekiti wa Mtaa wa Mlimani Boma, aliwapongeza CWM kwa juhudi zao za kutoa elimu hiyo kwa jamii, ili haki za wafanyakazi wa nyumbani ziweze kulindwa na kuthaminiwa.
“Wafanyakazi wa majumbani wanapitia madhila mengi, hivyo tunahitaji kuwa na chama chao maalum ili kuwatetea na kuhakikisha wanapata haki zao.ili kupunguza vitendo vya ukatili miongoni mwao
Hata hivyo, Mgunda aliahidi kutumia mikutano yake ya kijamii kutoa elimu kuhusu haki za wafanyakazi wa majumbani ambavyo anatarajia kufanya kuanzia tarehe mosi Februari mwaka huu 2025.
Mafunzo haya yameongeza uelewa miongoni mwa wafanyakazi na waajiri, ambapo wengi wao sasa wanatambua umuhimu wa mikataba ya ajira, haki ya likizo, na mishahara inayotambulika kisheria.
Hata hivyo, changamoto bado zipo, hasa katika kuwafikia wafanyakazi walioko maeneo ya vijijini, na wale wanaofanyiwa ukatili wa kimya kimya.
Washiriki wa mafunzo hayo walipendekeza kuundwa kwa vyombo maalum vya kushughulikia haki za wafanyakazi wa majumbani, Kuongeza uhamasishaji kuhusu sheria za kazi vijijini na mijini, Kuwapatia wafanyakazi wa majumbani elimu ya malezi na maadili, kwani mara nyingi wao ndio walezi wa karibu wa watoto katika familia nyingi
Mratibu wa CWM, Edson Yeyeye, alisisitiza kuwa jitihada hizi zitaendelea hadi sauti za wafanyakazi wa majumbani zisikike na kuheshimiwa kikamilifu.
 “Ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha haki na heshima kwa kila mfanyakazi wa majumbani, kwani mchango wao katika familia na jamii hauwezi kupuuzwa,” alisema Yeyeye.
Sasa ni wakati wa jamii kushirikiana ili kuhakikisha kwamba kila mfanyakazi wa majumbani anapata heshima anayostahili, na mahusiano ya kazi yanajengwa kwa misingi ya haki na usawa.
Nashauri wafanyakazi wa majumbani wapewe elimu ya malezi na maadili mara kwa mara, kwa sababu katika nyumba nyingi za mijini na hata vijijini, sauti ya mfanyakazi wa majumbani ndiyo inayopokelewa kwanza asubuhi, ikiongoza familia katika maandalizi ya siku.
Wakati mwingine, wao ndio waangalizi wa karibu wa watoto; wanahakikisha wanakula, wanavaa, na mara nyingi hata wanasaidia katika kujenga maadili ya msingi kwa watoto hao, ikiwa ni pamoja na kuwafundisha kusoma au kuandika. Hata hivyo, mchango huu wa kipekee mara nyingi unapuuzwa, ukifichwa na mwanga wa jukumu lao la kazi za nyumbani.

Dar es Salaam

Na Pd. Richard Mjigwa- C.PP.S

Mwenyeheri Giovanni Merlini ni Mtume mwenye ari na mwamko wa Fumbo la Pasaka ya Kristo linaloleta wokovu, shuhuda, amini wa Injili na mshauri mwenye busara.
Hayo yamo katika Waraka wake wa Kitume wa Baba Mtakatifu Fransisko wa kumtangaza Mwenyeheri huyo, ambaye Sikukuu yake itaadhimishwa kila mwaka Januari 12.
Mwenyeheri Giovanni (pichani) yeye alikuwa ni mhubiri mahiri; Mshauri mwenye busara na mjumbe wa matumaini na amani katika Kristo Yesu.
Katika maadhimisho ya Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana, Kristo Yesu, Nafsi ya Pili ya Fumbo la Utatu Mtakatifu anajifunua, kwa watu wake waliokuwa wamepokea Ubatizo wa toba na maondoleo ya dhambi.
Hii ni siku ya Ufunuo wa Fumbo la Utatu Mtakatifu, yaani Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu. “Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu ninayependezwa naye” (Mt, 3:13-17, Mk, 1:9-11, Lk, 3:21-22). Ni tukio linalotakatifuza maji yote ya Ubatizo, na umuhimu wa maisha ya sala. Rej Lk, 3:21 na katika kusali, Kristo Yesu anawafundisha Wafuasi wake kusali. Rej KKK 2607.
Huu ni mwaliko kwa Waamini kutafakri ufunuo wa Sura na Sauti ya Mungu. Ubatizo wa Bwana unahitimisha maadhimisho ya Kipindi cha Noeli, Mwanzo wa: maisha na Utume wa Kristo na ni siku maalum ya Ubatizo kwa watoto wachanga, changamoto na mwaliko kwa wazazi na walezi kuwarithisha watoto wao zawadi ya imani.
Ni katika muktadha wa maadhimisho ya Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana, Kardinali Marcello Semeraro, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Kuwatangaza Waamini kuwa Wenyeheri na Watakatifu kwa niaba ya Baba Mtakatifu Fransisko, Dominika Januari 12, 2025 amemtangaza Mtumishi wa Mungu Giovanni Merlini, kuwa ni Mwenyeheri na ambaye alizaliwa tarehe 28 Agosti, 1795 huko Spoleto, Perugia nchini Italia.
Akapewa daraja Takatifu la Upadri Desemba 19, 1818. Agosti 15, 1820 akajiunga na Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu, lililokuwa limeanzishwa na Mtakatifu Gaspari del Bufalo Agosti 15, 1815. Alijiunga na Shirika baada ya kuvutiwa sana na mahubiri yaliyotolewa na Mtakatifu Gaspari, kuhusu Fumbo la Ukombozi chemchemi ya upendo wa kimisionari.
Kumbe, Tasaufi ya Damu Azizi ya Yesu ni msaada kwa kila Mkristo kwa kuwa Damu ya Kristo ndiyo msingi wa ukombozi wa mwanadamu, na ni kielelezo cha juu kabisa cha upendo wa Mungu kwa watu wote.
Tasaufi hii ina msingi wake katika, na Neno la Mungu na katika Fumbo la Ekaristi Takatifu, ambalo ndilo chanzo na kilele cha maisha ya kila siku ya Kanisa, na maisha ya Mkristo kwa jumla.
Tena Ekaristi Takatifu ni ujumuisho mzima wa Imani ya Kikristo, na ni msingi wa mitazamo sahihi ya Kikristo. Rej KKK 1324 na 1327. Tasaufi ya Damu Azizi ya Yesu, Agano Jipya na la Milele, ikawa ni msingi wa maisha na sadaka, kwa bidii ya kutafakari na shauku ya kitume “cum ardore contemplativo et passione apostolica.”
Mwenyeheri Giovanni Merlini aliishi nyakati za Mapinduzi ya Napoleone, wakati wa mchakato wa mafundisho tanzu ya Kanisa. Papa Pio IX Desemba 8, 1854 akatangaza rasmi kwamba, Mwenyeheri kabisa Bikira Maria, tangu nukta ya kutungwa kwake mimba, kwa neema na upendeleo wa pekee wa Mwenyezi Mungu, kwa kutazamia mastahili ya Kristo Yesu, Mwokozi wa wanadamu wote, alikingiwa na kila doa la dhambi ya asili.
Mwenyeheri Giovanni Merlini akatangaza na kushuhudia tunu msingi za Kiinjili katika maisha ya kila siku kwa kutambua mbegu za Ufalme wa Mungu, na hivyo akajipambanua kuwa ni chombo cha huruma ya Mungu na amani; na shuhuda wa matumaini yasiyotahalisha. “Spes non confundit.”
Kati ya Mwaka 1847 hadi 1873 aliteuliwa kuwa ni Mkuu wa tatu wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu. Kama kiongozi, akaonesha utakatifu wa maisha, udugu, ari na mwamko wa kimisionari; ukaribu na majadiliano katika ukweli na uwazi; kupima mang’amuzi ya maisha na utume wa Kimisionari mbele ya Msalaba. Ni katika wakati wa uongozi wake, Shirika likapanuka na kuenea nje ya mipaka ya Italia hadi Kaskazini mwa Ulaya na nchini Marekani.
Katika maisha na utume wake alibahatika kuwa ni kiongozi wa maisha ya kiroho kwa Mtakatifu Maria De Mattias, utume alioutekeleza kwa kipindi cha miaka arobaini na miwili.
Akasaidia kujenga na kuwaimarisha Masista Waabuduo Damu Takatifu ya Yesu, ASC. Katika mashauri yake alikazia: majadiliano katika utu, heshima na ukuaji wa maisha ya kiroho, daima wakitafuta mapenzi ya Mungu.
Mwenyeheri Giovanni Merlini, alisaidiana na Mtakatifu Gaspari del Bufalo kupyaisha maisha ya Waamini na Makleri kwa namna ya pekee kama yaliyoasisiwa na Papa Pio VII (1800-1823: wa 251) na Pio 1X kwa njia ya mahubiri, mafungo, na hata wakati mwingine akahatarisha maisha yake kwa kutangaza Injili miongoni mwa majangili, kielelezo cha mtume wa msamaha unaobubujika kutoka katika Damu Azizi ya Kristo.
Fumbo la Pasaka ni kiini cha maisha na utume wa Kanisa na kwamba Waraka wa Kitume wa “Amantissimus human” wa Mwaka 1862 ulionesha umuhimu wa Tasaufi ya Damu Azizi ya Kristo, na kunako mwaka 1849 katika Waraka wa Kitume wa “Redempti sumus,” Sikukuu ya Damu Azizi ya Yesu, ikatangazwa kuwa ni Sikukuu kwa Kanisa zima. Mwenyeheri Giovanni Merlini akaitupa mkono dunia tarehe 12 Januari 1873 kwa ajali.
Tarehe 10 Mei 1973, Baraza la Kipapa la Kuwatangaza Waamini kuwa Wenyeheri na Watakatifu, likamtangaza kuwa ni Mtumishi wa Mungu. Tarehe 23 Mei 2024 Baba Mtakatifu Fransisko akaruhusu atangazwe kuwa ni Mwenyeheri. Katika Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana, Dominika tarehe 12 Januari 2025 akatangazwa kuwa ni Mwenyeheri.
Jumamosi tarehe 11 Januari 2025, kukafanyika Ibada ya mkesha wa nguvu ukiongozwa na AskofuVincenzo Viva wa Jimbo Katoliki Albano, nchini Italia. Misa ya shukrani imeadhimishwa Jumatatu, tarehe 13 Januari 2025 kwa kuongozwa na Askofu Mkuu Renato Boccardo wa Jimbo Kuu la Spoleto, Italia.
Baba Mtakatifu katika Waraka wake wa Kitume wa kumtangaza Mtumishi wa Mungu Giovanni Merlini kuwa ni Mwenyeheri, anasema, kwa hakika alikuwa ni Mtume mwenye ari na mwamko wa Fumbo la Pasaka ya Kristo linaloleta wokovu, shuhuda amini wa Injili na mshauri mwenye busara.
Sikukuu yake itakuwa inaadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Januari. Baba Mtakatifu Fransisko wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Sikukuu ya Ubatizo wa Bwana alisema, Giovanni Merlini, Padri Mmisionari wa Shirika la Damu Azizi, alijisadaka bila ya kujibakiza kwa ajili ya utume kwa watu wa Mungu, akawa mshauri mwenye busara kwa roho nyingi, na mjumbe wa amani.

Page 1 of 4