Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Makala

Makala (73)

DAR ES SALAAM

Na Edvesta Tarimo

Katika jamii nyingi, viatu vyenye kisigino kirefu vimejijengea nafasi ya kipekee kama alama ya urembo, hesima, hadhi na kujiamini kwa mwanamke. Kwa muda mrefu, kuvaa kiatu chenye kisigino kirefu kumechukuliwa kama sehemu ya mwonekano wa kitaaluma na kifahari, hususani katika mazingira ya kazi na hafla rasmi. Hata hivyo, nyuma ya mvuto huo wa nje, tafiti za kisayansi zinaendelea kuibua hoja nzito, kuhusu gharama ya kiafya inayoweza kujificha kwenye mtindo huu.
Kihistoria, kumbukumbu zinaonesha kuwa viatu vyenye kisigino havikuanza kama vazi la wanawake. Tafiti za kihistoria za mitindo zilizokusanywa na Fashion Institute of Technology, zinaonesha kuwa takribani mwaka 1000 BK, wanaume wa Uajemi waliokuwa wakipanda farasi, walitumia viatu vyenye kisigino, ili kuimarisha mshikamano wa mguu na farasi.

DAR ES SALAAM

Na David Mpangile

Ili kutimiza wajibu wao Wakristo, ikiwa ni sehemu ya matunda ya ubatizo, Waamini hujaliwa karama mbalimbali. 
Mafundisho ya Kanisa yanasisitiza kuwa karama yoyote itokayo kwa Roho Mtakatifu, yafaa katika kumsaidia mwamini katika safari yake ya kuutafuta utakatifu. 
Karama hiyo pia inaweza kuchangia katika ustawi wa Kanisa, na ni msaada kwa ndugu wengine katika Kristo. Hivyo ni makosa kuacha kuitumia. Hata hivyo, bado kuna kishawishi cha Walei wengi kushindwa kutumia vipawa walivyo navyo, kwa sababu wanatafsiri kwamba karama ni zile tu zinazohesabika kuwa kubwa, kama vile kutenda miujiza na kunena kwa lugha.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya Papa Gregori Mkuu, ambaye alikuwa Baba wa Kanisa wa mwisho na kiungo kati ya dola ya Kirumi ya zamani na ulimwengu mpya wa kishenzi. Leo tunawaletea historia ya maisha ya Mtume Muhammad na mwanzo wa Uislamu.  Sasa endelea…

Maisha ya Muhammad:
Katika kipindi cha ghasia na uvamizi wa Ulaya, ndipo Muhammad alizaliwa mwaka 570. Wazazi wake walikufa akabakia yatima na akalelewa na baba mdogo. Akiwa kijana alifanya kazi katika misafara ya ngamia ya mjane mmoja tajiri aliyeitwa Khadija.
Alifanya kazi vizuri, hata baadaye Khadija alimfanya Muhammad kuwa Mkuu wa misafara yake. Muhammad akiwa na umri wa miaka 25, alimwoa mwajiri wake Khadija aliyekuwa na miaka 35. Ndoa yao ilikuwa nzuri na ilidumu.

Mwanza

Na Paul Charles Mabuga

Simulizi ya Amos Katama (sasa marehemu) ni kioo cha maumivu ya kizazi kizima. Kauli yake kuhusu “soli ya 20 ya kiatu kuchakaa akitafuta ajira” si dhihaka, bali ni kovu la kisaikolojia linalowatafuna wahitimu wengi. Amos aliondoka duniani akiwa na Shahada ya Uandishi wa Habari mkononi, lakini mfuko ukiwa mtupu. Hali hii inatufanya tujiulize: Je, vyuo vyetu vinazalisha wasomi au vinazalisha watafuta kazi waliofungwa pingu za kifikra?

Na  Askofu Mstaafu Method Kilaini

Wahuni:    
Wahuni walikuwa wapiganaji wakali sana, na ndio walioleta matatizo yaliyozusha uvamizi. Wahuni walikuwa watu wa Mashariki ya mbali (Mongoliani, waasia wa ngozi ya njano). Wahuni walikuwa wachungaji wakiishi Kaskazini ya Milima ya Himalaya. 

Malisho yalipoisha, hawa wapanda farasi, walianza kuvamia nchi nyingine. Mwaka 200 Baada ya Kristo (BK), walikwea ukuta wakaivamia China na kusambaratisha himaya yake, na tangu hapo ikawa nyakati za giza kwa miaka 400 iliyofuata kwa China. 

MWANZA

Na Paul Mabuga

Mjadala wa “Uswahili ni nini”, uliibuliwa hivi karibuni na mchambuzi Maggid Mjengwa, akirejea fikra za Jenerali Twaha Ulimwengu na marehemu Edwin Mtei. 
Swali hili limezua taharuki chanya: Je, Mswahili ni nani katika ulimwengu wa leo? Je, bado ni yule “muongo muongo” aliyemchukiza Mtei, au ni utambulisho uliopata sura mpya, kuanzia mitaa ya Dar es Salaam hadi jijini Berlin?
Jenerali Ulimwengu, akizungumza hivi karibuni, katika makiwa ya marehemu Edwin Mtei, alifungua ukurasa wa kumbukumbu uliosisimua wengi. 
Alieleza kuwa Mzee Mtei alikuwa na msimamo usioyumba, dhidi ya kile alichokiita “Uswahili.” Katika muktadha wa kujiuzulu kwake Uwaziri, Mtei aliamini kuwa mfumo wa “Uswahili”, ulikuwa kikwazo kwa uadilifu wa kitaifa.

Na Mwandishi Wetu

Katika makala haya kuhusu Ubatizo wa Bwana, Mwadhama Protace Kardinali Rugambwa katika mahubiri yake, ametumia fursa hii kufafanua alama muhimu, zilizojionesha wakati Kristo Yesu alipobatizwa mtoni Yordani.

Anasema kwamba alama ya kwanza ni Maji: Alama ya kifo na uhai; Mbingu zikamfunukia, Roho Mtakatifu akashuka juu yake kama hua; Alama ya pili ni kufunguka kwa mbingu; Alama ya mabadiliko ya ndani ya mwanadamu, mbele ya Mwenyezi Mungu; Alama ya tatu ni Roho Mtakatifu aliyemshukia Kristo Yesu na sauti ya Baba wa milele ikasikika: Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu.

Ubatizo ni sakramenti inayotuingiza katika Ukristo, ni sakramenti inayotuondolea dhambi ya asili na adhabu zake zote. Ni kwa njia ya Ubatizo tunazaliwa upya kwa maji na Roho Mtakatifu, na hivyo tunakuwa ni watoto wa Mungu na wa Kanisa.

Na Dkt. Felician B. Kilahama

Namshukuru Mwenyezi Mungu aliye mwingi wa rehema, aliyeumba wanadamu kwa sura na mfano wake. Hili ni “wazo mbadala”, ikimaanisha kwamba kuna kinachotakiwa kufanyika, lakini katika harakati za utekelezaji likajitokeza ‘wazo mbadala’.
Uchaguzi Mkuu ulifanyika Oktoba 29, 2025, na aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, akatangazwa mshindi na kuapishwa rasmi Jumatatu, Novemba 3, 2025.
Baada ya zoezi hilo kukamilika, Rais aliunda Baraza la Mawaziri, ambalo pamoja na Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Viongozi wakuu wa Halmashauri husika, kwa pamoja inakuwa Serikali inayoongozwa na Rais.
Wakati wa kampeni za uchaguzi, kuna sehemu ambazo wananchi waliomba serikali itakayoundwa, kuanzisha wilaya na halmashauri mpya, ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma wanazohitaji, ikiwemo kutatuliwa kero haraka iwapo ofisi husika zitakuwa karibu.

Dar es Salaam

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mapokeo ya kihistoria tangu miaka ya 1880, yanathibitisha kwamba baadhi ya mataifa barani Ulaya mathalani, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji na Hispania, yaliweza kufika barani Afrika.
Hivyo, 1884 kukafanyika kikao maalumu jijini Berlin-Ujerumani, kwa lengo mahususi kugawana maeneo kuitawala Afrika.
Kwa upande wa Afrika-Mashariki, Wajerumani wakatawala “Tanganyika” na wakaweza kufika maeneo ya Iringa, ambako Hifadhi-Ruaha inapatikana. Wakiwa huko waliona sehemu imesheheni rasilimali nyingi za wanyamapori, na kuifananisha na “Bustani ya Edeni”.
Kiuhalisia Ruaha kuna urithi wa aina yake, mathalani milima na mabonde pamoja na rasilimali-misitu aina ya miombo, misitu inayostawi kandokando ya mito, na Mto Ruaha-Mkuu. Mto huu ni msaada mkubwa aina yake, ikiwemo wanyamapori wanaoishi kwenye hifadhi ya Ruaha.

MWANZA

Na Paul Mabuga

Hebu vuta picha: Zamani kijana wa Kitanzania hakukurupuka tu kuitwa mzazi. Kulikuwa na mifumo madhubuti ya Jando, Unyago, na yale mafunzo ya kando ya moto kutoka kwa babu na bibi, yaliyomjenga mtu kifikra na kihisia. 
Lakini leo, “moto” pekee unaowaunguza vijana wetu ni wa data za simu, na mianga ya mitandao ya kijamii. Wakati mifumo hiyo ya kijadi ikipumzika kwenye makaburi ya historia, tunapaswa kujiuliza kwa uchungu: Je, vijana wetu wanajifunza wapi kuwa wazazi?

Page 1 of 6