DAR ES SALAAM
Na Mwandishi wetu
Siku chache baada ya kutolewa katika michuano ya kimataifa, timu ya soka ya Singida Black Stars, imesema kuwa hasira zake itazimalizia katika mechi za ndani, ikiwemo Ligi Kuu Tanzania Bara.
Singida imekosa nafasi ya kutinga hatua ya robo fainali ya Shirikisho Afrika, baada ya kukusanya pointi ambazo haziwezi kumuweka katika nafasi mbili za juu.