Mwanza
Na Paul Charles Mabuga
Simulizi ya Amos Katama (sasa marehemu) ni kioo cha maumivu ya kizazi kizima. Kauli yake kuhusu “soli ya 20 ya kiatu kuchakaa akitafuta ajira” si dhihaka, bali ni kovu la kisaikolojia linalowatafuna wahitimu wengi. Amos aliondoka duniani akiwa na Shahada ya Uandishi wa Habari mkononi, lakini mfuko ukiwa mtupu. Hali hii inatufanya tujiulize: Je, vyuo vyetu vinazalisha wasomi au vinazalisha watafuta kazi waliofungwa pingu za kifikra?