DAR ES SALAAM
Na David Mpangile
Ili kutimiza wajibu wao Wakristo, ikiwa ni sehemu ya matunda ya ubatizo, Waamini hujaliwa karama mbalimbali.
Mafundisho ya Kanisa yanasisitiza kuwa karama yoyote itokayo kwa Roho Mtakatifu, yafaa katika kumsaidia mwamini katika safari yake ya kuutafuta utakatifu.
Karama hiyo pia inaweza kuchangia katika ustawi wa Kanisa, na ni msaada kwa ndugu wengine katika Kristo. Hivyo ni makosa kuacha kuitumia. Hata hivyo, bado kuna kishawishi cha Walei wengi kushindwa kutumia vipawa walivyo navyo, kwa sababu wanatafsiri kwamba karama ni zile tu zinazohesabika kuwa kubwa, kama vile kutenda miujiza na kunena kwa lugha.