MADRID, Hispania
Baada ya zaidi ya miaka 14 huko Atletico Madrid, kocha Diego Simeone ameanza kufikiria maisha mapya nje ya klabu hiyo, huku maswali kwa mashabiki, yakiwa mengi kuhusu wapi atakapokwenda.
Tangu alipowasili kama Meneja mwaka wa 2011, Diego Simeone ameibadilisha Atletico Madrid, kutoka timu isiyofanya vizuri, ikipambana kupata uthabiti ndani na barani Ulaya, na kuwa timu yenye ushindi mkubwa, na kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya.