Print this page

Wakurugenzi vyombo vya habari vya Kanisa wateta na wawakilishi Vatican

Na Mwandishi wetu

Wakurugenzi na wawakilishi wa vyombo vya habari vya Kanisa nchini Tanzania wamekutana na wawakilishi wa Kurugenzi ya Mawasilano ya Vatican na kujadili kuhusu ushirikiano wa pamoja kwa lengo la kukuza na kuimarisha mawasiliano kati ya Kanisa Katoliki ulimwenguni na jamii.
Kikao hicho kimefanyika hivi karibuni katika Ubalozi wa Vatican nchini uliopo Jijini Dar es Salaam.
Akifungua kikao hicho Mkurugenzi wa Mawasilano  wa Baraza la Maaskofu Katoliki nchini (TEC)  Padri Faustine Furaha ameeleza namna vyombo vya habari vya kanisa vinavyofanyakazi hapa nchini.
Alisema kupitia vyombo hivyo Kanisa limefanikiwa kuwafikia zaidi ya waamini Mmilioni 30 na kuwapatia ujumbe wa Injili.
Kupitia kikao hicho wawakilishi hao kutoka Vatican walieleza miradi ya kuboresha ushirikiano na mawasiliano baina ya Kanisa Katoliki na jamii ikihusisha vijana wenye umri usiozidi miaka 35.
Walieleza kuwa wahusika katika mradi huo mradi huo watatakiwa kuwa Shahada ya Mawasiliano,  wafanyakazi wa taasisi ya Kanisa Katoliki na wenye uwezo wa kuzungumza lugha ya Kiingereza.
Wameutaja mradi wa pili kuwa ni Mafunzo ya Muda wa miezi mitatu kwa Masista wa Kanisa Katoliki ulimwenguni ambao wana taaluma ya Mawasilano, wenye uzoefu wa kazi kwenye radio, Televisheni, gazeti na mitandao ya kijamii.
Vyombo vya mawasiliano vilivyoshiriki katika kikao hicho ni pamoja na Kurugenzi ya mMawasilino TEC, Tumaini Media, Jugo media, Radio Maria, Radio Habari Njema Mbulu, na gazeti la Kiongozi.

Rate this item
(0 votes)
Japhet