DAR ES SALAAM
Na Remigius MMavele
Madilu System alikuwa mwanamuziki maarufu wa Kongo anayejulikana kwa ustadi wake wa hali ya juu wa sauti ambaye alipata umaarufu hasa kama mmoja wa waimbaji wakuu katika kundi la TP OK Jazz, bendi kubwa zaidi ya Kiafrika kuwahi kutokea.
Madilu aliyezaliwa mnamo Mei 28, 1952 jijini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jina lake halisi Jean De Dieu Makiesse alianza kazi yake ya muziki mnamo 1969 na bendi iliyoitwa Symba, wakati wa mwanzo wa kazi yake, alikuwa mwimbaji wa bendi kadhaa ikiwa ni pamoja na Bamboula iliyoongozwa na Papa Noel, Les Etoiles, Festival des Macquisards iliyoongozwa na Sam Mangwana na Michelino na Fiesta Populaire iliyoongozwa na Faugus Izeidi.