Mwalimu na Mlezi wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Antoni wa Padua – Ntungamo, Jimbo Katoliki la Bukoba, Padri Roland Kashaga (katikati kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa Komunio ya Kwanza baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya watoto 90 kupokea Ekaristi Takatifu, iliyofanyika Parokia ya Bikira Maria wa Mateso - Mbezi Msakuzi, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam. Kulia katikati ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Fregiel Massawe. (Picha na Yohana Kasosi)