Songwe
Na Mwandishi wetu
Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, mkoani Songwe imepatiwa magari matatu ya kubebea wagonjwa (Ambulances) ili kutoa huduma za dharura na kwa rufaa za matibabu kwa wananchi.
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu (pichani) alitoa taarifa hiyo wakati akizungumza na Madaktari, Wauguzi na timu ya usimamizi wa Afya ngazi ya Halmashauri katika ziara yake mkoani Songwe.