Mbinga
Na Mwandishi wetu
Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma imefanikisha mpango wa kumtua ndoo kichwani mama baada ya kuanzisha huduma ya maji.
Hatua hiyo imetokana na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani Mbinga kukamilisha ujenzi wa mradi mkubwa wa maji utakaohudumia zaidi ya wakazi 3,600 wa kijiji hicho, na kijiji cha Mangwangala.