LILONGWE, Malawi
Chansela wa Chuo Kikuu cha Katoliki cha Malawi, Askofu Martin Anwel Mtumbuka, ametoa mwito wa kuanzishwa kwa wahitimu, wanaozingatia uadilifu na maadili thabiti, pamoja na ubora wa kitaaluma.
Akizungumza wakati wa Mkutano wa 25 wa Chuo Kikuu, kwa ajili ya utoaji wa Astashahada, Stashahada na Shahada, uliofanyika Ijumaa iliyopita, Askofu Mtumbuka alieleza wasiwasi wake, kuhusu idadi inayoongezeka ya watu walioelimika, ambao hawana uadilifu katika majukumu yao ya kitaaluma na utumishi wa umma.
“Tayari tuna watu wa kutosha walioelimika, lakini kwa kusikitisha, tuna watu wengi sana waliopotoka. Tunachohitaji sasa ni wanaume na wanawake walioelimika, ambao watahudumu kwa uaminifu, uadilifu na huruma,” alisema Askofu Mtumbuka.
Msemaji wa kuanza kwa Sherehe hiyo, Mheshimiwa Jaji Annabel Mtalimanja, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Malawi (MEC), pia aliwasihi wanafunzi waliohitimu hivi karibuni, kukataa ufisadi na rushwa, akielezea kuwa ni vikwazo vikubwa kwa maendeleo ya taifa.