DAR ES SALAAM
Na Joseph Mihangwa
Ghafla, Afrika imenyamaza kupiga kelele juu ya paa kutangaza sera zake za maendeleo zenye sura ya ubinadamu; sera zilizojaa kurasa za Vyombo vya Habari enzi za uhuru na zama za mageuzi ya uchumi kufuatia uhuru, kwa maandishi makubwa makubwa na kwa wino wa kuangaza:
“Ujamaa” kwa Tanzania; “Zambian Humanism” kwa Zambia; The Common Man’s Charter” – Uganda na “The Guinean Revolution” kwa Guinea ya Rais Ahmed Sekou Toure.