Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Waaswa kuitegemeza Tumaini Media

DAR ES SALAAM

Na Deus Kamanga

Waamini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Kanisa katika kufanikisha maendeleo kwa vyombo vya Habari vya Kanisa ili viweze kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa watu wote Ulimwenguni, kwani kwa kufanya hivyo watajipatia neema na baraka kwa Mungu.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Padri Vitalis Kassembo, Mkurugenzi wa Walei Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakati akitoa homilia katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Shukrani ya Umoja wa Marafiki wa Tumaini Media (UMTUME), kuadhimisha Siku ya Mawasiliano Duniani iliyofanyika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Fatima – Msimbazi, jijini Dar es Salaam.
Padri Kassembo ambaye pia ni Paroko wa Parokia ya Familia Takatifu - Mburahati, jimboni humo, alisema kuwa Kituo cha Tumaini Media jimboni Dar es Salaam, ni miongoni mwa vyombo vya Habari ndani ya Kanisa kinachofikisha ujumbe wa Mungu kwa watu, kikielimisha na kuhabarisha masuala mbalimbali ya kijamii yanayostawisha maelewano mazuri yenye kuleta mshikamano unaompendeza Mungu.
Padri Kassembo alisema kuwa jitihada zinazofanywa na Utume kwa ajili ya maendeleo ya Tumaini Media ni mfano dhahiri kwa waamini na watu wenye mapenzi mema na Kituo hicho cha Kanisa, hivyo akawataka waamini na watu wengine kuiga mfano huo kwa kuendelea kumshukuru Mungu, sanjari na kukichangia ili kisonge mbele.
Aliongeza pia kuwa ni jambo la msingi kwa kila mbatizwa kushirikiana na Kanisa na Taasisi zingine zenye nia njema ya kuviwezesha vyombo hivyo, wakiwemo UMTUME, kwa hali na mali kwa kuwa kufanya hivyo ni kujiwekea hazina mbinguni.
Awali Mkufunzi wa semina ya Umtume, Maalim Jeran Mushi aliwaasa Wanaumtume kudumisha upendo na umoja katika kutekeleza utume wao, kwa kutawaliwa na upole, unyenyekevu, hekima na amani.
Maalim Mushi alibainisha kuwa Wanaumtume wanapaswa kuwafikia watu wote katika hali ya unyenyekevu kwa kuwashirikisha lengo la kuisadia Tumaini Media kiuchumi, na kuacha tabia ya kukata tamaa kwa sababu Mungu Mwenyezi anaziona nia zao, na hawezi kuwaacha katika magumu yoyote.
Alifafanua kuwa kiasi hicho cha fedha kitaelekezwa kufanyia maboresho eneo la mapokezi katika ofisi za Tumaini Media, na wataendelea na maboresho kulingana na uhitaji wa maeneo mengine.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.