Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Dekano wa Dekania ya Mtakatifu Petro, Padri Elidius Kibangura (wa pili kushoto) akiwa na viongozi mbalimbali na Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Karoli Lwanga Tandale baada ya kuwapatia Sakramenti Takatifu ya Kipaimara waimarishwa 17.

Na Pd. Richard Mjigwa, C.PP.S

Jalai 12, kila mwaka, Mama Kanisa huadhimisha Dominika ya Utume wa Bahari, ikiwa ni Siku ya kumwomba, kumtukuza, kumsifu na kumshukuru Mungu kwa huduma yao.
Hakika ni mchango mkubwa, unaotolewa na mabaharia hao, pamoja na wavuvi, kwa ajili ya ustawi, maendeleo na mafao ya wengi.
Kwa kawaida, hiyo ni siku maalumu ya kutambua mchango na sadaka ya watu hao, ambao wakati mwingine, utu na heshima yao vinahatarishwa kutokana na changamoto mbalimbali, wanazokumbana nazo kila siku.
Utume wa Bahari, “Opus Apostolatus Maris”, unaojulikana na wengi kama “Stella Maris”, ulianzishwa tarehe 4 Oktoba 1920, na Waamini Walei wanaoshiriki: Ukuhani, Unabii na Ufalme wa Kristo Yesu, unaopata chimbuko lake kutoka katika Sakramenti ya Ubatizo.
Ni jukumu na wito wa Waamini Walei, kuutafuta Ufalme wa Mungu, unaosimikwa katika kweli na uzima; ni ufalme wa utakatifu na neema; ni ufalme wa haki, mapendo na amani; huku wakiyashughulikia mambo ya dunia, na kuyaelekeza kadiri ya mpango wa Mungu. 
Waamini Walei wanaitwa kuyatimiza majukumu yao wenyewe, wakiongozwa na roho ya Kiinjili, ili kumtangaza na kumshuhudia Kristo Yesu kwa imani, matumaini na mapendo thabiti! 
Ili kuonesha na kushuhudia ukaribu wa Kanisa kwa mabaharia, wavuvi pamoja na familia zao, Papa Pio XI, tarehe 17 Aprili 1922, aliridhia kuanzishwa kwa Utume wa Bahari “Opus Apostolatus Maris.” Leo hii kuna jeshi kubwa la watu, wanaojisadaka zaidi kuwadumia mabaharia na wavuvi, katika bandari 300 kwa kutembelea meli zisizopungua 70,000 kwa mwaka. 
Mama Kanisa anawashukuru kwa dhati Mitume hawa, wanaoendelea kujisadaka bila ya kujibakiza, kwa ajili ya huduma makini kwa mabaharia, wavuvi pamoja na familia zao. 
Wadau wa Utume wa Bahari, wamekuwa ni mashuhuda na vyombo vya uinjilishaji wa kina, kwa kuwafunulia watu wa Mungu, ile sura pendelevu ya Mama Kanisa, kwa kuonesha ukaribu wake kwa watu watakatifu wa Mungu, na hivyo kuwahamasisha kujisikia kuwa, ni sehemu hai ya Fumbo la Mwili wa Kristo yaani Kanisa. 
Takribani miaka 100 iliyopita, Dominika ya Utume wa Bahari, imekuwa ni kipindi muafaka cha ujenzi wa misingi ya majadiliano ya kidini, kiekumene na kitamaduni, kutokana na mwingiliano wa watu kutoka katika dini, tamaduni na Mataifa mbalimbali duniani.
Papa Pio XI alitamani sana kuona kwamba, Utume wa Bahari unaendelezwa kwenye Bahari na fukwe mbalimbali za dunia. Roho Mtakatifu, kwa maombezi ya Bikira Maria, aendelee kupyaisha utume na huduma hii, mintarafu mahitaji ya ulimwengu mamboleo! 
Kuna mabaharia ambao dhamiri zao zinahangaika sana, na mara nyingi Mapadri wa maisha ya kiroho, kwa mabaharia na wavuvi, wamekuwa ni msaada mkubwa. 
Mabaharia ni watu wanaofanya kazi zao, katika mazingira magumu na hatarishi, mara nyingi nje ya nchi, makazi na familia zao! 
Mapadri washauri wa kiroho katika muktadha kama huu, wanakuwa ni mashuhuda na vyombo vya Injili ya matumaini, kwa mabaharia na wavuvi waliopondeka na kuvunjika moyo! Mapadri wanapaswa kuwa ni watu wenye huruma, wapole na wanyenyekevu wanapowahudumia mabaharia, wavuvi pamoja na familia zao.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliwaletea historia ya kuibuka kwa Madhehebu mengine ya Kiprotestanti. Leo tunaendelea kuwaletea kuibuka kwa Madhehebu ya Kiprotestanti, hususani Uprotestanti chini ya John Calvin. Sasa endelea…

John Calvin 1509-1564:
Kati ya Waprotestanti waanzilishi, Calvin ndiye aliacha nyuma mafundisho ya msingi kwa Waprotestanti.  Calvin alizalilwa mwaka 1509 huko Ufaransa.  Alijifunza elimu dunia ya wakati huo (humanist), vilevile akajifunza Kilatini, Kiyunani na Sheria.  

Mwaka 1533, anasema aliongoka na kuitikia wito wa Mungu kuwa “Chombo cha kutangaza ukweli”. Alipokea wito huo kwa moyo wake wote na kuanza kuhubiri.  

Mwaka 1535, ilimbidi akimbie kutoka Ufaransa na kwenda Basle-Uswizi, kwa sababu ya upinzani dhidi ya mafundisho yake.  

Akiwa Basle, Uswizi, aliandika mafundisho yake ya dini, Teologia, ambayo baadaye aliyaboresha.  Ni muhimu kujua mafundisho haya ya Calvin, kwa sababu madhehebu mengi ya Kiprotestanti hata yale ambayo hayamkubali kama mwanzilishi wake, mafundisho yao yameingiliwa na teolojia yake. 

Calvin kimsingi alifundisha yafuatayo:
1.    Kwanza ya yote, Mungu ni mwenye mamlaka yote.  Yeye ni Muumbaji, Mtegemezaji  na Mtawala.  Yeye yuko juu sana na mwenye uamuzi wote. 

    Yeye huamua anavyotaka, hana sheria inayombana. Hivyo, binadamu hawezi kuungana naye kama walivyofundisha watakatifu, bali la kufanya ni kujiweka chini ya utashi wake na maagizo yake.  Kwa hilo alikuwa karibu na mafundisho ya Waislamu.

2.    Alifundisha kwamba, tangu milele, watu wengine walipangiwa tayari kwenda mbinguni na wengine kwenda motoni (predestination).  Mtu hawezi kufanya lolote kugeuza hilo.  

    Kwa wale waliopangiwa kwenda mbinguni, kuna ishara tatu za kuwatambua.  (a) Kushika imani  ya kweli (b) Maisha ya uadilifu (c) na kushiriki chakula cha Bwana.  

    Yeye na wafuasi wake,  kwa sababu walikuwa na ishara hizo, ilikuwa ni wazi kwamba wamepangiwa mbinguni. Hapo mtu anaweza kusema “Nimeokoka” kwa sababu kama mtu amepangiwa kwenda mbinguni haiwezi kugeuka. 

    Mtu hana uhuru wa kutenda mabaya au mema, kwa sababu yeye ni mwovu, bali Kristo  anamhesabia wokovu.  Hata hivyo yule anayekosa lazima aadhibiwe kwa sababu hakulazimishwa na mtu kutenda mabaya.

3.    Biblia ndio chanzo pekee cha ufunuo, na ishikwe na kufuatwa neno kwa neno kama ilivyoandikwa. 

4.    Kuna Kanisa lisiloonekana na Kanisa linaloonekana. Kanisa lisiloonekana, ni la wale wote waliopangiwa kwenda mbinguni, tangu mwanzo wa nyakati hadi mkamilisho wake.  Kanisa linaloonekana ni la watu wale wanaotimiza masharti  anayoyafundisha.

5.  Anazitambua Sakramenti mbili tu Ubatizo na Ekaristi; lakini sakramenti hizo siyo za lazima kwa wokovu. Katika ibada mbalimbali, anakataza nyimbo, pawepo zaburi tu, vilevile anakataza ibada nzuri, hija, maandamano, sanamu nk. 

6. Katika mafundisho yake alisisitiza sana juu ya umisionari. Alitayarisha watu ambao walikuwa tayari, bila kujali shida kwenda kuhubiri na kuwaongoa watu, kwa mafundisho yake. 
    Walifundisha vikundi na watu binafsi nyumba hadi nyumba. 

7. Hawakumtambua Papa, Maaskofu au Mapadri.  Kwao, kila mmoja aliyebatizwa ni Padri. Hivyo, kiongozi wa ibada huchaguliwa na watu, au huteuliwa na yeye na anaweza kumfukuza wakati wowote.

8.    Kwake mwisho wa dunia, uko mbali, hivyo lazima binadamu afanye kazi sana na kuendeleza ulimwengu.  Faida inayopatikana katika kazi hiyo, isitumike kwa anasa na starehe, bali iwekezwe au kusaidia maskini. 

Hii iliwapa Waprotestanti, nguvu za kipesa na kuhamasisha ubepari.  Hadi leo Waprotestanti wanajua biashara, kuwekeza na kuzalisha kuliko Wakatoliki. 

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi (nyuma), Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu (nyuma), wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Bodi ya Hospitali ya Kardinali Rugambwa, iliyopo Ukonga, jimboni humo, baada ya Maadhimisho ya Miaka 40 ya Hospitali hiyo. Wa tatu kushoto mbele ni Askofu Msaidizi Mteule wa Jimbo hilo, Vincent Mpwaji.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Walei, Parokia ya Mtakatifu Thoma wa Akwino – Kipunguni, jimboni humo, baada ya adhimisho la Misa Takatifu ya Kutabaruku Kanisa na Altare parokiani hapo.

Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama, Mhashamu Christopher Ndizeye (katikati) akiwa katika adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 25 ya Upadri iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa Kuu la Mt. Karoli Lwanga, jimboni humo. Kushoto ni Mwadhama Protase Kardinali Rugambwa na kulia ni Askofu Joseph Mlola wa Jimbo la Kigoma.

Mwenyekiti wa Shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Adolf Mrema (kulia), akimsikiliza Mwenyekiti Mstaafu wa Shirika hilo, Gordon Rwenyagira (kushoto), baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kuhitimisha Kampeni ya Tegemeza Tumaini Media ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Bonaventura – Kinyerezi, Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Paroko wa Parokia ya Kirua_Iwa, Jimbo Katoliki la Moshi, Padri Calistus Shayo, akiwa katika picha ya pamoja na Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) wa Parokia ya Mtakatifu Kizito – Kilongawima, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya WAWATA (WAWATA Day) iliyofanyika parokiani hapo.

Dar es Salaam

Na Arone Mpanduka

Hivi karibuni Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kupitia kwa Rais wake Wallace Karia, lilitangaza rasmi kuwa kuanzia msimu ujao wa 2026/2027, Ligi Kuu Tanzania Bara itaanza kutumia teknolojia mpya ya VS, ambayo itasaidia kutoa suluhisho la baadhi ya matukio tata ya uwanjani.
Uamuzi huo umekuja baada ya kushindikana kwa teknolojia ya VAR, ambayo ina gharama kubwa za uendeshaji.
VS NI NINI?
Kwa mujibu wa maana ya kawaida katika michezo, VS (Video Support) ni mfumo wa usaidizi wa video, unaotumika kwenye michezo kama vile mpira wa miguu, wavu au tenisi, ambao ni tofauti kidogo na VAR (Video Assistant Referee).
VS (Video Support) ni mfumo wa kidijitali unaoruhusu timu au wachezaji, kuomba marudio ya video kwa maamuzi muhimu ya uwanjani, kama vile goli, adhabu au makosa, sawa na jinsi wanavyofanya katika tenisi (Hawkeye), au mpira wa wavu (Challenge System). 
Tofauti na VAR, ambapo waamuzi wanaweza kuamua kutumia au la, lakini timu zinakuwa na idadi maalumu ya changamoto za kuomba.
INAFANYAJE KAZI UWANJANI?
Wakati mchezo unaendelea, wachezaji au nahodha anaweza kuomba marudio ya tukio tata, na kisha mwamuzi hulazimika kurudia na kufanya maamuzi.

LONDON, Uingereza
Meneja mpya wa klabu ya soka ya Chelsea, Xabi Alonso, aliyeanza kazi yake Stamford Bridge, ameweka ngumu na kutaka kumbakisha kiungo mshambuliaji, Enzo Fernandez, klabuni hapo.
Kiungo huyo wa kati wa Argentina, mwenye umri wa miaka 25, alikuwa anatakiwa na klabu ya soka ya Real Madrid ya Hispania, kwa bei kubwa ya Pauni milioni 120, lakini Alonso bado ameonesha nia ya kumuhitaji zaidi.
Alonso alikiri wazi kumuhitaji nyota huyo, wakati wa mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari, tangu achukue jukumu la kuiongoza Chelsea, kufuatia kuondoka kwake Real Madrid mnamo Januari.
“Ndio tumezungumza, lakini kama unavyoelewa, tulichosema kitabaki kuwa cha faragha,” alisema Alonso.
Aliongeza kuwa mshambuliaji Nicolas Jackson, atarudi kwenye kikosi wakati wa maandalizi ya klabu ya msimu nchini Australia na Asia, baada ya Bayern Munich, kuamua kutofanya uhamisho wake wa mkopo kuwa wa kudumu.

Page 1 of 66