Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Wanandoa wametakiwa kupendana na kuvumiliana katika shida na raha siku zote za maisha yao, kwani katika maisha ya ndoa kuna mengi yanayotokea, hivyo bila kuvumiliana, ndoa hizo haziwezi kudumu.
Wito huo ulitolewa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Shukurani kwa Mungu kwa Jubilei ya Miaka 25 kwa Wanandoa jozi tatu ambao ni Thomas Uiso na Misuka Makani, Damas Mugashe na Rose Emanuel, Deusdedit Rutazaa na Jaove Ijumba, ilifanyika katika Parokia ya Mtakatifu Kizito – Kilongawima, jimboni humo.
“Ndoa ni uvumilivu, siyo mwezako akikukosea kidogo tu, wewe unakuwa na hasira muda huo huo, sio vizuri, lazima muwe watu wa kusameheana, kwa sababu ninyi mmekuwa mwili mmoja, lazima muwe watu wakulindana kwa makosa mnayokwazana,” alisema Askofu Musomba, na kuongeza;

Dodoma

Na Mwandishi wetu

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeshauri Serikali kusimamia vyema Mkandarasi anayejenga uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma ili akamilishe ujenzi huo kwa wakati.
Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso alisema kuwa ni vema mkandarasi akaharakisha ujenzi wa uwanja huo, ili kwenda na mkataba wa ujenzi.
Alifafanua kwamba kumekuwa na tabia kwa baadhi ya Wakandarasi kuomba kuongezewa muda wa ziada wanapopewa kazi, bila kujua muda utakapoongezwa na gharama nazo zinaongezeka.
Hivyo wao kama Kamati, wanashauri Serikali kwanza ni kumsimamia mkandarasi akamilishe ujenzi kwa wakati.
“Kumekuwa na tabia ya Wakandarasi wetu wanapopewa kazi wanaongeza muda wa ziada ambao hautakiwi uingezwa mara kwa mara, Hivyo tunaomba eneo hili Serikali isimamie, kwani anapoongezewa muda, na gharama zinazidi zaidi za ule mkataba uliokuwa umesainiwa,”alisema kiongozi.

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Imeelezwa kwamba endapo ikatokea Askari ama Mwanajeshi  akafanya mauaji ya mtu ama watu katika vita vya haki, siyo dhambi.
Aidha, mauaji hayo yanapaswa kuwa katika zile jitihada zilizotumika kusuluhisha, lakini imeshindikana, kwani lengo la kufanya hivyo, ni kuimarisha amani katika maisha ya wanadamu.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Padri Paul Sabuni, Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Ambrose – IPTL, Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakati akitoa ufafanuzi wa swali alilodai kuulizwa na baadhi ya Waamini wanaofanya kazi ya Uaskari, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 2025 ya Ukristo kwa Wafanyakazi wa Sekta ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama, iliyoadhimishwa katika Parokia ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu – Makongo Juu, jijini Dar es Salaam.

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Waamini wamekumbushwa kuwalinda, kuwatunza, na kuwapenda Mapadri wao, na kamwe wasikubali Mapadri wao wachafuliwe na mtu mmoja au kikundi cha watu.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba alitoa wito huo hivi karibuni wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, alipofanya ziara yake ya kichungaji katika Parokia ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu – Buza, jijini Dar es Salaam.
“Sasa niwaombe kitu kimoja, endeleeni na ukarimu huo. Wapendeni Mapadri wenu, nafahamu kwamba mna Mapadri wawili hapa, jitahidini kuwapenda na kuwalinda, wetendeeni mema Mapadri wenu, msikubali Mapadri wenu wapate changamoto, msikubali Mapadri wenu wachafuliwe na mtu mmoja au kikundi cha watu, hakikisheni mnaendeleza ushirikiano kati yenu na Mapadri wenu katika Parokia hii ya Buza,” alisema Askofu Musomba.

Dar es Salaam

Na Laura Chrispin

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi amewasihi Waamini kutambua kwamba Bwana Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu aliyekubali kujinyenyekeza na kutoa mwili wake usulubiwe kwa ajili ya ukombozsi wa Wanadamu.
Askofu Ruwa’ichi alitoa wito huo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya Uwaka iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Clara-Mongo la Ndege Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.
“Imetimia siku 40 tangu kuzaliwa Yesu ambaye alijitoa sadaka kwa watu wake kwa sababu ya upendo aliokuwa nao kwa kuutoa mwili wake na kukaa kwetu, ikiwa ni hali ya unyenyekevu wa Kimungu, kwani mara zote ni mkamilifu kwa watu wake,”alisema Askofu Ruwa’ichi.

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Austin Makwaia Makani Investment (AMMI), Austin Makani amewashauri Wafanyakazi wa Tumaini Media kuhakikisha wanawafahamu vyema wateja wao, kwani hiyo itawasaidia kufahamu bidhaa gani wateja wao wanazitaka.
Makani ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tumaini Media, aliyasema hayo alipokuwa akitoa mada katika Semina Elekezi kwa Wafanyakazi wa Tumaini Media kuhusu mambo ya Masoko ilioyofanyika hivi karibuni ofisini kwake Posta, jijini Dar es Salaam.
‘Kwanza kabisa ukimfahamu vyema mteja wako, basi utauza bidhaa yako. Ni lazima pia ujue kwamba mteja anahitaji bidhaa gani, na kwa wakati gani. Muuzie mteja bidhaa ambayo anaitaka, siyo bidhaa unayotaka wewe…
“Tuchukulie mfano kwa watu ambao pengine wanapenda sana kula ‘chips’, je, ukienda kuvua samaki baharini, kwenye ile ndoano yako unayotumia kuvulia, utaweka kipande cha ‘chips?’ hapana, lazima uweke kitu ambacho samaki anakipenda, siyo kitu ambacho unapenda wewe.
Kwa hiyo, hata kwenye biashara, uza kile mteja anachotaka, siyo unachotaka wewe, kwa sababu inawezekana unachotaka wewe, mteja hakitaki,” alisema Makani.

Mansa, Zambia
Parokia ya Mtakatifu Michael – Namwandwe, na Kanisa Kuu la Kupalizwa kwa Maria, Jimbo Katoliki la Mansa, imezindua rasmi Wiki ya Wagonjwa, mpango unaozingatia afya unaolenga kuhamasisha huduma za kinga na ustawi miongoni mwa Waamini.
Mpango huo uliongozwa na Padri Rodgers Chanda, Mkurugenzi wa Kichungaji, pamoja na Padri Christopher Kanja kutoka Kanisa Kuu la Kupalizwa kwa Maria, katika onyesho la uongozi kwa kielelezo, huku Mapadre wote wawili wakishiriki kikamilifu katika kupima shinikizo la damu (B.P.) na kupima malaria, wakiwatia moyo Waamini kutanguliza afya zao.

LUSAKA, Zambia

Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Zambia (Zambia Conference of Catholic Bishops: ZCCB) limezindua Kampeni ya kufuta madeni ya Mwaka wa Jubilei 2025, ikitoa wito wa msamaha wa haraka wa deni, haki ya kiuchumi, na uwazi katika usimamizi wa madeni ya Zambia.
Uzinduzi huo ulifanyika katika Kapingila House mjini Lusaka nchini humo mwishoni mwa Mkutano wa Kwanza wa Baraza Kuu wa ZCCB kwa 2025, iliyokwenda na wito wa Baba Mtakatifu Fransisko wa haki ya kiuchumi na msamaha wa madeni duniani kote kama sehemu ya Mwaka wa Jubilei 2025.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Rais wa ZCCB, Askofu Mkuu Ignatius Chama wa Jimbo Kuu Katoliki la Kasama, alisisitiza tena msingi wa Kibiblia wa mapokeo ya Jubilei, akinukuu kitabu cha Mambo ya Walawi, 25:1-8 kinachosisitiza huruma, haki na ufufuaji wa jamii zilizoelemewa na madeni yasiyo ya haki.

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Fransisko amesema kuwa mateso na mahangaiko ya mwanadamu, ni zawadi ya matumaini na uaminifu wa Mungu katika Fumbo la Pasaka, na kwamba upendo wa Mungu daima utawaandama waja wake hata wakati wa majaribu na vikwazo katika maisha yao.
Papa alitoa ujumbe huo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya 33 ya Wagonjwa Duniani mwaka 2025, iliyoadhimishwa mjini Vatican, siku ambayo ilianzishwa Mei 13 mwaka 1992, na kuadhimishwa kwa mara ya kwanza kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa Lourdes nchini Ufaransa, mnamo Februari 11 mwaka 1993.
Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa kwa ngazi ya kijimbo yaliyoadhimishwa mwaka huu wa 2025, yananogeshwa na kauli mbiu isemayo, “Na tumaini halitahayarishi, lakini hutuimarisha wakati wa majaribu,” huku Baba Mtakatifu akiwaalika watu wote wa Mungu kuwa Mahujaji wa Matumaini.

VATICAN CITY, Vatican

Wanajeshi na Polisi wametakiwa kutambua kwamba wameitwa na Mungu ili kutetea wanyonge, kulinda waamini, kuhamasisha watu kuishi kwa amani, pamoja na kuendeleza haki na amani kila mahali.
Hayo yalisemwa na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Fransisko katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Vikosi vya Wanajeshi, Polisi na Usalama, aliyoiadhimisha mjini Roma hivi karibuni.
“Ni nani bora kuliko ninyi, wanajeshi na polisi wapendwa, wavulana na wasichana, wanaweza kushuhudia vurugu na kusambaratika kwa nguvu za uovu zilizopo ulimwenguni? Mnapigana nao kila siku. Kiukweli mmeitwa kutetea wanyonge, kulinda Waamini, kuhamasisha kuishi kwa amani kwa watu…
“Kila mmoja wenu anafaa kwa nafasi ya ulinzi, ambaye anatazama mbele sana, ili kuepusha hatari na kuendeleza haki na amani kila mahali. Ninawasalimu ninyi nyote kwa upendo mkuu, Ndugu wapendwa, ambao mmefika Roma kutoka sehemu nyingi za dunia kusherehekea Jubilei yenu maalum…..

Page 1 of 47