Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

BAGAMOYO

Na Mathayo Kijazi

Baada ya mchakato wa muda mrefu hatimaye Bagamoyo Lango la Ukristo Tanzania sasa historia yake imekamilika, kutokana na kuundwa kuwa Jimbo jipya Katoliki, huku Baba Mtakatifu Fransisko akimteua Mhashamu Askofu Mteule Stephano Musomba, kuwa Askofu wa kwanza wa jimbo hilo.
Kabla ya uteuzi huo Mhashamu Musomba alikuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, aliyekuwa akisimamia Mawasiliano jimboni humo.

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Waamini wameonywa kuepuka kukata tamaa kutokana na majaribu wanayokutana nayo, kwani hayo ni sehemu ya maisha yao.
Kauli hiyo ilitolewa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia – Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Musa Kihoo wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima iliyofanyika parokiani hapo.

MBEYA

Na Angela Kibwana

Mhashamu Godfrey Jackson Mwasekaga, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Mbeya, amesema malengo ya Kwaresima ni kufanya toba, wongofu wa ndani na uaminifu kwa neno la Mungu.
Aidha, amesema kuwa Neno la Mungu ni chakula cha kiroho, na ni taa ya kuwaongoza waamini kwenye njia ya Ukristo wao.
Askofu Mwasekaga alisema hayo wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu, aliyoadhimisha katika Parokia ya Mtakatifu Clara wa Asizi- Shewa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya.

Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Yakobo Mkuu Mtume – Kijitonyama, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika iliyoadhimishwa parokiani hapo hivi karibuni.

Mapadri na Viongozi wa Halmashauri ya Walei kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakifurahia jambo wakati wa mkutano wao, uliofanyika katika viwanja vya Kituo cha Msimbazi, jimboni humo hivi karibuni.

Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mlima wa Karmeli – Bunju, Jimbo Katoliki Teule la Bagamoyo, Padri Dominic akiwaombea Wakatekumeni wapya wanaojiandaa kubatizwa katika Mkesha wa Pasaka wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima iliyoadhimishwa parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi)

DAR ES SALAAM

Na Joseph Mihangwa

Ghafla, Afrika imenyamaza kupiga kelele juu ya paa kutangaza sera zake za maendeleo zenye sura ya ubinadamu; sera zilizojaa kurasa za Vyombo vya Habari enzi za uhuru na zama za mageuzi ya uchumi kufuatia uhuru, kwa maandishi makubwa makubwa na kwa wino wa kuangaza:
“Ujamaa” kwa Tanzania; “Zambian Humanism” kwa Zambia; The Common Man’s Charter” – Uganda na “The Guinean Revolution” kwa Guinea ya Rais Ahmed Sekou Toure.

Ujenzi wa Miundo mbinu:
Mwishoni mwa mkutano waliunda Shirika lililoitwa: ‘Inter-Regional Episcopal Board of Eastern Africa (ITEBEA)’. Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Zambia, Fr. Killian Flynn, OFM Cap alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wake wa kwanza na kuanzia mwaka 1964 akawa na ofisi ya kudumu Nairobi, Kenya.
Fr. Killian Flynn ndiye Baba wa Amecea aliyehudumu hadi mwaka 1972. Askofu Mkuu Adam Kozlowiecki, (Baadaye Kadinali) wa Lusaka, Zambia alikuwa Mwenyekiti wake wa kwanza.
Mkutano wa Pili ulikuwa huko Roma: Wakati wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikani (1962 -65) Maaskofu walipata muda wa kufahamiana zaidi na mnamo Novemba 1964 Maaskofu walikutana Roma katika Chuo cha Mt.  Anselmo.

SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY

DAR ES SALAAM

Na Paul Mabuga

Hivi karibuni kumekuwa na mjadala kuhusu muziki wa Singeli unaotutambulisha kama Watanzania.
Wapo ambao hawakubaliani na hilo na wengine wanaunga mkono hoja ya utambulisho huu kama ilivyotolewa mara kadhaa na mwanafunzi wa zamani wa Mzumbe Sekondari na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi.

SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Kiongozi wa zamani wa kikundi cha ushangiliaji cha Timu ya Simba kijulikanacho kama ‘Kidedea’, Said Muchacho amesema kuwa mechi za Simba na Yanga za miaka ya sasa zimepooza, ikilinganishwa na miaka ya zamani.
Akizungumza na Tumaini Letu katika mahojiano maalum, Muchacho alisema kwamba kuanzia kipindi cha miaka ya 2000 kurudi nyuma, hekaheka zilikuwa kubwa sana kuelekea mechi za Simba na Yanga lakini kwa sasa haoni shamrashamra hizo.

SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY

Page 1 of 48