Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Orodha ya Wasanii Matajiri Tanzania 2024

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Mwaka 2024 unaendelea kushuhudia tasnia ya muziki nchini Tanzania ikiendelea kushamiri, huku wasanii wakizidi kujipatia umaarufu na utajiri mkubwa.
Muziki wa Bongo Flava umevuka mipaka ya Afrika Mashariki, ukiwavutia mashabiki lukuki duniani kote.
Kupitia vipaji vyao vya kipekee na bidii katika kazi zao, baadhi ya wanamuziki wamefanikiwa kujikusanyia utajiri mkubwa wa kutikisa.
Taarifa zinadai kuwa orodha hii ya wasanii matajiri zaidi Tanzania mwaka 2024, na kuufanya muziki wa Tanzania kupata thamani sokoni, na hivyo kuzibwaga nchi nyingi za jirani kutopata mpenyo.
Diamond Platinumz,
Nasibu Abdul Juma almaharufu kama Diamond Platnumz au Simba wa WCB anaendelea kutamba kileleni mwa orodha ya wasanii matajiri zaidi Tanzania.
Utajiri wake unatokana na muziki wake unaoendelea kutikisa pande mbalimbali za Afrika na Dunia kiujumla mathalan katika biashara mbalimbali, ikiwemo lebo yake ya WCB, uwekezaji katika mali isiyohamishika, na mikataba kibao ya matangazo.
Maisha yake ya kifahari yamekuwa yakionekana kupitia magari yake ya kifahari, nyumba za kifalme, na safari kwenda nchi za kigeni.
Juma Jux
Juma Mussa Mkambala almaharufu kwa jina la kisanii kama Juma Jux amejizolea utajiri mkubwa kupitia muziki wake unaovuma, hasa nyimbo zake za mapenzi zinazogusa hisia za wengi.
Uwezo wake wa kuandika nyimbo zenye mashairi ya kuvutia na sauti yake tamu vimemfanya kuwa mmoja wa wasanii wanaotafutwa sana Tanzania.
Jux amekuwa miongoni mwa wasanii wanaoishi maisha ya kifahari nchini Tanzania, uku akishuhudiwa kumiliki imagari ya kifahari mbalimbali, ikiwemo Mercedes Benz E-Class ya mwaka 2021, ambayo gharama yake ni zaidi ya dola elfu 53 bila ya kodi ambazo ni karibia shilingi milioni 160 za Kitanzania.
Harmonize
Konde Boy, Harmonize, amejipatia nafasi ya tatu katika orodha hii kutokana na muziki wake unaopendwa na mamilioni, lebo yake ya Konde Music Worldwide, na biashara zake nyingine, ikiwemo ya Redio.
Ubunifu wake katika muziki na mtindo wake wa kipekee, umemfanya kuwa miongoni mwa wasanii wanaolipwa pesa nyingi zaidi kwa show nchini.
Nafasi ya tatu ikifuatiwa na msanii Zuchu, Marioo, Nandi, Ommy Dimpoz, Rayvanny, Ali Kiba na Niki wa pili akimalizia nafasi ya kumi.
Muziki unalipa ukiiufanya kwa bidii na kwa ubunifu zaidi, kwani ni sehemu ya ajira ya vijana wengi kwa sasa nchini.

Rate this item
(3 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.