Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Kocha Man United afichua harakati zilizombakisha

MANCHESTER, Uingereza
Meneja wa Manchester United Erik ten Hag ameweka wazi kuwa  likizo yake ya majira ya kiangazi iliingiliwa na klabu hiyo mara baada ya kumfuata kwake na kumwomba aendelee kubaki ndani ya klabu yao.
Mustakabali wa Ten Hag ulikuwa mashakani kabla ya kuiongoza United kupata ushindi katika fainali ya Kombe la FA, lakini klabu hiyo imeamua kumweka Mholanzi huyo mahali pazuri.
United walimaliza katika nafasi ya nane msimu uliopita - nafasi yao ya chini kabisa katika enzi ya Premier League.
Mmiliki mwenza mpya wa United Sir Jim Ratcliffe inadhaniwa alizungumza na kocha wa zamani wa Bayern Munich Thomas Tuchel lakini Mashetani Wekundu hatimaye wakaamua kumbakisha Ten Hag.
“Wasimamizi wa klabu walikuja kwangu nikiwa likizoni, ghafla walijitokeza kwenye mlango wangu na kuniambia wanataka kuendelea nami.”
“Manchester United wameniambia kwamba walizungumza na Tuchel, lakini hatimaye walifikia hitimisho kwamba tayari wana meneja bora,” aliongeza.
Katika msimu wake wa kwanza, Mholanzi huyo aliiongoza klabu hiyo hadi nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu, pamoja na fainali za Kombe la Carabao na Kombe la FA na Kisha akawaongoza kwa ushindi wa Kombe la EFL mnamo 2023.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.