Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Klabu ya soka ya Simba imesema kuwa kinachoendelea hivi sasa katika sajili zao za wachezaji wa Kitanzania, ni sehemu ya hujuma za kuwachafua ili waonekane hawajui wanachokifanya.
Hivi karibuni Klabu za Coastal Union ya Tanga, Geita Gold ya Geita, na KMC ya Kinondoni, kwa nyakati tofauti zilikuja juu zikipinga sajili za wachezaji wake waliosajiliwa na wekundu hao kwamba hazikuwa halali kwa sababu wachezaji bado wana mikataba nao.
Simba ilimtangaza beki Lameck Lawi kutoka Coastal Union kwamba imemsajili, kisha Valentino Mashaka wa Geita Gold, pamoja na Awesu Awesu wa KMC, lakini hadi sasa imeonekana kukwama kwa Lawi, huku wengine ikiwanasa kwa tabu.
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa wekundu hao wa Msimbazi, Ahmed Ally alisema kuwa wanahisi kuna jambo linaendelea, kwa sababu haiwezekani usajili wa wachezaji wa ndani uonekane una makosa, halafu wa wachezaji wa nje uonekane hauna dosari.
“Simba hatujawahi kukosea katika eneo la usajili, na ndiyo maana hata siku moja huwezi kusikia mchezaji katupeleka FIFA kisa anatudai. Tunafanya mambo yetu kwa weledi mkubwa. Leo hii haiwezekani tusajili wachezaji kutoka nje ya Tanzania bila malalamiko halafu ikitokea tunasajili mchezaji kutoka Geita au Kinondoni tu hapo, ikaja kuonekana hatukufuata utaratibu. Hizi ni namna za kutuchafua,” alisema.
Alisema kuwa wamesajili wachezaji wapatao nane wa Kimataifa, lakini hakuna klabu yoyote kutoka nje iliyoibuka kuzungumzia makosa ya usajili kwa wachezaji hao.
Simba imefanya usajili wa wachezaji 13 hadi sasa, ambao ni Lameck Lawi kutoka Coastal Union, Joshua Mutale kutoka Power Dynamos, Steven Dese Mukwala kutoka Asante Kotoko, Jean Charles Ahoua kutoka Stella Club d’Adjamé na Abdulrazack Mohamed Hamza kutoka Super Sport United.
Wengine ni Valentino Mashaka kutoka Geita Gold FC, Augustine Okejepha Kutoka Rivers United, Debora Fernandes Mavambo Kutoka Mutondo Stars, Omary Omary Kutoka Mashujaa FC, Karaboue Chamou Kutoka Racing Club d’Abidjan, Valentin Nouma kutoka St. Eloi Lupopo, Yusuph Kagoma kutoka Singida Black Stars FC na Kelvin Kijili kutoka Singida Fountain Gate.
Dirisha la usajili kwa Ligi Kuu soka Tanzania Bara, Ligi ya Championship, First League na Ligi Kuu ya Wanawake msimu wa 2024/25 ambalo lilifunguliwa Juni 15, litafungwa Agosti 15 mwaka huu, ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.