Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Bajeti yawakuna wenye viwanda

Mkurugenzi wa Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI), Leodegar Tenga, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maoni ya wenye viwanda waliojadili bajeti hiyo. Mkurugenzi wa Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI), Leodegar Tenga, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maoni ya wenye viwanda waliojadili bajeti hiyo.

DODOMA

Na Mwandishi wetu

Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI), limesema kuanzishwa kwa ada ya kuendeleza viwanda kwa bidhaa zinazotoka nje kwenye Bajeti Kuu ya Serikali, kutasaidia kulinda viwanda vya ndani, kuchochea uwekezaji, na kuongeza mauzo ya nje.
Mkurugenzi wa Shirikisho hilo, Leodegar Tenga alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maoni ya wenye viwanda waliojadili bajeti hiyo.
Alisema kuwa hatua ya serikali kupunguza ada na tozo zinazotolewa na wakala wa udhibiti ili kupunguza gharama za uzalishaji, kupunguza ushuru wa forodha wa malighafi za viwandani na pembejeo za uzalishaji, kutaongeza ushindani wa viwanda vya ndani.
Tenga alisema kwamba kuondoa kodi ya ongezeko la thamani kwa bidhaa za nguo zinazotengenezwa kwa pamba inayolimwa nchini kutachochea uwekezaji katika tasnia ya nguo nchini.
“Hatua za kodi zilizopendekezwa hapo juu zinalenga kusaidia viwanda vya ndani katika kupunguza gharama za uzalishaji, kuhimiza matumizi ya nyenzo za ndani, kuongeza ushindani, na kukuza ukuaji wa uchumi,” alisema Tenga.
Tenga alipongeza bajeti kuu ya Serikali kwa kuweka mambo muhimu ambayo yatachochea ukuaji wa viwanda nchini.
Alibainisha kuwa Serikali imekuwa sikivu kwa wenye viwanda na kila wanapokuwa na jambo, wamekuwa wakifunguliwa milango ya majadiliano, na kwamba hakuna jambo la wenye viwanda ambalo linakwama.
Tenga aliendelea kusema wenye viwanda wamefurahia sana bajeti ya serikali kwa kuzingatia uendelezaji wa miradi ya kimkakati kama reli ya kisasa (Standard Gauge Railway: SGR) ambayo alisema itasiadia kwa kiwango kikubwa kukuza viwanda vya ndani katika kuzalisha kwa wingi bidhaa.
Azungumzia mradi SGR
Tenga alisema kwamba miradi kama SGR inasaidia kukuza uchumi, kwani viwanda vitazalisha kwa wingi na bidhaa kusafirishwa kwa urahisi kwa haraka tofauti na sasa ambapo usafirishaji umekuwa ukisababisha bei kupanda.
“Nchi ambayo iko makini, inaendeleza miradi mikubwa kama ya ujenzi wa reli, barabara, miradi ya maji kama kuendeleza miradi ya kimkakati ya barabara maji, bandari kwa sabbau huwezi kuendeleza viwanda kama huna umeme au una matatizo ya usafirishaji,” alisema Tenga.
Tenga alifahamisha kwamba bajeti ya mwaka huu inakusudia kuhamasisha mapato ya ndani zaidi ikilinganishwa na bajeti ya 2023/24.
Kwa mujibu wa Tenga, jambo muhimu katika bajeti ya mwaka huu ni Serikali kufanya mageuzi mbalimbali ya muundo wa kodi, ada, tozo na marekebisho ya sheria na kanuni ili kuboresha mazingira ya biashara.
Alisema pia kuwa marekebisho ambayo yamependekezwa kuhusiana na sekta ya viwanda ni katika ongezeko la thamani VAT, ushuru wa bidhaa, ada na tozo za wakala, pamoja na ushuru wa forodha.
Tenga amesema kuwa baadhi ya hatua chanya, ni pamoja na kuanzishwa kwa tozo ya maendeleo ya viwanda kwa bidhaa zinazotoka nje, yenye lengo la kulinda viwanda vya ndani, kuchochea uwekezaji na kuongeza mauzo ya nje; kupunguza ada na tozo zinazotolewa na vyombo vya udhibiti, ili kupunguza gharama za uzalishaji.
Amesema pia kuwa wamefurahishwa na kupunguzwa kwa ushuru wa forodha kwenye malighafi za viwandani na pembejeo za uzalishaji, ili kuongeza ushindani wa viwanda vya ndani na kutozwa ushuru wa VAT kwenye bidhaa za nguo zinazotengenezwa kwa pamba inayolimwa hapa nchini ili kuchochea uwekezaji katika viwanda vya nguo vya ndani.
Alisema hatua za kodi zilizopendekezwa hapo juu zinalenga kusaidia viwanda vya ndani katika kupunguza gharama za uzalishaji, kuhimiza matumizi ya vifaa vya ndani, kuongeza ushindani, na kukuza ukuaji wa uchumi.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.