Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

KMC yajiengua kunyatia Ubingwa Ligi Kuu

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Uongozi wa klabu ya soka ya KMC umejitoa katika mbio za ubingwa msimu huu kutokana na kutokuwa na misuli ya kutosha katika kushindana na vilabu vingine.
Mtendaji wa klabu hiyo Daniel Mwakasungura alisema kuwa bado wanaendelea kujitafuta, huku akiweka wazi kuwa bado hawapo katika ramani za waokupambana na wenye uwezo wa kifedha .
Mwakasungura alifunguka kuwa wameliona hilo kwa mwaka huu, na kuamua kuijenga timu yao ili ikishakuwa sawa, waanze kupambana kwa misimu mingine ya ligi huko baadaye lakini kwa sasa bado hawana wachezaji wenye uwezo wa kiushindani.
Alisema kuwa kwenye upande wa soko la usajili, wenzao wamewaacha mbali sana kuliko wao, kwani gharama ambazo wanatumia vilabu vingine katika kusajili wachezaji, ni kubwa kuliko za wao, na hivyo kusababisha hata kupokonywa wachezaji wengi wzuri.
“Unajua kwenye soko la ushindani unatakiwa ujitutumue kweli sasa sisi tunamuona mchezaji, na tunatamani kumsajili lakini unakuta fedha tunayotoa ni ndogo kuliko ambayo wenzetu wakiamua kuitoa kwa mchezaji huyo huyo”, alisema Mwakasungura.
Alisema pia kuwa kwa sasa wao wanajenga timu ili iwe tishio kwa miaka inayokuja, kwani tayari wameshaanza kujipata katika namna ya uchezaji, hivyo vimebaki vitu vichache ambavyo wao kwa kusaidiana na bechi la ufundi, wanavitengeneza.
KMC msimu uliopita ilibaki kidogo kushuka kwenda kucheza Ligi ya Championship, lakini walijipapatua na kuendelea kubaki katika Ligi Kuu. Kwa msimu, na sasa wanachokifanya ni kujihakikishia nafasi ya kutoshuka Daraja ili malengo yao ambayo waliyaweka, yaweze kutimia.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.