Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Simba yaanika kilichomng’oa Fredy

Fredy Michael Fredy Michael

DAR ES SALAAM

Na Deus Helandogo

Uongozi wa klabu ya soka ya Simba kupitia kwa Meneja wake Ahmed Ally, umefunguka sakata la kuachana ghafla na mshambuliaji wao Fredy Michael, ambaye amedumu ndani ya klabu hiyo kwa miezi michache tu.
Ahmed Ally aliweka wazi kwamba sababu za kuachana na nyota huyo ni kutokana na kuwa alishindwa kufundishika, mara baada ya kocha wao Fadlu Davis kumfanyia mazoezi mengi na kuzungumza naye, lakini bado kiwango chake kilikuwa hakiridhishi.
Ahmed alisema kuwa moja kati ya wachezaji ambao wao kama uongozi walikuwa wanafikiri a kuwa atakuwa kiongozi kwa wachezaji wengine, ni yeye, lakini kutokuwa timamu kimwili kumesababisha kocha kuomba kutafutiwa mchezaji mwingine.
Alisema pia kuwa wakati wa maandalzi ya msimu mpya wa ligi walipoweka kambi kule Misri, kocha Fadlu alikuwa akimfuatilia na kuzungumza naye mara kwa mara, lakini bado hakuwa katika utimamu wa mwili.
“Kocha alizungumza naye mara kwa mara tangu alipowasili kambini lakini hakuweza kufanya zaidi atu alikuwa akishuka kila siku na ndiyo maana kocha alitaka kutafutiwa mchezaji mwingine haraka zaidi, ndipo tukamtafuta mwamba Christian Lionel Ateba”, alisema Ahmed.
Alisema pia kwamba suala la kuachana na Fredy, ni kutokana na matakwa ya kocha na ni kutokana na kutopedezwa na kiwango chake alichoonyesha kwenye mazoezi laini. Kwa sasa wamemalizana naye na hivyo wanaanza upya.
Aidha, alizungumzia juu ya kulidhishwa na kikosi chao, huku akiweka wazi kuwa msimu huu, pamoja na kuwa wanajenga timu, lakini wana mipango ya kuchua ubingwa msimu huu na kurudisha ufalme wao ambao waliupoteza kwa watani zao Yanga, lakini watahakikisha wanafanya vyema.
Mpaka sasa, klabu ya Simba imefanikiwa kucheza michezo miwili ya ligi dhidi ya Tabora United na Fountaine Gate na kufanikiwa kubeba alama zote 6 na kujikusanyia mabao 7 wakiwa juu katika msimmo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.