Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Kocha Julio. Kocha Julio.

DAR ES SALAAM

Na Nicholaus Kilowoko

Kocha Jamhuri Kihwelo amesema haoni mchezaji yeyote mzawa wa kumfananisha na mshambuliaji John Bocco, hasa kwenye nidhamu ya ndani na nje ya uwanja.
Bocco ambaye alistaafu rasmi kuichezea timu ya Simba SC na kugeukia ukocha wa timu za vijana za Simba SC, hivi karibuni alipewa shukrani za dhati na kheri katika maisha yake mapya na uongozi wa wekundu hao.
Akimzungumzia mkongwe huyo, Kocha huyo mwenye jina maarufu kama Julio alisema anaufahamu vyema uwezo wake uwanjani, pamoja na nidhamu aliyonayo ambayo imemfikisha mahali pazuri kwenye soka lake, licha ya kutocheza soka nje ya nchi.
Alisema kuwa Tanzania ina wachezaji wengi wenye uwezo mkubwa wa soka lakini nidhamu yao si nzuri, na hivyo kuwafanya washindwe kufika mbali na kujikuta wanastaafu soka wakiwa na umri mdogo.
“Mimi nimefundisha wachezaji wengi waliojaaliwa vipaji vizuri na vikubwa, lakini hawana nidhamu ikilinganishwa na Bocco.Unaweza kuwaambia wachezaji waingie kambini siku fulani, lakini cha kushangaza wanachelewa kuripoti. Bocco alipojiunga na Simba akitokea Azam FC, aliibadilisha kwa kiasi kikubwa katika eneo la nidhamu,”alisema Julio.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Klabu ya Soka ya Azam FC Thabit Zacharia maarufu kama Zaka Zakazi, alisema kwamba Bocco ataendelea kubaki katika mioyo ya mashabiki na viongozi wa Azam FC kutokana na nidhamu yake.
Alisema pia kuwa Bocco hakuwa mtu wa kupigana uwanjani ama kucheza rafu zisizo na msingi ama kuwa mtu wa starehe nje ya uwanja.
“Nakumbuka Bocco wakati yupo Azam FC, ikitokea Ligi imesimama kwa wiki moja ama mbili kupisha ratiba zingine, wachezaji wenzake wote walikuwa wanaondoka kwenye hosteli, yeye anabaki peke yake na kufanya mazoezi binafsi.Anaweza kuchukua mpira akawa anaukokota goli hadi goli. Hakuwa anaijua pombe wala starehe nyingine yoyote.”
Alisema kuwa Bocco ndiye aliyefunga mabao yaliyoiwezesha timu hiyo kutinga Ligi Kuu kwa mara ya kwanza mwaka 2008 na kisha kuchangia katika ubingwa iliyopata msimu wa 2013/14 na kukata tiketi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.