Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Simba Queens yampa jeuri Mgosi

Musa Mgosi Musa Mgosi

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Benchi la Ufundi la Timu ya Soka ya Simba Queens kupitia kwa kocha msaidizi Mussa Mgosi, ametamba kuwa atahakikisha klabu hiyo inabeba ubingwa mpaka pale yeye atakapoondoka.
Mgosi (pichani) ametamba kuwa kutokana na uwezo waliokuwa nao wachezaji wake, watahakikisha wengine kombe hilo wanaishia kuliona wakati likiwa linatangazwa tu mwanzoni mwa msimu, lakini kulichukua itakuw ni story za Abunuasi.
Alisema pia kuwa umakini wa wachezaji wake, hasa wanapokuwa mazoezini kabla ya mechi, ndiyo sababu kuu ya kuwafanya wafanikiwe kuchukua ubingwa kwa mara nyingine tena.
Mgosi alisema kuwa lengo lao ni kuhakikisha wanapoenda kushiriki michuano ya Kimataifa waweze kufanya vizuri, na hili litawezekana tu mara baada ya kufanyika kwa usajili mkubwa ndani ya klabu yao kwa kuchukua wachezaji wenye uwezo.
“Tunataka kuuvunja utawala wa Mamelods na tutajitahidi kufanya usajili mzuri ili kubeba ubingwa wa Cecafa, na kisha tutafanya tena usajili kwa ajili ya Klabu bingwa ambayo ina timu zenye wachezaji wazuri wa kiushindani”, alisema Mgosi.
Alisema pia kuwa wachezaji wao wamekuwa chachu ya kufanikiwa klabu hiyo kwenye ligi yao kutokana na usikivu waliokuwa nao mara baada ya kumalizika kwa mechi na kuandaa maandalizi ya mechi nyingine.
Klabu hiyo kwa sasa inajiandaa na michuano ya Afrika kwa wanawake, ambapo msimu uliopita hawakufanikiwa kushiriki michuano hiyo kutokana na kuukosa ubingwa wa Ligi uliobebwa na klabu ya JKT Queens.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.