Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Ten Hag amuunga mkono Ralf Rangnick

MANCHESTER, Uingereza
Meneja wa Manchester United, Erik ten Hag amesema kuwa kocha wa zamani wa muda Ralf Rangnick alikuwa sahihi kabisa kwamba klabu hiyo inahitaji kufanyiwa upasuaji wa moyo.
Ten Hag (54), aliteuliwa kuwa meneja mnamo 2022 baada ya Rangnick kutawala kwa miezi saba.
Mjerumani huyo ambaye kwa sasa anainoa timu ya Taifa ya Austria, aliiongoza United hadi nafasi ya sita kwenye Premier League, lakini alishinda mechi 11 pekee kati ya 29 alizocheza.
Ten Hag ambaye alitia saini nyongeza ya mkataba wa mwaka mmoja mwezi huu, alisema kwamba uchambuzi wa Rangnick ulikuwa sahihi.
“Rangnick alikuwa sahihi kabisa,” Ten Hag alisema katika mahojiano na gazeti la Uholanzi AD Sportwereld.
“Tumekuwa tukifanya kazi kwa bidii juu ya hili kwa miaka miwili, lakini alilosema ni sawa kabisa: ni operesheni ya kina, ngumu sana. Na nilipoanza nilijua kuwa itakuwa kazi ngumu.”
United wamefanyiwa mabadiliko makubwa nje ya uwanja tangu Sir Jim Ratcliffe apate asilimia 27.7 ya hisa za klabu hiyo Desemba mwaka jana.
Omar Berrada, Dan Ashworth, Jason Wilcox na Christopher Vivell wote wamejiunga katika nyadhifa katika ngazi ya bodi mwaka huu, wakati klabu imetoa £50m kuboresha uwanja wa mazoezi.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.