Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

ZAIKO LANGA LANGA: Bendi iliyozalisha nyota wengi wa muziki Congo DR

DAR ES SALAAM

Na Alone Mpanduka

Wiki hii tunaitazama Bendi ya Zaiko Langa Langa ambayo ilizaliwa mwaka 1970 huko nchini Congo DR (zamani Zaire).
Mwanzo kabisa ilijulikana kama Orchestra Zaiko, lakini baadaye likaibuka jina la Langa Langa kufuatia kutumbuiza kwenye vilabu vya pombe. Langa Langa ni Kilingala, kikiwa na maana ya kulewa.
Zaiko inaweza kulinganishwa na bendi ya Msondo Ngoma ya hapa nchini kwa historia zao zinavyokaribiana kwenye ukongwe na kuzalisha wanamuziki wengi mahiri. Msondo Ngoma na Zaiko Langa Langa, zimetoa wanamuziki wengi wenye majina makubwa kimuziki.
Wanamuziki nyota wa nchini humo akina Papa Wemba, Bozi Boziana, Dindo Yogo, Evoloko Ley Ley ‘Joker’, Defao Matumona, Koffi Olomide, na wengine wengi, chimbuko lao limetoka kwenye shina la Zaiko Langa Langa.
Bendi nyingi kama Isifi Lokole, Yoka Lokole, Viva la Musica, Langa Langa Stars, Zaiko Familia Dei, Choc Stars, Le Anti Choc, Le Grand Zaiko Wawa, Quartie Latin na nyinginezo nyingi, zimetoka kwenye chimbuko la Zaiko ambayo sasa inajulikana kama Zaiko Langa Langa Nkolo Mboka, yaani ‘Wakuu wa Mji’.
Idadi kubwa ya bendi zilizotokea ubavuni mwa Zaiko Langa Langa zimekuwa zikijiita ‘Ukoo wa Langa Langa’ (Clan Langa Langa).
Bendi hizo ni Isifi Lokole iliyoanzishwa na Papa Wemba, Bozi Boziana, Evoloko Jocker na Mavuela Somo, Yoka Lokole iliyoanzishwa na Papa Wemba, Bozi Boziana na Mavuela Somo.
Bendi ya Grand Zaïko Wa Wa iliyoanzishwa na Felix ‘Pepe’ Manuaku Waku aliyeungana na Shimita El Diego na Djo Poster. Bendi ya Viva La Musica iliyoanzishwa na Papa Wemba akiwa na Emeneya Mubiala na Theodore Djangi Dindo Yogo.
Bendi ya Choc Stars iliyoanzishwa na wanamuziki akina Bozi Boziana, Tshimpaka Roxy na kuungana na akina Ben Nyamabo, Carlito Lassa, na Defao Matumona.
Bozi Boziana akiungana na Deyesse Mukangi, Jolie Detta, Dodoli, Walingonda, Fifi Mofude, na wengineo, waliungana na kuanzisha bendi ya L’Orchestre Anti-Choc.
Langa Langa Stars iliyoanzishwa na Waze la Mbongo Kiamuangana Mateta ‘Verckys’, Evoloko Jocker, Tshimpaka Roxy, Emeneya Mabiala na Djo Mali.
Zaiko Langa Langa Familia Dei, ilianzishwa na akina Lengi Lenga, Ilo Pablo, Bimi Ombale, Beniko Popolipo, Petit Poisson, na Djimi Yaba.
Zaïko Langa Langa Nkolo Mboka yenyewe chini ya N’Yoka Longo, Meridjo, Oncle Bapius, Zamuangana, Nono Atalaku, Mbuta Matima, Malage de Lugendo, Adamo Ekula, Baroza, na Shiro Shiro, ikaanzisha bendi zingine za Zaiko Universel chini ya wanamuziki Meridjo na Oncle Bapius Muaka wakati bendi ya Langa Langa Rénove ikiongozwa na mwanamzuiki Evoloko Jocker.
Histori ya bendi ya Zaiko Langa Langa imekuwa ikikosolewa na baadhi ya watu, wakitaja kwamba ilianzishwa mwaka 1970.
Inasadikika kwamba bendi hiyo ilianzishwa rasmi Desemba 24 mwaka 1969 jijini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wakati huo ikijulikana kama Orchestra Zaiko.
Wakati huo muziki wa Kongo ulitawaliwa zaidi na bendi za African Jazz ya Joseph Athanase Tchamala Kabaselleh ‘Le Grand Kalle’, African Fiesta ya Nicolas Kassanda wa Mikalay maarufu kama Dk. Nico, Tout Puisant Orchestre Kinnie Jazz (TP OK Jazz) ya L’Okanga La Ndju Pene Luambo Luanzo Makiadi Franco na hata African Fiesta National ya Pascal-Emmanuel Sinamoyi Tabu, maarufu Tabu Ley Rochereau, aliyoianzisha baada ya kutengana na Dk. Nico na mwaka 1970 akaibadili jina na kuiita Orchestre Afrisa Intanationale.
Waanzilishi wa Zaiko Langa Langa walikuwa wanamuziki ambao baadhi walikuwa wanapigia bendi ndogo ndogo za mitaani, na wengine walikuwa wanafunzi.
Baadhi yao ni mpiga Konga maarufu D.V. Moanda, ambaye jina lake halisi ni Vital Moanda-di Veta Marcelin Delo, Henry Mongombe, Olemi Eshar-Eshar dem’belina, Andre Bita, Mavuela ‘Somo’ Simeon, Evoloko Lay Lay ‘Joker’, Teddy Sukami, Oncle Bapius aliyekuwa akipiga bass, Zamuangana Enock le Meilleur, baba ya wapiga solo wa kizazi kipya Kongo Felix Manuaku Waku na N’Yoka Longo Mvula, anayejulikana kama Jossart, ama Vieux Mbombas ambaye asili yake ni kutoka nchini Angola.
Hawa walikuwa wakipiga muziki wa Soukous. Katika upande wa Pop waliokuwa wakifungua pazia katika shoo zote za bendi hiyo, kulikuwa na akina Bimi Ombale, Mbuta Matima Zephirin na Mashakado Mbuta.
Hiyo ndiyo Zaiko Langa Langa, bendi kongwe nchini humo kwa sasa ambayo bado inaendelea kujikongoja, licha ya wanamuziki wengi kuondoka.
Ikumbukwe kwamba Januari mwaka huu, alifariki Nono Monzuluku ambaye alijiunga na Zaiko Langa Langa mwaka 1982 akiwa na miaka 22 tu. Baadaye bendi (Zaiko) iliongeza rapa mwingine (Doudou Adoula) miaka ya 1980 katikati kuelekaa mwishoni.
Bendi inahesabika kama Chuo cha Muziki katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa sababu bendi nyingi zinazotamba hivi sasa, ambazo zilianzishwa kuanzia miaka ya 1970, zimetoka ubavuni mwake.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.