Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Unaijua riadha ya kubeba mkeo mgongoni?

DAR ES SALAAM

Na Alone Mpanduka

Katika nchi ya Finland kuna mashindano ya kukimbia riadha, huku ukiwa umemmeba mkeo mgongoni. Mashindano hayo yalianza mnamo karne ya 19, na kuwa mchezo rasmi mwaka 1992, huku baadaye wakiruhusu raia wa nchi zingine kushiriki mwaka 1995.
Mchezo huo ambao umetokea kupendwa na wengi hadi kupewa hadhi ya Kimataifa, unahusisha wapenzi au wanandoa na lazima mke atakayebebwa awe wa mwanaume husika.
Pamoja na hayo, mwanamke atakayebebwa atatakiwa kuwa na uzito usiopungua kilo 49, na kama itakuwa pungufu, basi itabidi afungashiwe mzigo ili uzito wake ufikie kilo 49.
Sheria inasema wenza wawe na zaidi ya miaka 18, na uzito wa kilo 50 na kuna adhabu ikiwa utamuangusha mwenza wako.
Mshindi hupatikana kwa mwanaume aliyeweza kukimbia kwa kasi zaidi na mkewe kichwani, na zawadi kuu ambayo ni pombe, itatolea kwa katoni sawa na uzito wa mke wake kwa kutumia mzani maalum yaani ‘bembea’.
Wazungu wameupa mchezo huo jina la Kiingereza la ‘Wife Carrying Competition’. Si kwamba mtu hubeba mke wake, bali mwanamume hubeba mwanamke na kuanza mbio akiwa naye.
Mwanamke huyo huwa ni mwanatimu mwenza wa manamume. Mashindano haya hufanyika na kupendwa sana Finland, na ratiba yake ni Julai ya kila mwaka.
Kwa kawaida mwanaume mchezaji hutakiwa kukimbia na mzigo huo wa mwanamke umbali wa mita 254, akiwa kamuweka ama mgongoni au mabegani.
Kuna changamoto kadhaa kwenye mchezo huo, kwani maeneo ya kukimbia si tambarale, kuna maeneo yenye maji na matope na mengine makavu lakini ya milima.
Mshindi wa mashindano hayo huzawadiwa simu ya mkononi, na mke hupewa bia, na anayeshika nafasi ya mwisho anapatiwa tambi na chakula cha mbwa.
Wazo la kuanzisha shindano hilo lilipatikana mnamo karne ya 19 kupitia matukio ya kihalifu ya mtu mmoja aitwaye Ronkainen ambaye aliwashawishi vijana wenzake kuiba na kubeba gunia la mbegu ama kumbeba nguruwe na kukimbia naye.
Inaelezwa kwamba jamaa huyo alikuwa mwizi aliyeishi karibu na mwanzo wa karne ya 19, yeye pamoja na genge lake, walishambulia vijiji vya karibu na kuiba mizigo mikubwa na kisha kukimbia nayo wakiwa wameibeba kichwani.
Genge lake la uhalifu liliiba chakula na wake za watu kutoka vijijini, na kisha kuwabeba migongoni huku wakikimbia.
Mwanamume huyo aliwapa changamoto watu wake kuonyesha nguvu zake, kwanza kubeba mizigo, na pili kukimbia nayo.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.