Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Watu wa Mungu Ukraine wadai kiu ya haki, amani

KIEV,Ukraine

Watu wa Mungu nchini Ukraine, bado wanaendelea kukabiliwa na kiu ya haki na amani kutokana na mapigano ya vita yanayoendelea nchini humo, kati ya majeshi ya Serikali dhidi ya majeshi vamizi ya Urusi.
Katika mahubiri yake kwenye Adhimisho la Misa Takatifu, Mwadhama Pietro Kardinali Parolin kwa niaba yake na Askofu Msaidizi Edward Kawa wa Jimbo la Lviv la Kanisa Katoliki nchini Ukraine, alikazia muujiza unaotamaniwa ni amani nchini humo.
Kardinali huyo (pichani) alisema kuwa watu wa Mungu nchini Ukraine kama ilivyokuwa kwa Nabii Eliya, wanaitwa na kutumwa kutangaza Habari Njema ya Wokovu, inayosimikwa katika fadhila ya amani, kwani hakuna jambo ambalo haliwezekani kwa Mungu, akiwasihi Waamini kuendelea kusali ili kuombea amani Taifa lao.
“Madhabahu ni mahali ambapo panapaswa kukuza na kudumisha ari na moyo wa Sala ya Kanisa, maadhimisho ya Sakramenti za Kanisa kama sehemu ya kazi ya ukombozi.. ni mahali pa shuhuda za imani, matumaini na mapendo, kielelezo cha Kanisa linalokesha na kusali daima,”alisema Kardinali Parolin.
Alisema kuwa ni matumaini ya Baba Mtakatifu Fransisko kwamba katika madhabahu, kamwe hawatakosekana Wamisionari wa huruma, mashuhuda wa upendo wa Mungu unaookoa na kuponya! Madhabahu yawe ni mahali pa kumwilisha upendo, kielelezo cha utekelezaji wa Amri ya Upendo kwa Mungu na jirani.
Kardinali Parolin katika Ibada hiyo alifuatana na Padri Ruslan Mykhalkiv, Gombera wa Seminari ya Jimbo Katoliki la Kyiv-Zhytomir; pamoja na Padri Andriy Lehovich, Katibu Muhtasi wa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la lviv, nchini Ukraine.
Hii inaonesha kwamba hakuna jambo lisilowezekana mbele ya Mungu. Somo la pili linakazia kuhusu toba na wongofu wa ndani. Watu wa Mungu nchini Ukraine wanaitwa na kutumwa kutekeleza unabii wa kusali bila ya kuchoka, ili Mwenyezi Mungu aweze kuwaongoa wenye kiburi, wanaopandikiza mbegu ya chuki na uhasama, vita na kifo, ili waweze kusitisha vitendo hivi vinavyosigina utu, heshima na haki msingi za binadamu.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.