Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Papa awakingia kifua Wakimbizi

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Fransisko ameiasa Jumuiya ya Kimataifa kuhakikisha inaendelea, kuwapokea na kuwahifadhi wakimbizi duniani kote.
Baba Mtakatifu alitoa wito huo hivi karibuni wakati wa Siku ya Kimataifa ya wakimbizi akisema kwamba inapaswa kuwa ni fursa ya kuelekeza macho na usikivu wa kidugu kwa wale wote wanaolazimika kuyahama makazi yao kutafuta amani na usalama.
Baba Mtakatifu alisema hayo baada ya Katekesi yake katika fursa ya kuelekea kilele cha Siku hiyo inayoadhimishwa kila ifikapo Juni 20 ya kila mwaka.
Katika salamu mbali mbali baada ya katekesi, akizungumza na waamini na mahujaji waliofika katika uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, kwa, Baba Mtakatifu Fransisko, alisema kwamba jamii inapasswa kutowanyanyasa wakimbizi na wahamiaji.
“Iwe ni fursa ya kuelekeza macho ya usikivu na ya kidugu kwa wale wote wanaolazimika kuyahama makazi yao kutafuta amani na usalama. Sote tumeitwa kuwakaribisha, kuwahamasisha, kuwasindikiza na kuwaunganisha wale wanaobisha hodi kwenye milango yetu,”alisema Baba Mtakatifu Fransisko.
”Ninaomba kwamba Mataifa yafanye kazi ili kuhakikisha hali ya kibinadamu kwa wakimbizi na kuwezesha michakato ya ujumuishaji.”
Baba Mtakatifu aliwakaribisha kwa moyo mkunjufu mahujaji wanaozungumza lugha ya Kiitaliano, kwa namna ya pekee, Chama cha Marafiki wa Kardinali Celso Costantini, wakisindikizwa na Askofu Giuseppe Pellegrini wa Jimbo la Concordia-Pordenone, katika kuadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Concilium Sinense ya Shanghai.
Katika hatua nyingine, Baba Mtakatifu Fransisko amewaombea wagonjwa, wazee, wenye ndoa wapya na  hasa vijana.
Aidha alikubusha siku kuu ya Mwanzislihsi wa Shirika lake inayoandimishawa kila Juni 21, kila mwaka.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.