Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Zambia, Malawi wapata Balozi

LUSAKA, Zambia
Baba Mtakatifu Fransisko ametangaza uteuzi wa Balozi mpya wa Kitume kwa nchi mbili katika Jumuiya ya Mabaraza ya Maaskofu Wanachama katika eneo la Mashariki mwa Afrika (Association of Member Episcopal Conferences in Eastern Africa: AMECEA); Zambia na Malawi.
Baba Mtakatifu, katika ujumbe wake, alimtaja Askofu Mkuu Gian Luca Perici kuwa Balozi wa Kitume nchini Zambia na Malawi.
Anachukua nafasi ya Askofu Mkuu Gianfranco Gallone ambaye alitumwa tena Uruguay katika wadhfa huo mwanzoni mwa mwaka 2023.
Askofu Mkuu Perici aliyezaliwa mwaka 1964 nchini Italia, alipewa daraja la Upadri mwaka 1991, na ana Shahada ya Uzamivu katika Sheria za Kanisa.
Askofu Perici alijiunga na huduma ya Kidiplomasia ya Jimbo Kuu tarehe 1 Julai mwaka 2001, na amehudumu katika Baraza la Kitume huko Mexico, Haiti, Malta, Angola, Brazil, Sweden, Hispania na Ureno.
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Zambia, Padri  Francis Mukosa, alisema kuwa wamepokea uteuzi huo kwa moyo wa Kitume na kumkaribisha Askofu Mkuu Perici.
Baba Mtakatifu Paulo VI (1963-1978: wa 262), alifungua Baraza la Watawa nchini Zambia Oktoba 27 mwaka 1965, huku Askofu Mkuu Alfredo Poledrini akiwa Balozi wa kwanza wa Kitume.
Tangu mwaka 1965, Zambia ilikuwa na Mabalozi tisa wa Kitume ambao pia wanacheza kama mabalozi wa Vatican.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.