Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Alex Kachhelewa

Viongozi wa Matifa ya Afrika Mashariki (East African Community: EAC) na wale wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community: SADC), walikutana hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Mkutano Maalumu kuhusu kusaka suluhu ya mzozo wa vita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Mzozo huo ni kati ya Majeshi ya Serikali ya DRC dhidi ya Vikosi vya Waasi wa Movement For March 23- au maarufu kama M23, wanaosadikiwa kuuteka Mji wa Goma, Mashariki mwa nchi hiyo.
Katika mkutano huo ambapo Rais wa DRC Felix Tshisekedi Shilombo, yeye alishiriki kwa njia ya Mtandao, Viongozi hao walifanya maamuzi yatakayosaidia kurejesha amani  katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), iliyogubikwa na mzozo wa muda mrefu zaidi kuwahi kushuhudiwa.
Mkutano huo uliwakaribisha viongozi hao chini ya Mwenyeji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, uliohudhuriwa na wakuu wa nchi na serikali kutoka mataifa wanachama wa EAC na SADC,  ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa EAC, Rais William Ruto wa Jamhuri ya Kenya, na Mwenyekiti wa SADC, Rais Emmerson Mnangagwa wa  Jamhuri ya Zimbabwe,  hapakuwapo Rais wa Congo DRC Felix Tshisekedi, ambaye alishiriki kwa njia ya mtandao.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Joseph Mayanja, maarufu kwa jina lake la jukwaani, Jose Chameleone, ni mmoja wa waanzilishi wa muziki wa Uganda, ni mwanamuziki maarufu wa Afrobeat nchini Uganda akiwa na nyimbo nyingi zilizovuma kwa jina lake, akiimba muziki wake kwa kutumia mchanganyiko wa lugha za Luganda, Kiingereza na Kiswahili.
Mwanamuziki huyo mwenye talanta nyingi, alitoa rekodi yake ya kwanza na Ogopa DJs nchini Kenya mwaka 1996, kwa kutoa wimbo wake wa kwanza, ‘Bageya’, ambao alimshirikisha msanii wa Kenya, Redsan, wimbo ambao ulimpa mafanikio makubwa.
Jose Chameleone alizaliwa Aprili 30, 1979 mjini Kampala, nchini Uganda. Wazazi wake ni Gerald Mayanja (Baba), na Prossy Mayanja (Mama), lakini pia ana ndugu zake wanaojulikana ambao ni Douglas Mayanja a.k.a Weasel - Msanii wa Goodlyfe Crew, na msanii wa solo Pius Mayanja a.k.a Pallaso - Msanii wa muziki Henry Kasozi - Mkurugenzi Mtendaji wa Fling Fire cloth line marehemu Emmanuel Mayanja, a.k.a AK47.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Imepita miaka 21 sasa tangu kocha Jose Mourinho kupewa jina la utani la ‘Special One’, likiwa na tafsiri ya Mtu Maalum.
Jina hilo limekuwa kubwa duniani na hivyo kumtambulisha vilivyo katika medani ya soka.
Picha lilianzia mwaka 2004 ambapo Chelsea ilimtambulisha kwa waandishi wa habari kocha wao mpya, Jose Mourinho.
Raia huyo wa Ureno alijiunga na Chelsea akitoka kuwa bingwa wa Ulaya akiwa na FC Porto.
Waandishi wa habari wakamuuliza kama anaweza kurudia kufanya alichokifanya akiwa FC Porto, yaani kuahidi ubingwa na kuuchukua.

MANCHESTER, Uingereza
Tangu amepoteza mara mbili mfululizo dhidi ya Zhilei Zhang mwaka 2023, Joe Joyce, raia wa Uingereza, hajakaa sawa licha ya kushinda pambano lililofuata dhidi ya Kash Ali, lakini bado alipoteza mbele ya Derek Chisora.
Aprili 05 mwaka huu, Joe Joyce atamkabili Mwingereza mwenzake Dillian Whyte jijini Manchester, lakini kabda ya pambano hilo, Joe ambaye amewahi kuwa bingwa wa World Boxing Organisation (WBO) Interim, atapasha misuli kwa pambano la raundi nane dhidi ya Patrick Korte wa Ujerumani, Machi mosi.

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Kufuatia kuwa na mwendelezo mzuri tangu alipojiunga na klabu ya soka ya Simba, kocha raia wa Afrika Kusini Fadlu Davis, imeelezwa kuwa ameanza kuufatiliwa na viongozi wa juu wa klabu ya soka ya USM Alger, kutoka nchini Algeria.
Habari ambazo Tumaini Letu imepekua na kuzidaka zinaeleza kuwa matajiri hao kutoka Algeria wanataka kuvunja kibubu kwa ajili ya kuhakikisha kocha huyo wanamtwaa, ili akawasaidie kwenye Ligi yao pamoja na michuano ya Klabu Bingwa Afrika, kitu ambacho kinaonekana kuwachanganya Simba.
Ikumbukwe hata kocha Sead Ramovic aliwaponyoka Yanga hivi karibuni baada ya matajiri wa Belouizdad kuweka pesa nyingi mezani, dau ambalo inaelezwa liliwawia vigumu Yanga kumbakisha.

Mbunge wa Jimbo la Njombe, Deo Mwanyika (wa nne katikati), akipokea Kombe kutoka kwa nahodha wa timu ya Utalingoro, Adalbert Ngole, baada ya timu hiyo kuibuka mshindi katika Mashindano ya Kombe la Ng’ombe kwa kuichapa timu ya Uwemba 1-0 mshindi alipata zawadi ya ng’ombe. Kushoto kwa Mbunge ni Diwani wa Kata ya Utalingoro, Erasto Mpete. (Picha kwa hisani ya Bertold Njawike)

Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA), Parokia ya Kristo Mfalme – Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakishangilia moja ya matukio wakati ya Sherehe yao WAWATA Day Kiparokia, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu. (Picha na Yohana Kasosi)

Waandishi wa Habari wakiwa kanisani wakifuatilia Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Wanamawasiliano, iliyoadhimishwa katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Fatima – Msimbazi, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam. (Picha na Mathayo Kijazi)

Paroko Msaidizi wa Parokia ya Kristo Mfalme – Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Bonaventure Kisoka akizindua mashine ya mazoezi iliyonunuliwa na Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) wa Parokia hiyo wakati ya Sherehe ya WAWATA Day kiparokia. (Picha na Yohana Kasosi)

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba (aliyeshika fimbo ya Kichungaji), akiwa katika picha ya pamoja na Wanandoa wa Parokia ya Mtakatifu Paulo Mtume - Kisegese, Rufiji mkoani Pwani, jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya Somo wa Parokia hiyo, iliyoadhimishwa parokiani hapo. Kulia kwa Askofu ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Gaspar Bolongola. (Picha na Yohana Kasosi)