Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Waamini wamekumbushwa kuwalinda, kuwatunza, na kuwapenda Mapadri wao, na kamwe wasikubali Mapadri wao wachafuliwe na mtu mmoja au kikundi cha watu.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba alitoa wito huo hivi karibuni wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika, alipofanya ziara yake ya kichungaji katika Parokia ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu – Buza, jijini Dar es Salaam.
“Sasa niwaombe kitu kimoja, endeleeni na ukarimu huo. Wapendeni Mapadri wenu, nafahamu kwamba mna Mapadri wawili hapa, jitahidini kuwapenda na kuwalinda, wetendeeni mema Mapadri wenu, msikubali Mapadri wenu wapate changamoto, msikubali Mapadri wenu wachafuliwe na mtu mmoja au kikundi cha watu, hakikisheni mnaendeleza ushirikiano kati yenu na Mapadri wenu katika Parokia hii ya Buza,” alisema Askofu Musomba.

Dar es Salaam

Na Laura Chrispin

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi amewasihi Waamini kutambua kwamba Bwana Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu aliyekubali kujinyenyekeza na kutoa mwili wake usulubiwe kwa ajili ya ukombozsi wa Wanadamu.
Askofu Ruwa’ichi alitoa wito huo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya Uwaka iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Clara-Mongo la Ndege Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.
“Imetimia siku 40 tangu kuzaliwa Yesu ambaye alijitoa sadaka kwa watu wake kwa sababu ya upendo aliokuwa nao kwa kuutoa mwili wake na kukaa kwetu, ikiwa ni hali ya unyenyekevu wa Kimungu, kwani mara zote ni mkamilifu kwa watu wake,”alisema Askofu Ruwa’ichi.

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Austin Makwaia Makani Investment (AMMI), Austin Makani amewashauri Wafanyakazi wa Tumaini Media kuhakikisha wanawafahamu vyema wateja wao, kwani hiyo itawasaidia kufahamu bidhaa gani wateja wao wanazitaka.
Makani ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tumaini Media, aliyasema hayo alipokuwa akitoa mada katika Semina Elekezi kwa Wafanyakazi wa Tumaini Media kuhusu mambo ya Masoko ilioyofanyika hivi karibuni ofisini kwake Posta, jijini Dar es Salaam.
‘Kwanza kabisa ukimfahamu vyema mteja wako, basi utauza bidhaa yako. Ni lazima pia ujue kwamba mteja anahitaji bidhaa gani, na kwa wakati gani. Muuzie mteja bidhaa ambayo anaitaka, siyo bidhaa unayotaka wewe…
“Tuchukulie mfano kwa watu ambao pengine wanapenda sana kula ‘chips’, je, ukienda kuvua samaki baharini, kwenye ile ndoano yako unayotumia kuvulia, utaweka kipande cha ‘chips?’ hapana, lazima uweke kitu ambacho samaki anakipenda, siyo kitu ambacho unapenda wewe.
Kwa hiyo, hata kwenye biashara, uza kile mteja anachotaka, siyo unachotaka wewe, kwa sababu inawezekana unachotaka wewe, mteja hakitaki,” alisema Makani.

Mansa, Zambia
Parokia ya Mtakatifu Michael – Namwandwe, na Kanisa Kuu la Kupalizwa kwa Maria, Jimbo Katoliki la Mansa, imezindua rasmi Wiki ya Wagonjwa, mpango unaozingatia afya unaolenga kuhamasisha huduma za kinga na ustawi miongoni mwa Waamini.
Mpango huo uliongozwa na Padri Rodgers Chanda, Mkurugenzi wa Kichungaji, pamoja na Padri Christopher Kanja kutoka Kanisa Kuu la Kupalizwa kwa Maria, katika onyesho la uongozi kwa kielelezo, huku Mapadre wote wawili wakishiriki kikamilifu katika kupima shinikizo la damu (B.P.) na kupima malaria, wakiwatia moyo Waamini kutanguliza afya zao.

LUSAKA, Zambia

Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Zambia (Zambia Conference of Catholic Bishops: ZCCB) limezindua Kampeni ya kufuta madeni ya Mwaka wa Jubilei 2025, ikitoa wito wa msamaha wa haraka wa deni, haki ya kiuchumi, na uwazi katika usimamizi wa madeni ya Zambia.
Uzinduzi huo ulifanyika katika Kapingila House mjini Lusaka nchini humo mwishoni mwa Mkutano wa Kwanza wa Baraza Kuu wa ZCCB kwa 2025, iliyokwenda na wito wa Baba Mtakatifu Fransisko wa haki ya kiuchumi na msamaha wa madeni duniani kote kama sehemu ya Mwaka wa Jubilei 2025.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Rais wa ZCCB, Askofu Mkuu Ignatius Chama wa Jimbo Kuu Katoliki la Kasama, alisisitiza tena msingi wa Kibiblia wa mapokeo ya Jubilei, akinukuu kitabu cha Mambo ya Walawi, 25:1-8 kinachosisitiza huruma, haki na ufufuaji wa jamii zilizoelemewa na madeni yasiyo ya haki.

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Fransisko amesema kuwa mateso na mahangaiko ya mwanadamu, ni zawadi ya matumaini na uaminifu wa Mungu katika Fumbo la Pasaka, na kwamba upendo wa Mungu daima utawaandama waja wake hata wakati wa majaribu na vikwazo katika maisha yao.
Papa alitoa ujumbe huo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya 33 ya Wagonjwa Duniani mwaka 2025, iliyoadhimishwa mjini Vatican, siku ambayo ilianzishwa Mei 13 mwaka 1992, na kuadhimishwa kwa mara ya kwanza kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa Lourdes nchini Ufaransa, mnamo Februari 11 mwaka 1993.
Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa kwa ngazi ya kijimbo yaliyoadhimishwa mwaka huu wa 2025, yananogeshwa na kauli mbiu isemayo, “Na tumaini halitahayarishi, lakini hutuimarisha wakati wa majaribu,” huku Baba Mtakatifu akiwaalika watu wote wa Mungu kuwa Mahujaji wa Matumaini.

VATICAN CITY, Vatican

Wanajeshi na Polisi wametakiwa kutambua kwamba wameitwa na Mungu ili kutetea wanyonge, kulinda waamini, kuhamasisha watu kuishi kwa amani, pamoja na kuendeleza haki na amani kila mahali.
Hayo yalisemwa na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Fransisko katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Vikosi vya Wanajeshi, Polisi na Usalama, aliyoiadhimisha mjini Roma hivi karibuni.
“Ni nani bora kuliko ninyi, wanajeshi na polisi wapendwa, wavulana na wasichana, wanaweza kushuhudia vurugu na kusambaratika kwa nguvu za uovu zilizopo ulimwenguni? Mnapigana nao kila siku. Kiukweli mmeitwa kutetea wanyonge, kulinda Waamini, kuhamasisha kuishi kwa amani kwa watu…
“Kila mmoja wenu anafaa kwa nafasi ya ulinzi, ambaye anatazama mbele sana, ili kuepusha hatari na kuendeleza haki na amani kila mahali. Ninawasalimu ninyi nyote kwa upendo mkuu, Ndugu wapendwa, ambao mmefika Roma kutoka sehemu nyingi za dunia kusherehekea Jubilei yenu maalum…..

DAR ES SALAAM

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mitihani ya kuhitimisha Kidato cha Nne, Tanzania (CSEE) ilifanyika Novemba 11 hadi 29, 2024.
Matokeo yakatangazwa rasimi Januari 23, 2025 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (National Examinations Council of Tanzania: NECTA) Dk. Said Mohammed kupitia hafla na Waandishi wa Habari.
Taarifa iliyotolewa na Mtendaji Mkuu wa NECTA, ilionyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia tatu (3) kutokana na watahiniwa wengi kufaulu.
Hiyo inamaanisha kuwa kati ya watahimiwa 516,695, kati ya hao watahiniwa 477,262 wamefauli kwa madaraja: I, II, III na IV; ikiwa ni ufaulu wa asilimia 92.37 kulinganisha na matokeo ya mitihani ya 2023 yenye ufaulu wa asilimia 89.36 tu.
Kadhalika, ufaulu kwa madaraja ya I, II na III ni watahiniwa 221,952 sawa na asilimia 43, wakati mwaka 2023 walikuwa watahiniwa 197,426 sawa na asilimia 37.4 tu.
Vile vile, matokeo yameonyesha kuwa waliopata daraja la nne (iv) pamoja na waliopata alama (sufuri) wamepungua kulinganisha na matokeo ya mwaka 2023; hivyo kuashiria ongezeko la asilimia 5.6 wa ubora wa kufaulu.
Hata hivyo, Katibu Mtendaji, NECTA alibainisha kuwa kwa matokeo ya mwaka 2024, watahiniwa 67, NECTA imelazimika kufuta matokeo yao kutokana na udanganyifu wakati wakifanya mitihani.

DAR ES SALAAM

Na Alex Kachhelewa

Viongozi wa Matifa ya Afrika Mashariki (East African Community: EAC) na wale wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community: SADC), walikutana hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Mkutano Maalumu kuhusu kusaka suluhu ya mzozo wa vita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Mzozo huo ni kati ya Majeshi ya Serikali ya DRC dhidi ya Vikosi vya Waasi wa Movement For March 23- au maarufu kama M23, wanaosadikiwa kuuteka Mji wa Goma, Mashariki mwa nchi hiyo.
Katika mkutano huo ambapo Rais wa DRC Felix Tshisekedi Shilombo, yeye alishiriki kwa njia ya Mtandao, Viongozi hao walifanya maamuzi yatakayosaidia kurejesha amani  katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), iliyogubikwa na mzozo wa muda mrefu zaidi kuwahi kushuhudiwa.
Mkutano huo uliwakaribisha viongozi hao chini ya Mwenyeji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, uliohudhuriwa na wakuu wa nchi na serikali kutoka mataifa wanachama wa EAC na SADC,  ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa EAC, Rais William Ruto wa Jamhuri ya Kenya, na Mwenyekiti wa SADC, Rais Emmerson Mnangagwa wa  Jamhuri ya Zimbabwe,  hapakuwapo Rais wa Congo DRC Felix Tshisekedi, ambaye alishiriki kwa njia ya mtandao.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Joseph Mayanja, maarufu kwa jina lake la jukwaani, Jose Chameleone, ni mmoja wa waanzilishi wa muziki wa Uganda, ni mwanamuziki maarufu wa Afrobeat nchini Uganda akiwa na nyimbo nyingi zilizovuma kwa jina lake, akiimba muziki wake kwa kutumia mchanganyiko wa lugha za Luganda, Kiingereza na Kiswahili.
Mwanamuziki huyo mwenye talanta nyingi, alitoa rekodi yake ya kwanza na Ogopa DJs nchini Kenya mwaka 1996, kwa kutoa wimbo wake wa kwanza, ‘Bageya’, ambao alimshirikisha msanii wa Kenya, Redsan, wimbo ambao ulimpa mafanikio makubwa.
Jose Chameleone alizaliwa Aprili 30, 1979 mjini Kampala, nchini Uganda. Wazazi wake ni Gerald Mayanja (Baba), na Prossy Mayanja (Mama), lakini pia ana ndugu zake wanaojulikana ambao ni Douglas Mayanja a.k.a Weasel - Msanii wa Goodlyfe Crew, na msanii wa solo Pius Mayanja a.k.a Pallaso - Msanii wa muziki Henry Kasozi - Mkurugenzi Mtendaji wa Fling Fire cloth line marehemu Emmanuel Mayanja, a.k.a AK47.