Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Remigius Mmavele

Nyboma Mwan’dido Danos David Laurent Canta, alizaliwa Desemba 24, 1952 katika mji wa Nioki uliopo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mkongwe huyu wa muziki aliyeanza muziki akiwa na umri wa miaka 18, amejizolea sifa ulimwenguni kote kutokana na sauti yake ya dhahabu.
Alianza muziki mwaka 1969 alipojiunga na bendi ya Baby National iliyokuwa inaongozwa na Freddy Mulongo. Akiwa katika bendi hiyo, Nyboma alipata fursa ya kutunga wimbo wake wa kwanza unaoitwa ‘Apolosa.Baada ya hapo alijiunga na bendi inayoitwa wa Super Mosinzo.
Akiwa katika bendi hiyo, Nyboma alipata wadhamini wawili, ambao ni Achille Ngoy ambaye alikuwa Mkurugenzi anayehusika na sanaa kwenye Gazeti la Likembe. Mdhamini mwingine ni Bavon Marie-Marie, mdogo wake Franco Luambo.
Bavon Marie-Marie alikuwa na matumaini makubwa kwa Nyboma kwa kuwa alikuwa na fikra ya kuanzisha bendi yake aliyotaka iitwe  ‘Bana 15 Ans’ bendi ambayo alikuwa na kusudio la kumchukua Nyboma kuwa mwimbaji wake kinara.
Isivyo bahati, Bavon Marie-Marie akafariki ghafla, kifo kutokana na ajali ya gari aliyokuwa akiendesha, na huo ndio ukawa mwisho mipango yake yote, na marehemu Bavon. Akiwa bado Mtu ambae anajitafuta, Nyboma alijiunga na kundi la Negro Succès ambako ndiko alikoanza kujiimarisha zaidi kimuziki.
Mwaka 1970, baada ya kifo cha Bavon ambaye alikuwa kiongozi mwenza wa kundi la Negro Succes, Nyboma aliondoka kwenye kundi hilo, na mwaka 1972 akajiunga na kundi la “Bella-Bella” lililokuwa linaongozwa na wanandugu wawili  Maxime na Emile Soki lililokuwa chini ya lebo ya Verckys’s.
Akiwa katika kundi hilo, alitunga nyimbo LILI, PETE TOSI TOLATA, MBUTA. Wimbo Mbuta ndio uliotokea kupendwa na wapenzi wengi wa muziki. Katika wimbo huo, Nyboma ameshirikiana na Pepe Kalle.
Baada ya muda, ukatokea mtafaruku kati ya Maxime Soki na Verckys Kiamuangana uliosababishwa na kile kinachoelezwa kuwa kundi la “Bela-Bela” likiwa chini ya LEBO (VÉVÉ), Maxime Soki, hajazingatia maelekezo ambayo alipewa na LEBO “VÉVÉ”.
Wanamuziki wa Kundi la “Bella-Bella” walitakiwa kwenda Mjini Lubumbashi kufanya onyesho kutokana na mkataba, lakini badala ya kwenda Lubumbashi, Maxime Soki yeye alichukua usafiri akaondoka na kundi hilo wakaenda kufanya onyesho katika mji wa Matadi.
Kitendo hicho kilimkasirisha sana “Verckys Kiamuangana,” akaamua kumsimamisha kazi kwa muda Maxime Soki. Kitendo hicho kilitafsiriwa kama udhalilishaji, na Maxime Soki na hakukubaliana na uamuzi huo, hivyo akaamua kujiondoa kwenye lebo ya Veve.
Baada ya kufanya uamuzi huo, Maxime Soki alijaribu kumshawishi Nyboma aongozane nae, ila Nyboma alikataa pendekezo hilo. Maxime Soki, akaondoka akiwa na ndugu yake Emile pamoja na mpiga gita Shaba Kahamba.
Mwaka 1973 , Nyboma akaanzisha bendi ya Lipua-Lipua akiwa na Pepe Kalle. Mwaka huo huo wa 1973 akateuliwa Msanii Bora wa Mwaka 1973, na Mwaka 1974, akateuliwa tena kuwa msanii bora.
Nyboma na Pepe Kalle waliamua kuiita bendi yao jina la Lipua Lipua kwa sababu Lipua-Lipua kwanza ni wimbo uliotungwa na “MELEMBU” wakati bado wakiwa katika bendi ya Bella-Bella. Lipua-Lipua ikimaanisha “Wasichana wasiodumu kwenye mahusiano na Mtu mmoja”, leo na huyu, kesho na mwengine.
Kitendo chao cha kutoongozana na Okestra BELLA-BELLA na kuamua kubaki chini ya uongozi wa LEBO “VEVE”, ndicho kilichosababishwa wakapachikwa pia Jina la Lipua-Lipua.
Akiwa na bendi ya Lipua-Lipua, ,Nyboma alitunga nyimbo nyingi, zikiwemo:’ Amba, Mwaluke, Ayidjo, Ditutala, Niki Bue’.
Bendi ya Lipua-Lipua ilikuwa na wanamuziki hawa : Rickos Tonton (Solo Gita), Mulembu (Mwimbaji), Assossa Tshimanga (Mwimbaji), Barly Barliento (Bass Gita), Bisikita Piet (Rhythm Gita), ambae baadae   mpiga rhythm Mombassa Vata, akaja kuchukua nafasi yake.
Jina Lipua-Lipua likaleta shida baada ya bendi hiyo kuamua kujiondoa kwenye lebo ‘Veve’, kitendo ambacho Verckys Kiamuangana hakuridhishwa nacho, akawaomba wabaki chini ya lebo hiyo, ikashindikana. Kuona hivyo, akawazuia kutumia jina Lipua-Lipua akawaeleza kwamba hawana ruksa ya kutumia jina hilo ambalo kwake yeye ni hatimiliki ya LEBO yake (VEVE / SAKUMUNA).

NEW YORK, Marekani
Mwanariadha wa mbio za Olimpiki nchini Marekani, Fred Kerley, alipigwa risasi na kukamatwa na polisi kufuatia makabiliano na maafisa huko Miami, Florida.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 ambaye alishinda shaba ya mita 100 katika Michezo ya Paris ya majira ya kiangazi mwaka jana, anakabiliwa na mashtaka ya kutotumia nguvu, kupinga afisa wa polisi, na uvunjifu wa amani kufuatia tukio hilo la Alhamisi jioni.
Maafisa walikuwa wakichunguza tukio jingine wakati Kerley alipowaendea kwa tabia ya uchokozi juu ya wasiwasi kuhusu gari lake, kulingana na ripoti ya polisi.
Ripoti hiyo ilisema Kerley aliendelea kuwapinga maafisa na kutumia harakati za kukwepa kukamatwa kabla ya kupigwa mieleka chini na maafisa wanne.
Vyombo vya habari vya ndani huko Miami viliripoti, nje kwamba siku ya Ijumaa Kerley alifika mahakamani na sasa ameachiliwa kwa dhamana.
Pamoja na shaba yake huko Paris, Kerley pia alishinda medali ya fedha ya mita 100 kwenye Michezo ya Tokyo mnamo 2021, na dhahabu kwenye Mashindano ya Dunia ya 2022.
Pia, ameshinda medali za dhahabu za dunia za 4x100m na 4x400m, na amerekodi muda wa sita wa kasi wa mita 100 katika historia kwa sekunde 9.76.

MELBOURNE, Australia
Novak Djokovic anasema bado anapata kiwewe anapotembelea Melbourne, miaka mitatu baada ya kufukuzwa kwa sababu ya kanuni za Covid-19 za Australia.
Djokovic, ambaye hakuchanjwa dhidi ya virusi hivyo, visa yake ilifutwa na serikali ya Australia kwa misingi ya afya na utaratibu mzuri.
Alilazimika kukaa katika hoteli ya uhamiaji kwa siku tano, huku akikata rufaa bila mafanikio dhidi ya uamuzi huo, na hatimaye kulazimika kuondoka nchini humo, kumaanisha kwamba alikosa michuano ya Australian Open 2022.
Djokovic alirejea Melbourne mwaka uliofuata, vizuizi vya Covid vikipunguzwa, na akashinda Grand Slam kwa mara ya 10 ya rekodi.
“Mara kadhaa ya mwisho nilipotua Australia kupitia udhibiti wa pasipoti na uhamiaji, nilikuwa na kiwewe kidogo kutoka miaka mitatu iliyopita, lakini athari zingine bado hukaa pale ninapopitisha udhibiti wa pasipoti, nikiangalia tu ikiwa kuna mtu kutoka eneo la uhamiaji anakaribia”, alisema Djokovic.

DAR ES SALAAM

Na Deus Helandogo

Raga, maarufu kama Rugby, ni mchezo ulioanzishwa mwanzoni mwa karne ya 19 katika Mataifa ya Uingereza na Marekani, na una namna nyingi ya kuchezwa, kama vile kwa kutumia mikono pamoja na miguu, huhusisha wachezaji 15 kwa kila upande wa timu shindani
Mchezo huu ni maarufu sana kwenye Mataifa ambayo yana shabihiana kiutamaduni na Taifa la Uingereza, ikiwemo Umoja wa Jumuiya ya Madola kama vile Austalia, Kenya, Afrika Kusini, Canada na Namibia, kwenye baadhi ya Mataifa mchezo huu ni mchezo ambao una sifa ya kuwa mchezo wa Kitaifa
Raga ilianza pamoja na mchezo wa mpira wa miguu, na baadae sheria za michezo hiyo miwili zikatofautiana  na kuwa michezo miwili tofauti. Raga ikabaki ikichezwa kwa kutumia mikono na miguu, huku mpira wa miguu akaanza kuchezwa  kwa kutumia miguu tu
Mpira unaotumika kuchezea Raga umetengenezwa kwa mfumo wa umbo mviringo, mithili ya yai unaoweza kubebeka na kukimbia nao, ukiwa mkononi, na inapotokea kuurusha haumsumbi mchezaji huurusha kwa haraka
Takwimu zinaonesha kuwa mchezo huu umezidi kukua kwa kasi ulimwenguni  kwani huchezwa na kila jinsia na umri wowote. Mwaka 2023, ilithibitika kuwa zaidi ya watu milioni kumi (10) hucheza  mchezo huu  duniani kote.
Na katika kipindi hicho, watu milioni 8.4 walikuwa wamesajiliwa na Chama cha mchezo huo duniani ambacho kifupi chake ni (IRFB), na Mataifa 116 yana vyama vinavyoongoza mchezo wa Raga duniani kote.
Kuanzia miaka ya 1863, mchezo huu ulikuwa unachezwa kama ridhaa kwa kujifurahisha zaidi, na siyo kazi rasmi ambayo ilikuwa na maslahi, mpaka ilipofika mwaka 1995 ndipo sheria mpya zilitungwa na kuurasimisha mchezo huu ambapo ulianza kulipa wachezaji, makocha  na waamuzi,  hivyo watu wakaanza kunufaika na mchezo wenyewe.
Mchezo wa kwanza wa Raga wa Kimataifa  ulichezwa mnamo 27 Machi, 1871 kati ya Scotland na Uingereza huko Edinburgh, Scotland ilishinda mchezo huo kwa bao moja, hadi kufikia mwaka 1881, ambapo Ireland na Wales zilikuwa na timu za uwakilishi katika mashindano ya Kimataifa
Mashindano muhimu zaidi katika mchezo wa Raga ni Kombe la Dunia la Raga, mashindano ya wanaume, ambayo yamekuwa yakifanyika kila baada ya miaka minne tangu kuzinduliwa kwa michuano hiyo mnamo mwaka 1987.
Afrika Kusini ndiyo Mabingwa watetezi baada ya kuifunga New Zealand 11-12 katika fainali ya Kombe la dunia la Raga 2023 nchini Ufaransa.
Lakini katika historia, Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya kushinda makombe, kwani imeshinda Kombe la Dunia mara nne (1995, 2007, 2019 na 2023).
New Zealand imeshinda taji hilo mara tatu (1987, 2011 na 2015); Australia imeshinda mara mbili (1991 na 1999); na Uingereza mara moja (2003).
England ndio timu pekee kutoka Kaskazini mwa Bara la Ulaya ambayo imeshinda Kombe la dunia la Raga
Kombe la Dunia la Raga limeendelea kukua tangu kuanzishwa kwake mwaka 1987 kwani mashindano ya kwanza, ambayo timu 16 zilishiriki ilionyeshwa kwa nchi 17, na jumla ya watazamaji milioni 230 wa televisheni, walishuhudia. Mauzo ya tiketi wakati wa hatua za bwawa na fainali za mashindano hayo, yalikuwa chini ya milioni Kombe la Dunia la mwaka 2007 lililoshindaniwa na nchi 94, na mauzo ya tiketi yalikuwa  3,850,000.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Mshambuliaji wa Yanga, Kennedy Musonda, amefunguka juu ya ukweli wa maisha yake binafsi, huku akiweka wazi kuwa malengo yake ya kwanza yalikuwa ni kuwa Mhandisi, lakini mwisho wa siku mambo hayakwenda vile ambavyo alikuwa anataka.
Nyota huyo (pichani) ambaye anamudu uwanjani kwenye nafasi ya mshambuliaji wa kati na pembeni alisema kuwa mwanzo alikuwa anataka kuwa Mhandisi kabla ya soka kummbadilishia mwelekeo na hatimaye akaacha kile alichokuwa anatamani kukifanya.
Musonda alisema kuwa alitakiwa kwenda chuo kwa ajili ya kusomea Uhandisi, lakini soka lilimbadilishia mfumo wa maisha na sasa amekuwa mfumania nyavu uwanjani.
“Mwanzo nilitakiwa kwenda chuo kusomea Usanifu wa Majengo, lakini mpira ulinipa mwelekeo mwingine wa maisha ndiyo kama hivi kwa sasa, nachezea Yanga”, alisema Musonda.
Kuhusu kazi yake na majukumu yake uwanjani kama mchezaji sasa wa Yanga, Musonda amepanga kufunga mabao zaidi na kuisaidia Yanga kushinda kila mchezo wake msimu huu.
Lakini, kwa upande mwingine Musonda alifunguka juu ya ugumu anaoupata wa namba tangu asajiliwe ndani ya Yanga huku akiweka wazi kuwa juu ya mkanganyiko wa mashabiki wake, wanaojiuliza juu ya kwa nini hafunguki akiwa na Yanga huku kwenye timu yake ya Taifa akifunga.
Musonda alisema kuwa kwenye timu yake ya Taifa, anapata nafasi sana na ndiyo maana anafunga sana, lakini kwa upande wa klabu imekuwa tofauti, kwani hapati nafasi sana. Mpaka sasa amecheza mara 20 pekee, hali inayopelekea kupata changamoto ya kupachika mabao.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Wakati wa kufanyika kwa droo na hata baada ya kuanza kwa michuano ya Afrika ambayo Simba na Yanga wanashindania Ubingwa, mashabiki wengi na wadau wa soka walikuwa na maoni tofauti juu ya timu zao wakizichambua katika viwango vya juu, lakini kwa sasa hali imekuwa tofauti, kwani maji na unga vimeanza kujitenga.
Mpaka sasa bado mambo hayajaenda sawa kwa klabu za Tanzania ambazo zinashindana katika michuano hiyo ya Afrika msimu huu, tofauti na ilivyotarajiwa.
Simba inashiriki Kombe la Shirikisho kutokana na kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi msimu uliopita, huku watani zao klabu ya soka ya Yanga ikishiriki michuano ya Klabu Bingwa Afrika, na hii ni baada ya kuwa Mabingwa msimu iliopita katika Ligi Kuu Soka Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya soka ya Simba, Ismail Aden Rage, aliweka wazi kuwa klabu ya soka ya Yanga bado hawajawa katika kiwango bora kama walivyokuwa katika misimu miwili ya nyuma na hilo limechangia kuwepo kwenye nafasi waliyopo sasa.
Rage alisema na kuweka wazi mara baada ya kufanya tathmini yake katika mchezo wao uliopita waliocheza katika dimba la Benjamini Mkapa, akidai kuwa walipata nafasi nyingi za kufunga, lakini walishindwa kuzitumia ipasavyo dhidi ya wapinzani wao TP Mazembe.
Alisema kuwa bado Yanga wana safu mbovu ya ushambuliaji ambayo inawasababisha washindwe kupata matokeo chanya kwenye mechi zake msimu huu.
Yanga ilipata ushinda wa mabao 3-1 dhidi ya TP Mazembe katika mechi ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, iliyochezwa Jumamosi, Januari 4 mwaka huu.
Kuhusu Simba, Rage alisema kuwa, bado inajitafuta, japokuwa imefanya vyema katika michezo yake mitatu kati ya minne, ambayo mpaka sasa imeshacheza katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho, wakipata ushindi huku wakifungwa mchezo mmoja.
Watanzania wengi bado hawana matumaini ya dhati juu ya klabu hizo kutokana na nafasi walizokuwa nazo kwenye misimamo ya makundi yao, huku kwa sasa ni mahesabu ya vidole tu ndiyo yaliyobaki.
Yanga kwa kuchechemea katika michezo minne, ameshinda mchezo mmoja, akipata sare mchezo mmoja huku akifungwa michezo miwili, na amekusanya alama nne, akishika nafasi ya tatu katika msimamo wa kundi lake michuano ya Klabu Bingwa Afrika, hatua ya makundi.
Simba nayo ni kama wanaingia wanatoka, kwani katika michezo minne, ameshinda michezo mitatu, akifungwa mchezo mmoja, akijikusanyia alama tisa, akishika nafasi ya pili kwenye hatua ya makundi katika michuano ya Kombe la Shirikisho.
Timu zote hizo zinatarajiwa kutupa karata zao nyingine katika viwanja vya ugenini January 12 ambapo klabu ya Simba watawafuata Bravos ya Angola huku klabu ya soka ya Yanga ikiwafuata Al Hillal ya kutokea kule Sudan.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akiwa katika picha ya pamoja na Kamati Tendaji ya Parokia ya Mtakatifu Cesilia, Kisarawe II, jimboni humo. Kulia kwa Askofu ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Roger Kamuzinzi, na kushoto ni Paroko Msaidizi. (Picha na Yohana Kasosi)

Waamini wa Parokia ya Bikira Mama wa Kanisa, Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sikukuu ya Krismas iliyoadhimishwa hapo hivi karibuni.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akibariki matoleo wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Noeli katika Parokia ya Mtakatifu Agustino – Salasala. Kushoto ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Peter Assenga. (Picha na Mathayo Kijazi)

Padri Denis Kunambi, Paroko wa Parokia ya Roho Mtakatifu Segerea, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam akikabidhi vitendea kazi kwa Kamati Tendaji ya Kigango cha Kuzaliwa Bikira Maria, Kisukuru, Parokia ya Roho Mtakatifu, Segerea, wakati wa Misa Takatifu ya Uzinduzi wa Kigango hicho.