Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Mwanakwaya Tina Turner alivyotikisa miaka ya 70 na 80

Tina Turner Tina Turner

DAR ES SALAAM

Na Alone Mpanduka

Jina lake halisi ni Anna Mae Bullock, japo tunamfahamu zaidi kama Tina Turner. Pamoja na kufahamika kama mtunzi na mwimbaji wa muziki, pia alifanya vyema kama mwigizaji wa filamu na mwandishi wa vitabu.
Alizaliwa Marekani mwaka 1939 ambapo alikua na dada zake wawili.Kwakuzaliwa ni raia wa Marekani lakini mwaka 2013 alibadili nyaraka zake na kuwa raia wa Uswisi.
Alizaliwa Anna Mae Bullock tarehe 26 mwezi Novemba mwaka 1939, katika jamii ya vijijini ya Tennessee ya Nutbush, ambayo alielezea katika wimbo wake wa 1973 “Nutbush City Limits,” kama “jamii ya zamani tulivu, na mji wa farasi mmoja.”
Akiwa binti mdogo alikua akiimba katika kwaya ya kanisani kwenye Kanisa la Kibabtisti huko Nutbush Marekani
Aliishi na bibi yake ambaye alikuwa ameshika sana dini, na katika moja ya Makala ya maisha yake inayofahamika kama I, Tina alinukuliwa akisema kuwa wazazi wake hawakumpenda na hawakumhitaji.
Katika maisha yake ya ujana na kabla ya kuwa Tina Turner alishawahi kufanya kazi za vibarua kama vile nesi msaidizi na mfanyakazi wa kazi za ndani.
Katika harakati za kimuziki, safari yake ilianza baada ya kuvutiwa na mwimbaji Ike Turner, ambaye alikuwa akiimba na bendi ya ‘Kings of rythim’. Sikumoja alipata fursa ya kushika kipaza sauti mbele ya mwimbaji huyo, akapewa fursa ya kuimba zaidi, na siku hiyo alibaki akiimba usiku mzima.
Tangu siku hiyo, aliendelea kumfunza namna ya kuimba na kutoa burudani.Hivyo, wimbo wake wa kwanza kurekodi ilikuwa ni 1958 uliitwa ‘Boxtop’ na wakati huo jina lake la stejini alitumia ‘Little Ann’.
Aliandika wimbo wake wa ‘a fool in love’ kwa ajili ya msanii Art Lassiter lengo, ikiwa yeye mwenyewe aimbe kama msaidizi, lakini bahati mbaya au nzuri, msanii huyo aliyelengwa hakufika. Ikamlazimu Little Anna kurekodi mwenyewe, kwani tayari alikuwa amelipia muda wa studio.
Hapo ndipo maisha yake yalipobadilika. Wimbo huo ulinunuliwa kwa dola $25,000 kama malipo ya awali tu. Hii ikapelekea Ike Tuner kumbatiza jina la stejini “TINA”. Baadae Ike Turner alimuongezea jina lake la mwisho ‘turner’ kisha akamsajili kisheria ili kulinda haki zake endapo mwanamuziki huyo angetaka kujiondoa chini ya menejimenti yake.
Endapo Bullock angeondoka, basi jina la Tina Turner bado lingebaki kuwa hakimiliki ya Ike, na angemuweka msanii mwingine yeyote kwa jina hilo hilo.
Hivyo, kuanzia hapo Anna Mae Bullock akatambulika rasmi katika jukwaa la muziki kimataifa kama Tina Turner.
Baadae, Tina aliolewa na Ike Turner mumewe ambaye walikuwa wakifanya muziki pamoja. Na baada ya takriban miongo miwili ya kufanya kazi na mume wake aliyemshutumu kwa unyanyasaji waliachana, ambapo Tina alibaki na magari mawili tu, pamoja na jina lake.
Baada ya kuachana, Tina aliibuka kama msanii wa kujitegemea na akawa mmoja wa wasanii wa pop wakubwa wa miaka ya 1980 na albamu yake ya ‘Private Dancer’.
Taarifa za kifo cha Tina Turner zilitikisa ulimwengu mwezi Mei mwaka jana, ambapo vyombo mbalimbali vya habari kimataifa vilitangaza taarifa za mwanamuziki huyo kuaga dunia akiwa nchini Uswisi katika umri wa miaka 83
Iliripotiwa kuwa msanii huyo alikuwa na afya dhoofu katika miaka ya hivi karibuni, kwani aligunduliwa na saratani ya utumbo mnamo 2016, na kupandikizwa figo mwaka 2017.
Taarifa za kifo chake zilitangazwa kupitia mtandao wake wa Instagram, ambapo iliandikwa:
“Ni kwa huzuni kubwa kwamba tunatangaza kufariki kwa Tina Turner. Kwa muziki wake na shauku yake isiyo na kikomo ya maisha, alivutia mamilioni ya mashabiki ulimwenguni kote na kuwatia moyo nyota wa kesho. Leo tunasema kwaheri kwa rafiki mpendwa ambaye anatuachia kazi yake kuu zaidi: muziki wake. Huruma zetu zote za dhati ziende kwa familia yake. Tina, tutakukumbuka sana”.
Wafuasi wake kutoka maeneo mbali mbali duniani walimiminika katika mitandao ya kijamii kutuma salamu za rambi rambi, huku vituo vya redio na televisheni vikicheza nyimbo zake kwa bidii kubwa kumuenzi.
Tina Turner, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 83, aliunda rekodi nyingi za R&B, funk, rock na pop, zote zikiwa na uwezo wake wa kipekee wa sauti.
Nyimbo hizo zinafuatilia hadithi yake kutoka kwa ushirikiano wake usio na furaha na mumewe wa kwanza Ike, hadi miaka ya 1980 kurudi kwa hisani ya kikundi cha pop cha synth cha Uingereza.
Miaka ya 80, ilishuhudia nyimbo zake kadhaa zikiingia kwenye Top 40, zikiwemo “Typical Male,” “The Best,” “Private Dancer” na “Better Be Good To Me.”
Tamasha lake la 1988 mjini Rio de Janeiro, Brazil, lilivutia watu 180,000, ambalo linasalia kuwa moja ya hadhira kubwa zaidi ya tamasha kwa msanii yeyote.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.