Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Agostino Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Peter Assenga, akiwa katika picha ya pamoja na Watawa wa Kike, Viongozi wa Kamati Tendaji na Wakatekumeni baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kesha la Pasaka, iliyofanyika parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi)

Dekano wa Dekania ya Mtakatifu Thomas More, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Romwald Mukandala ambaye pia ni Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Kizito Kilongawima, jimboni humo akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Kamati Tendaji na wa Vyama vya Kitume baada  ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Pasaka iliyoadhimishwa Parokiani hapo.

Dar es Salaam

Na Remigius Mmavele

Mwanamuziki Jean – Pierre Gina wa Gina ni mtoto wa Corneille EFONGE mwenye asili ya MONGO, kutoka mkoa wa Equateur na wa Élise LISIMO, mwenye asili ya Mongando (familia ya Justin Disasi),

Jean-Pierre EFONGE akiwa mdogo alionyesha ishara za uwezo mkubwa wa muziki. Alizaliwa Mei 13, 1953 katika Jiji la Kinshasa.
Akiwa na chombo chenye nguvu cha kuimba, Efonge alijiunga na Kwaya ya Parokia ya Mtakatifu Paulo, katika mji wa Barumbu mjini Kinshasa akiwa na umri mdogo sana.

ANKARA, Uturuki
Kocha Jose Mourinho ametoa heshima za dhati za kuguswa na kifo cha Baba Mtakatifu Fransisko, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 88.
Mourinho, ambaye kwa sasa anainoa Fenerbahce lakini hapo kabla amewahi kuzinoa Chelsea, Tottenham na Manchester United za Uingereza, alitumia ukurasa wa Instagram kumuenzi Baba Mtakatifu  Fransisko.
Mreno huyo aliandika: “Ili kuwa mkuu, zaidi ya yote unahitaji kujua jinsi ya kuwa mdogo. Unyenyekevu ni msingi wa ukuu wa kweli. Papa Fransisko. Matumaini ni mwanga usiku. Grande Papa.”
Baba Mtakatifu ambaye aliugua ugonjwa wa mapafu na sehemu ya pafu moja kuondolewa akiwa kijana, alilazwa katika hospitali ya Gemelli mnamo Februari 14 kwa shida ya kupumua ambayo ilikua ni nimonia.
Alitumia siku 38 huko, muda mrefu zaidi wa kukaa hospitalini kwa upapa wake wa miaka 12.
Vilabu kadhaa vya Ligi Kuu ya Italia, Serie A vilituma salamu za heshima kwa Papa, kufuatia kifo chake ikiwemo timu kongwe ya AS Roma.
“Roma inaungana na kuomboleza kifo cha Papa, msiba ambao unahuzunisha sana jiji letu na ulimwengu mzima,” Roma ilisema katika taarifa.

NEW YORK, Marekani
Mchezaji wa zamani wa NBA na mwanaharakati wa haki za binadamu Enes Kanter Freedom, amesema kuwa Baba Mtakatifu Fransisko ni zaidi ya kiongozi wa kiroho duniani na ishara ya matumaini na amani.
Mchezaji huyo wa Kiislamu alieleza kuwa alianzisha uhusiano wa maana na kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki, jambo ambalo lilimpa msukumo wa kuanzisha kambi ya mpira wa kikapu mjini Vatican, na kuwaleta pamoja watoto wa imani tofauti.
“Michezo huwaleta watu pamoja. Haijalishi historia yako, dini yako, rangi yako, yeyote yule,” Freedom aliiambia NewsNation.
“Tulileta watoto wa Kiislamu, watoto wa Kikristo, watoto wa Kiyahudi, na tulikuwa na wakati mzuri.”
Freedom alikumbuka ushirikiano wake na Papa, ikiwa ni pamoja na wakati ambapo Baba Mtakatifu alipomuomba asimame, ili aone urefu wa mchezaji wa mpira wa vikapu.
“Kila wakati ninapomwona, bila shaka aliweka tabasamu usoni mwangu,” alisema.
Alisema kwamba viongozi kutoka kote duniani wamekuwa wakitoa heshima kwa Papa tangu kifo chake.

Dar es Salaam

Na Arone Mpanduka

Mshindi wa pili wa mbio za Boston Marathon Alphonce Felix Simbu, amesema kuwa kifo cha Baba Mtakatifu Fransisko kimeleta simanzi kubwa ulimwenguni, hasa kwa Wakatoliki.
Akizungumza na Tumaini Letu kwa njia ya simu, Simbu alisema kwamba kifo chake pia kimeleta pigo kubwa kwa wanamichezo kwa kuwa alikuwa mpenda michezo enzi za uhai wake.
“Sijapata nafasi ya kumfuatilia sana kwa upande wa michezo, lakini nimekuwa nikisikia kwamba alikuwa mdau mkubwa wa michezo mbalimbali. Mimi ninamuombea kwa Mungu apate pumziko la milele,”alisema.
Hivi karibuni Simbu aliandika historia mpya katika mbio za kilomita 42 kwa kushika nafasi ya pili, mbio za Boston Marathon zilizofanyika huko Massachusetts, Marekani.
Alimaliza mbio hizo kwa muda wa saa 2:05:04, akitanguliwa kwa sekunde chache na Mkenya John Korir aliyeibuka kidedea kwa muda wa saa 2:04:45, ikiwa ni muda wa pili kwa kasi zaidi katika historia ya mbio hizo.
Katika mbio hizo, Simbu alionesha ushindani wa hali ya juu, akiibuka kinara kutoka kwa kundi kubwa la wanariadha waliotabiriwa kufanya vizuri, akiwemo Cybrian Kotut wa Kenya aliyeshika nafasi ya tatu na Mmarekani Conner Mantz aliyemaliza wa nne.

Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini(TFF), limeahidi kuendelea kuwekeza kwenye teknolojia ya Msaidizi wa Video (VAR) kwa kutoa elimu kwa waamuzi wengi zaidi, na hata kuzalisha wakufunzi wazawa ili kuhakikisha usimamizi wa mechi nchini, unaendana sawa na mabadiliko kulingana na wakati kwa kufuata viwango vya kimataifa.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Sheria, Habari na Masoko wa Shirikisho hilo, Boniface Wambura ambaye pia ni Msimamizi Mkuu wa Kozi mbalimbali, zinazowezeshwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Alisema kuwa wanahitaji kuona mabadiliko chanya kwenye usimamizi wa mechi nchini, hivyo kupitia VAR wanaamini watapunguza malalamiko ya maamuzi na kuongeza ubora wa ligi na mashindano mengine wanayosimamia.
Alisema kwamba anaamini hadi kufikia muda rasmi wa kuanza matumizi ya teknolojia hiyo katika Ligi ya Tanzania, waamuzi wengi watakuwa na weledi mkubwa kuhusiana na matumizi yake.
Wambura alisema kuwa kozi hizo zitaendelea kutolewa kwa makundi mbalimbali, ili kuongeza zaidi idadi ya namba kubwa ya waamuzi wenye ujuzi wa kutumia teknolojia hiyo ya VAR.
Tayari TFF ilitangaza mpango wa kuanza kutumia baadhi ya mashine za VAR, ili kupunguza malalamiko ya kimaamuzi ingawa bado kuna uhitaji mkubwa wa mashine nyingi, ili kila uwanja uwe unatoa haki ya kimaamuzi.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Licha ya ratiba na takwimu za msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kuonyesha kwamba Yanga imebakiza michezo minne ili kumaliza msimu huu, wenyewe wanasisitiza kwamba wamesaliwa na mechi tatu pekee.
Yanga imebakiza mechi dhidi ya Namungo FC (nyumbani), Tanzania Prisons (ugenini), Dodoma Jiji (nyumbani) na Simba SC (nyumbani).
Mbali na ratiba kuonyesha hivyo, wenyewe wamesisitiza kwamba kwa sasa anazifukuzia pointi zao tisa, ili wamalize Ligi na kushangilia ubingwa wa nne mfululizo wa Ligi Kuu.
Afisa Habari wa Klabu hiyo Ali Kamwe (Pichani) alisema kuwa wao wanachotambua kwa sasa wana kazi kubwa ya kuhakikisha wanashinda mechi tatu zilizo mbele yao.
“Tuna mechi tatu zilizobaki mbele yetu, tutajitahidi kuhakikisha tunapata ushindi mechi zetu zote ili kutangaza ubingwa, hiyo nyingine hatuifahamu na haituhusu. Mashabiki wetu tunawasihi wasianze sherehe sasa hivi, ni mapema mno kwa sababu hatujamaliza mechi zetu tatu,” alisema Kamwe.
Hadi sasa wapenzi wa soka wanasubiria siku ambayo Bodi ya Ligi itaweka wazi tarehe ya mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga, ambao ulipangwa kuchezwa Machi 8 mwaka huu lakini ukaahirishwa.
Bodi hiyo bado imeonekana kuwa na kigugumizi cha kupanga tarehe ya mechi hiyo, kufuatia Yanga kupeleka malalamiko katika Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo Duniani (CAS).
Tayari CAS hivi karibuni ilitoa siku 10 kwa walalamikiwa kuwasilisha utetezi wao, baada ya Yanga kupeleka rufaa yao kuhusiana na kile kilichotokea Machi 8.
Mchezo wa Simba na Yanga una umuhimu mkubwa, kuchezwa kwa sababu huenda ndio ukawa mchezo utakaompata bingwa wa Ligi Kuu msimu huu.
Hiyo itatokea endapo Simba na Yanga wote wakaendelea kushinda bila kupoteza pointi yoyote, hadi watakapokutana wenyewe kwa wenyewe.

Na Laura Chrispin

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro – Oyesterbay, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Alister Makubi amewaasa wauguzi kuwa na roho ya huruma na wasiwe wa kwanza kuwakatia tamaa wengine, bali wawe mahujaji wa matumaini, huku wakitambua kuwa Yesu ndiye muuguzi wa kwanza aliyewaponya wagonjwa.
Padri Makubi aliyasema hayo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Wauguzi na Wagonjwa, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Fatima – Msimbazi, jimboni humo.
“Muuguzi hutakiwi kumkatia mtu tamaa, bali unatakiwa kuwa ni mtu wa matumaini kama Yesu alivyompa matumaini, yule mgonjwa aliyelala kwa miaka 38 kwa kumwambia ainuke na aende, na kuachana na maji yale yaliyokuwa kwenye birika,” alisema Padri Makubi, na kuongeza.
“Wauguzi kuweni na huruma kwa kuwatakia mema wagonjwa wenu, na kuwaambia wasimame na kuchukua magodoro yao ili waende, kwani wakati mwingine ugonjwa ni kama mradi, kwa sababu mtu anapoumwa, mwingine hufaidika.”
Padri huyo aliendelea kusema kuwa kila mtu anaumwa kimwili na kiroho, na kwamba wamepona kwa kufanya maungamo kwa kusafisha roho zao na kuwa watoto wapya wa Mungu.

Na Mathayo Kijazi

Wanaojigamba kutokana na afya, elimu, mali walizonazo, wametakiwa kuacha kufanya hivyo na kujiweka karibu zaidi na Mungu, kwani ndiye aliyewawezesha.
Wito huo ulitolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki Teule la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Lameck Musomba -OSA, wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya 5 ya Kwaresma, katika Parokia Teule ya Mtakatifu Anthony wa Padua – Nyeburu, iliyopo chini ya Parokia ya Mtakatifu Yohane Paulo II - Buyuni, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.
“Afya, elimu, utajiri pamoja na mazuri yote uliyonayo, ni Mungu ndiye aliyekuwezesha kuvipata, ni Mungu ndiye aliyekufanya kuwa hivyo ulivyo. Na kwa sababu hiyo, kiri udhaifu wako mbele yake,” alisema Askofu Musomba.
Askofu Musomba aliwataka Waamini kuacha dhambi ya uzinzi pamoja na yale yote yasiyompendeza Mwenyezi Mungu, kwani hayo hayatoi utambulisho ulio bora mbele za Mungu.