Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

1. Utangulizi
Kipindi cha Kwaresima kinahusika na liturujia ya kubariki mafuta na kuweka wakfu Krisma. Askofu hana budi kuwa kuhani mkuu wa kundi lake. Maisha ya Waamini wake katika Kristo, kwa namna fulani yanatokana naye na kumtegemea yeye.
Askofu huadhimisha Misa ya Krisma, pamoja na Mapadri waliotoka sehemu mbalimbali za Jimbo Lake. Katika Misa hiyo huweka wakfu Krisma na kubariki mafuta mengine. Misa hii ya Krisma ni njia mojawapo kubwa ya kuonyesha ukamilifu wa Ukuhani wa Askofu, na ni ishara ya muungano mkubwa uliopo kati ya Askofu na Mapadri wake.
Misa ya Kubariki mafuta ya Krisma, hufanyika kabla ya Misa ya Karamu ya Mwisho ya Bwana. Misa haiadhimishwi bila mkusanyiko wa Waamini. soma kwenye Tumaini Letu

Na Remigius Mmavele

Deusdedit Method Rwegasira almaarufu Mzee wa Katoma Band alizaliwa Aprili 26, 1963, Kata ya Katoma, mkoani Kagera, jirani kabisa na nyumbani kwa Askofu Mstaafu Methodius Kilaini wa Jimbo Katoliki la Bukoba. Baba yake alikuwa anaitwa Method Rwegasira ambaye alikuwa Mhandisi wa ndege katika Kikosi cha Anga, Ukonga jijini Dar es salaam na mama yake alikuwa Emiliana Alfred.
Alianza elimu ya shule ya msingi katika Shule ya Msingi Katoma A mwaka 1973, na baadae alihamia Shule ya Msingi Minazi Mirefu iliyopo jijini Dar es salaam, ambako alisoma kuanzia mwaka 1973 hadi 1979.
Mwaka 1983 alijiunga na Chuo cha Ufundi cha Dar es salaam katika Kozi ya GCE, na kuhitimu mwaka 1986, na kisha aliendelea na FTC kuanzia mwaka 1986, na kuhitimu mwaka 1989.
Mwaka 1990, alijiunga na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) katika Kambi ya Ruvu kwa mujibu wa Sheria, ambako alihitimu mwaka 1991. Mwaka 1992 aliajiriwa na Kampuni ya Uchukuzi ya Express Tanzania Limited, ambako alifanya kazi kwa mwaka mmoja akiwa fundi magari. Aliamua kuachana na kazi hiyo baada ya mwaka mmoja kwa ajili ya kutafuta maslahi mazuri zaidi.

Na Nicolaus Kilowoko

Diego Forlán Corazo ana umri wa miaka 45 sasa, akiwa amezaliwa mwaka 1979. Ni mchezaji wa sasa wa mchezo wa tenisi akitokea Uruguay, lakini pia ni Meneja wa soka na mchezaji wa zamani wa kandanda ambaye alicheza kama mshambuliaji.
Akichukuliwa kuwa mmoja wa washambuliaji bora zaidi wa kizazi chake, Forlán ni mshindi mara mbili wa Pichichi Trophy na Kiatu cha Dhahabu cha Ulaya katika ngazi ya klabu.
Akiwa na timu ya taifa ya Uruguay, alipata mafanikio ya kipekee katika Kombe la Dunia la FIFA la 2010, akimaliza kama mfungaji bora wa pamoja akiwa na mabao matano, akishinda bao la michuano hiyo, na kushinda Mpira wa Dhahabu kama mchezaji bora wa mashindano hayo.

LONDON, ENGLAND
Mshambuliaji wa Corinthians Memphis Depay amekosoa uamuzi wa Shirikisho la Soka la Brazil (CBF), kuwaadhibu wachezaji kwa mbwembwe za kusimama juu ya mpira wakati wa mechi.
CBF imetangaza kwamba wachezaji wanapaswa kuonyeshwa kadi ya njano, iwapo watasimama juu ya mpira kwa miguu yote miwili, na timu pinzani ikapewa mkwaju wa faulo usio wa moja kwa moja.
Uamuzi huo ulikuja baada ya Depay kufanya hatua hiyo katika dakika za majeruhi, wakati wa ushindi wa fainali ya Paulista A1 dhidi ya Palmeiras mnamo Machi 28.
Ustadi huo, uliochezwa karibu na bendera ya kona baada ya Depay kujifanya kuvuka mpira ndani ya kisanduku, uliwakera wachezaji wa Palmeiras na kuzua rabsha kubwa kati ya timu zote mbili.
Kipa wa akiba wa Palmeiras, Marcelo Lomba na kiungo wa kati wa Corinthians, Jose Martinez walitolewa nje baada ya ukaguzi wa muda mrefu wa VAR, ambao ulisababisha zaidi ya dakika 18 za muda wa nyongeza, kuongezwa na maafisa.
Katika barua iliyofuata kwa vilabu, CBF ilisema kwamba kitendo cha kusimama kwenye mpira ni chokozi kwa mpinzani na kutoheshimu mchezo.

LONDON, ENGLAND
Mlinzi wa Memphis Grizzlies, Ja Morant ametozwa faini ya dola 75,000, kwa kosa la kutumia ishara ya vidole wakati wa mchezo.
Morant alitoa ishara hizo wakati wa ushindi wa Grizzlies wa 110-108, dhidi ya Miami Heat huko Florida hivi karibuni.
NBA inasema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alionywa hapo awali na ofisi ya ligi, kwamba ishara ya kutumia vidole inaweza kutafsiriwa katika mtazamo mbaya.
Morant ambaye aliifunga timu inayoongoza kwa pointi 30 amesimamishwa mara mbili na NBA, kwa kuonyesha ishara ya bastola kwenye mitandao ya kijamii.
Alipigwa marufuku kwa michezo minane bila malipo mnamo Machi 2023, kwa kutoa ishara ya bunduki kwenye video ya Instagram Live.
Morant pia alipewa adhabu ya kufungiwa michezo 25 ili kuanza msimu wa 2023-24, baada ya video yake kuonyesha akipiga picha akiwa na bunduki kusambaa mtandaoni.
Baada ya tukio la kwanza, aliomba msamaha na kusema alichukua jukumu kamili kwa matendo yake.
Alisema kuwa atafanya kazi katika kujifunza mbinu bora za kukabiliana na mfadhaiko na ustawi wake kwa ujumla, na kwamba baada ya kutafakari, aligundua kile anachopaswa kupoteza.

Na Nicolaus Kilowoko

Kocha wa zamani wa Yanga Princess, Edna Lema ‘Mourinho’, ambaye kwa sasa ameongezwa kwenye Benchi la Ufundi la kikosi cha Wanaume cha Yanga, amekiri kuvutiwa na uwezo wa mchezaji Pacome Zouzoua.
Edna ambaye ameunganishwa katika kikosi cha wanaume mara baada ya Ligi ya wanawake kusimama, hivi karibuni ameonja ushindi wa kwanza mara baada ya timu yake ya Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union.
Alisema kuwa miongoni mwa wachezaji ambao anavutiwa nao na wenye uwezo, uzoefu, akili na maarifa wakiwa uwanjani ni Pacome ambaye kwa sasa ana mabao nane kwenye orodha ya wafungaji wa Ligi Kuu.

BAGAMOYO

Na Mathayo Kijazi

Baada ya mchakato wa muda mrefu hatimaye Bagamoyo Lango la Ukristo Tanzania sasa historia yake imekamilika, kutokana na kuundwa kuwa Jimbo jipya Katoliki, huku Baba Mtakatifu Fransisko akimteua Mhashamu Askofu Mteule Stephano Musomba, kuwa Askofu wa kwanza wa jimbo hilo.
Kabla ya uteuzi huo Mhashamu Musomba alikuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, aliyekuwa akisimamia Mawasiliano jimboni humo.

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Waamini wameonywa kuepuka kukata tamaa kutokana na majaribu wanayokutana nayo, kwani hayo ni sehemu ya maisha yao.
Kauli hiyo ilitolewa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia – Goba, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Musa Kihoo wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Kwanza ya Kwaresima iliyofanyika parokiani hapo.

MBEYA

Na Angela Kibwana

Mhashamu Godfrey Jackson Mwasekaga, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Mbeya, amesema malengo ya Kwaresima ni kufanya toba, wongofu wa ndani na uaminifu kwa neno la Mungu.
Aidha, amesema kuwa Neno la Mungu ni chakula cha kiroho, na ni taa ya kuwaongoza waamini kwenye njia ya Ukristo wao.
Askofu Mwasekaga alisema hayo wakati akitoa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu, aliyoadhimisha katika Parokia ya Mtakatifu Clara wa Asizi- Shewa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya.

Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Yakobo Mkuu Mtume – Kijitonyama, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika iliyoadhimishwa parokiani hapo hivi karibuni.