Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Benki ya Biashara ya Mkombozi imepandishwa hadhi kutoka Soko la Ukuzaji Mitaji la Dar es Salaam Stoke Exchange(DSE) (EGM) na kwenda Soko Kuu la Uwekezaji (MIMS).
Akizungumza katika hafla ya kuipandisha hadhi Benki hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande alisema kuwa benki hiyo imepanda kutoka hatua moja kwenda nyingine ndani ya muda mfupi.
“Hongereni sana Mkombozi Bank kwa hatua hii mliyofikia, kwa sababu mmepanda hadhi kutoka hatua moja kwenda nyingine ndani ya muda mfupi sana…msiridhike na hatua hiyo mliyoifikia, kwa sababu kuna maneno yanasema ‘Mpanda patosha, huvuna pa mkwisha,”alisema Chande.
Naibu Waziri Chande aliwasihi watendaji wa Benki hiyo kutoridhika na hatua waliyofikia, badala yake waendelee kufanya uhamasishaji ili Benki iendelee kukua.
Aidha, Chande aligusia pia suala la riba kwa wanaochukua mikopo, na kusema kuwa Serikali inaendelea kulifanyia kazi suala hilo, ili riba inayochukuliwa, isiwe ya kuwaumiza wananchi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Mkombozi, Respige Kimati, alisema kuwa Benki hiyo imewekeza nguvu nyingi ili kuanza kutoa gawio kuanzia mwakani 2025.
Alisema pia kuwa Benki hiyo imekuwa mstari wa mbele kuungana na Serikali katika kuwashika mkono watu waliopatwa na majanga mbalimbali ndani ya jamii.
Kimati aliongeza kuwa Benki ya Mkombozi kwa sasa imepiga hatua kubwa ikilinganishwa na miaka 10 iliyopita, ina wakala zaidi ya 1000 kote nchini.

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Fransisko ameiasa Jumuiya ya Kimataifa kuhakikisha inaendelea, kuwapokea na kuwahifadhi wakimbizi duniani kote.
Baba Mtakatifu alitoa wito huo hivi karibuni wakati wa Siku ya Kimataifa ya wakimbizi akisema kwamba inapaswa kuwa ni fursa ya kuelekeza macho na usikivu wa kidugu kwa wale wote wanaolazimika kuyahama makazi yao kutafuta amani na usalama.
Baba Mtakatifu alisema hayo baada ya Katekesi yake katika fursa ya kuelekea kilele cha Siku hiyo inayoadhimishwa kila ifikapo Juni 20 ya kila mwaka.
Katika salamu mbali mbali baada ya katekesi, akizungumza na waamini na mahujaji waliofika katika uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, kwa, Baba Mtakatifu Fransisko, alisema kwamba jamii inapasswa kutowanyanyasa wakimbizi na wahamiaji.
“Iwe ni fursa ya kuelekeza macho ya usikivu na ya kidugu kwa wale wote wanaolazimika kuyahama makazi yao kutafuta amani na usalama. Sote tumeitwa kuwakaribisha, kuwahamasisha, kuwasindikiza na kuwaunganisha wale wanaobisha hodi kwenye milango yetu,”alisema Baba Mtakatifu Fransisko.
”Ninaomba kwamba Mataifa yafanye kazi ili kuhakikisha hali ya kibinadamu kwa wakimbizi na kuwezesha michakato ya ujumuishaji.”
Baba Mtakatifu aliwakaribisha kwa moyo mkunjufu mahujaji wanaozungumza lugha ya Kiitaliano, kwa namna ya pekee, Chama cha Marafiki wa Kardinali Celso Costantini, wakisindikizwa na Askofu Giuseppe Pellegrini wa Jimbo la Concordia-Pordenone, katika kuadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Concilium Sinense ya Shanghai.
Katika hatua nyingine, Baba Mtakatifu Fransisko amewaombea wagonjwa, wazee, wenye ndoa wapya na  hasa vijana.
Aidha alikubusha siku kuu ya Mwanzislihsi wa Shirika lake inayoandimishawa kila Juni 21, kila mwaka.

TAFAKURI YA SOMO LA INJILI DOMINIKA YA 12 MWAKA B

Na Pd. Gaston George Mkude

Amani na Salama!
Baadhi ya miujiza inayosimuliwa katika Maandiko Matakatifu, inatuacha na mshangao mkubwa: Mti uliolaaniwa kwa kukosa kutoa matunda wakati si majira yake (Marko, 11:13), maji yanageuzwa kuwa divai (Yohane, 2:1-11), Yesu akitembea juu ya maji, na Petro akimwomba naye atembee juu ya maji (Matayo, 14:22-33), Petro analipa zaka ya hekalu kwa kupata pesa kutoka kinywa cha samaki (Matayo 17:24-27). Hivyo, ili kupata ujumbe kutoka miujiza ya namna hii, hatuna budi kuingia ndani kabisa bila kuishia katika miujiza pekee.
Muujiza wa leo pia ambapo Yesu anatuliza dhoruba ya upepo mkubwa baharini, ni moja ya miujiza inayotutaka kutafakari zaidi ili kuweza kupata ujumbe kusudiwa. Baada ya kulisoma somo la Injili ya leo, mara moja tunaweza kuwa na maswali kadhaa.
Mwinjili anatuambia kuwa ilikuwa jioni, na kama ni jioni iliwapasa kurejea nyumbani Kapernaumu, na siyo kuvuka na kwenda upande mwingine, maana bado swali kwa nini muda ule walivuka kwenda upande mwingine? Na zaidi sana, kwa nini walienda upande wa Wagerasi, watu waliokuwa wapagani na wasiochangamana na Wayahudi? Na hata tukisoma zaidi Injili ya Marko, tunaona kuwa Yesu hakupokelewa wala kufahamika vyema katika nchi ile ya Wagerasi. (Marko, 5:17)
Na hata wafuasi wake wanaomwamsha ili awaokoe katika hatari ile ya dhoruba kubwa, na wanafanya hilo, kwani waliamini katika uwezo wa Yesu, lakini Yesu anawakemea kwa kuwa hawana imani. Pia, hata baada ya Yesu kuituliza dhoruba ile kubwa, tunashangaa kuona wanafunzi wake, badala ya kufurahi, wamejawa na uoga na hofu kuu.
Ni kwa msaada wa maswali haya ndipo tunaweza sasa kuona somo la Injili la leo linatualika kwenda ndani zaidi ili kuweza kupata ujumbe kusudiwa. Si nia wala lengo la Mwinjili Marko kutupa simulizi tu la muujiza alioufanya Yesu wa kuituliza dhoruba, bali tangu mwanzo tunaona ni nia ya Mwinjili Marko kutusaidia hatua kwa hatua katika kumtambua Yesu ni nani, utambulisho wa Kimasiha unaojifunua hatua kwa hatua.
Hivyo, masimulizi na nia kuu ya Mwinjili Marko ni kumtambulisha Yesu kwetu, kwa kila mmoja anayetaka kukutana na kumjua Masiha, basi Injili ya Marko ni msaada mkubwa kwetu. Ni Injili ambayo tangu mwanzoni inajaribu kujibu swali lile la; Yesu ni nani.
Leo tunakutana na chombo kikiwa baharini pamoja na vyombo vingine, zaidi sana pia chombo hiki kikielekea katika nchi ya wapagani, yaani Wagerasi, mawimbi makali na makubwa, giza la usiku, maana ilikuwa jioni, Yesu amelala katika shetri na juu ya mto, upepo mkali, hofu na uoga uliowajaa wafuasi wa Yesu, ni moja kati ya lugha ya picha tunazokutana nazo mara nyingi katika Maandiko Matakatifu.
Injili yetu ya leo inaanza na kutuambia muda wa muujiza ndio jioni, na uelekeo wa chombo kile alimokuwemo Yesu na wanafunzi wake.
Ni jioni. Ndiyo kusema ni baada ya Yesu kumaliza utume na misheni yake ya kuusimika na kuutangaza Ufalme wa Mungu, wanafunzi wake wanaingia chomboni pamoja na Yesu na kuelekea upande mwingine, lakini wanakwenda wapi haswa?
Ni baada ya kusoma zaidi Injili ya Marko, kwamba walikuwa wanaelekea katika nchi ile ya Wagerasi, waliokuwa wapagani. (Marko 5:1) Na ndipo tunaona mara moja kuwa katika nchi ile kulikuwepo na nguruwe malishoni mlimani, ambapo Yesu baada ya kumponya mtu aliyekuwa na pepo wachafu, pepo wale wakamwomba Yesu, kutoka na kuwaingia nguruwe, na hata nguruwe wale wakaishia wote baharini. Uwepo wa nguruwe kati yao ni ishara tosha kuwa watu wale hawakuwa Wayahudi, bali wapagani, kwani Wayahudi ni marufuku kufuga au kula nyama ya nguruwe.
Chombo ndiyo ishara ya jumuiya ya Wakristo yaani Kanisa lake Yesu Kristo, ambao baada ya Yesu kukamilisha utume na misheni yake, wanaalikwa kutoka na kwenda kuitangaza Habari Njema ya Wokovu kwa watu wote. Lakini tunaona chomboni lazima pia awepo na Yesu, kwani uwepo wake ni wa lazima na wa muhimu kwa usalama wa jumuiya ya Kanisa. Tunaona leo chombo kikiwa katikati ya safari, kinakuwa katika hatari kubwa kwa upepo mkubwa na dhoruba.
Mwinjili Marko anatuambia pia kwamba kulikuwa na vyombo vingine, ndiyo kusema Mwinjili anajaribu kutuonesha kuwa hata baada ya utume wa Yesu Kristo kukamilika hapa duniani, kulikuwa na jumuiya kadhaa za Kikristo katika Kanisa lile la mwanzo.
Ilikuwa jioni, ndiyo kusema ilikuwa giza. Giza katika Maandiko ni ishara hasi, ni kukosekana utaratibu kama ilivyokuwa mwanzo kabla ya uuumbaji. (Tohuwabohu - Mwanzo, 1 :2). Fujo ni kukosekana uwepo, na hasa uweza wake Mwenyezi Mungu.
Ni hapo katika uwepo wa giza tunaona yule mwovu anatawala, na hivyo tunahitaji uwepo wake Mungu ili kututoa na kutuacha salama katika mitego ya yule mwovu. Chombo kinasafiri saa ile ya giza, saa ile ya fujo, saa isiyokuwa ya mwanga wala utulivu. Ni saa ile ambayo chombo kinakuwa katika hatari kubwa na kupigwa na kuyumbishwa na upepo mkali wa dhoruba.
Yesu anakuwepo chomboni, lakini amelala katika shetri, sehemu ambayo kwa desturi anakaa nahodha, muongoza meli au vyombo vya majini. Ni Yesu anayepaswa kuwa nahodha na rubani wa chombo kile, yaani Kanisa lake, Ni yeye ambaye tunapaswa kumkimbilia na kumlilia. “Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?” (Marko, 4 :38).

Kwa kumalizia Tafakuri hii nunua TumainiLetu

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, akibaliki matoleo ya waamini wakati wa Adhimisho la Takatifu la Misa ya Kipaimara, iliyofanyika Parokia ya Mtakatifu Clara-Magole, Jimboni humo. Kulia ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Christian Singano.

Viongozi na waamini wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mwokozi, Sinza Jimbo Kuu Katoliki la Dar es  Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara iliyofanyika hivi kalibuni parokiani hapo.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi  akiwapatia vijana vyeti baada ya kupokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, katika Adhimisho la Misa Takatifu iliyofanyika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mwokozi, Sinza jijini Dar es Salaam.

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Clara –Magole, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Christian Singano [katikati mwenye kanzu] akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Kamati Tendaji ya parokia hiyo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara.

Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Ambrosi –IPTL, Salasala, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Paul Sabuni akimkabidhi Mwenyekiti mpya wa Parokia Teule ya Utatu Mtakatifu-IPTL, Restituta Mingo, bahasha  za kutegemeza Tumaini Media, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika iliyokwenda sanjali na kuapishwa Viongozi wapya wa Parokia hiyo. (Picha zote na Yohana Kasosi).

Maskofu kutoka Majimbo mbalimbali ya Kanisa Katoliki nchini na Wakuu wa Mashirika ya Kitawa, wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Maaskofu, uliofanyika katika Ukumbi wa AMECEA, Baraza la Maskofu Kurasini (TEC), jijini Dar es Salaam. (Picha na Yohana Kasosi)

MWANZA

Na Paul Mabuga

Upepo unavuma katika jua la saa nane, na miti iliyo karibu inatoa ukinzani,  hali hii inazalisha mvumo ulio sawa na wimbo mzuri unaopigwa kwa ala tupu! Hakika, hali hii ingeweza kuwa ya kufurahisha, lakini la hasha! Aron Malifweda [48], [siyo jina lake halisi kwa sababu za kitaaluma], zaidi ya kutafakari kila swali analoulizwa kwa ajili ya makala haya, huku akiwa ameketi kiambazani kwenye nyumba yake iliyo kwenye moja ya miji mdogo kanda ziwa, ni kama haoni wala kusikia kingine cha ziada katika mazingira yake.
Ni kwa sababu amechanganyikiwa na kuzama katika fikra zisizo na msaada wala  ufumbuzi, anaona ni kama ametengwa na jamii yake kutokana na hali aliyonayo, anachokitamani anaona kama ananyimwa, na hivyo kukata tamaa.
Alitaka awe na  watoto, ikashindikana kwa nguvu za kiume [syo rijali]. Lakini sasa anataka kuasili mtoto anakayerithi mali zake, lakini amepewa sharti, kwamba ni  lazima aoe na kuishi na mke.
“Unajua nimehangaika kwa  miaka mingi, iwe kwa madaktari hospitali, ama tiba asilia, lakini sikufanikiwa. Baadaye daktari mmoja ninayemwamini akaniambia kwamba siwezi kuondokana na hali hiyo nilipata huzuni sana siku hiyo, na nikaona dunia yote imeniangukia.
Nikifikira maisha ya kukaa bila mke wala watoto, nilikiona hata kifo kinaninyemelea! Nimehangaika hivii kwa zaidi ya miaka 15,” anasema Malifwedha, wakati akisimulia kisa chake cha sharti la kuhifadhiwa utambulisho.
Anasema kuwa kama suluhisho katika hilo, alishauriwa na daktari huyo kwamba atafute mtoto wa kuasili ndiye atakayekuwa  mrithi wa mali zake, jambo ambalo anaeleza kuwa  awali lilikuwa gumu, kwani wapo waliomkatisha tamaa kwa kumtishia kuwa anaweza kupata kijana, akamlea, lakini baadaye atakapokua, asimjali na kumkimbia akirejea katika familia yake ya uzao wa kibayolojia.
“Walikuwa wananiambia, Unaweza kupata mtoto wa kuasili na kumsomesha, lakini akifika chuo kikuu, akakukumbia na kukutelekeza,” anasimulia Malifwedha na kuongeza kuwa, “Baada ya ushauri wa Maafisa Ustawi wa Jamii katika eneo langu, nilipata moyo wa kuanza mchakato wa kupata mtoto wa kuasili, ambao. Licha ya jambo kwenda vyema, lakini sasa nimefikia pahala umekwama kutokana na sharti nililopewa, kwamba ni lazima nioe!”
Kwa mujibu wa Tovuti ya Wakala wa Uzazi na Vifo, kuasili watoto ni mchakato wa kisheria ambao huhamisha uwajibikaji wa mzazi kutoka kwa wazazi wa kuzaliwa kwa watoto, kwenda kwa wazazi  wa kuwalea. Kuasili mtoto kunaongozwa na sheria  ya kuasili mtoto, Sura Namba 335 Toleo la Mwaka 2002.
Na kwa mujibu wa sheria hiyo, mara mtoto anapoasiliwa, basi unajengwa uhusiano wa kudumu na wa moja kwa maoja kati yake na wazazi waliomuasili, na kwamba haki zote kutoka kwa wazazi wake wa kibayolojia [wa damu] zinafutika na kuhamia katika familia yake mpya. Pia, Wazazi wa damu nao haki zao kwa mtoto aliyeailiwa, nazo zinakoma.
Tukirejea kwa Malifedha, anaeleza kuwa baada ya kupata mtoto wa kuasili, na wazazi wake wa damu kutoa ridhaa chini ya usimamizi wa Maafisa Ustawi wa Jamii, na uchumguzi wa kina kufanyika katika kipindi cha miezi sita, alijaza fomu mbali mbali na taarifa za ufuatiliaji zikaandikwa, tena zikionesha kwamba ana mwenendo mzuri, na ana uwezo wa kuasili.
Bila shaka mchakato kama huu, kulingana na taratibu, baadaye ulihitaji idhinisho la mamlaka ya juu ya Ustawi wa Jamii. Kutoka hapo, hoja hupelekwa mahakamani mbele ya jaji, na  kama kutakuwa na kukidhi matakwa ya kisheria, basi, hutolewa amri ya kuasili, na mchakato huwa umekamilika. Hata hivyo, katika muda wote Maafisa Ustawi wa Jamii huendelea kufuatilia ustawi na maslahi ya mtoto.
Pengine kilichoonekana kuwa ni kikwazo kwa Malifwedha kwa mujibu wa sheria hiyo, ni kwamba mzazi wa kiume anayeishi pake yake haruhusiwi kumuasili mtoto wa kike, ama vingunevyo kuwe na mazingira mahsusi! Ingawaje hata huvyo  anaruhusiwa kuasili mtoto wake wa kiume. Na pia, kuwe na tofauti ya umri wa miaka  isiyopungua 21 kati ya mzazi anayeasili, na mtoto anayeasiliwa.
Tena basi, inaelekezwa katika kanuni za sheria hiyo kwamba katika mazingita yanayofaa, mtoto aliyeasiliwa, atakapofikisha umri wa miaka 14, ataelezwa hali ya kuasiliwa kwake na maafisa ustawi wa jamii katika eneo husika.
Kuhusu suala na kuoa Malifwedha anasema, “Nilikwenda kwa wanasheria, wakaniambia kuwa huyo mwanamke nikimuoa, atakuwa na haki zote kama mke kwenye mali zangu, hata kama itakuwa ni ndoa ya kudanganyia ili tu nipate kibali cha kuasili! Hilo nalo nkaliona gumu. Nikashauriwa niende kwa Wakurya,  eti huko ukioa mwanamke aliyezalia nyumbani, na ukishatioa mahari, watoto wanakuwa mali yako.”
Sadick Hunga ambaye ni Mwandishi wa Habari anayefanya kazi zake Mkoani Mara, na ambaye ni mmoja wa wanajumuia ya Wakurya wanaoishi Mkoani humo,  anasema katika mahojiano kwa njia ya simu kwamba, mila hiyo ipo katika jamii yake na imeendelea kuwepo, kwamba katika jamii hiyo, wakati wote watoto huwa ni mali ya mwanaume aliyelipa mahari.
“Huyu jamaa sisi tunamuambia karibu ‘tata’ [baba]! Yaani huku kwetu, kama mwanamke amezalia nyumbani, akaja mwanaume kumuoa, analipa mahali ya mke, mathalani ng’ombe sita, lakini baadaye atatakuwa kuwalipia watoto mahari nyingine inayoitwa ‘kuborora’, ambayo inaweza kufikia hadi ng’ombe wawili kwa kila mtoto, na kutokea hapo watoto hao wanakuwa mali yake daima dumu, hata wana umri mkubwa namna gani,” anasema Hunga.
Katika mtazamo mwingine Hunga anasema kuwa miongoni mwa jamii ya Wakurya, ikiwa mwanamke ameachana na mume wake, na  ikatokea akaolewa na mwanaume mwingine, basi, watoto wote watakaozaliwa katika familia mpya ni mali ya yule mume wa awali, “na hii imetokea majuzi huko Serengeti! Itaondoka tu ikiwa mume mpya atalipa mahari kurejesha iliyokwishakulipwa kabla.”
Wakati hali ikiwa hivi, Malifwedha bado yupo njia panda juu ya nini akifanye ili kukabiliana na hali hii, kwani ana malalamikio mengine. Anadai kwamba ndugu zake wanamtenga na hususan yanapokuja matukio kama harusi huwa hashirikishwi, na hilo linamuongezea mawazo! “Yaani utasikia tu kuna harusi huko, lakini hushirikishwi, huwa najiuliza, sijui wananionaje,” anasema.
Kuna changamoto nyingine pia, kwani Malifwedha akifikisha umri wa miaka 50, yaani katika kipindi cha miaka miwili ijayo, kwani suala la kuasili litakuwa na kipingamizi, kwani halitakuwa katika maslahi ya mtoto, na hususani katika maendeleo na makuzi yake. Na itakuwa ni kazi kubwa kujenga hoja dhidi ya pingamizi kama hizi kulingana na kanuni za kuasili.
Mrumbi wa masuala ya ndoa na muendeshaji wa kipindi cha ‘Ndoa Aminifu’ cha Runinga ya Tumaini, Paschal Maziku, anasema kwamba ndoa katika Kanisa Katoliki huwa ni kwa ajili ya manufaa ya wanandoa wenyewe, watoto wanaowalea na jamii kwa ujumla, na wala siyo kwa manufaa binafsi kama ilivyo katika jambo hili katika makala haya.
“Isitoshe, huyu bwana hawezi kuwa na ndoa, kwani ndoa huwa kati ya mwanamke na mwanaume rijali. Sasa jamaa na hali aliyonayo, haiwezekani, maana ndoa ili  ikamilike inahitaji kuwa ‘consummated’ [tendo la ndoa kufanyika ndani ya muda unaovumilia kwa busara ana kupatilizwa], kinyume na hapo inavunjwa”
Kuhusu, kuasili watoto, Maziku anasema, huko ni sawa na mtoto kuwa ‘displaced’ [kuwa pasipostahili],  na kwamba, “ni vema tukarejea katika mila zetu, kama ni yatima ama ana mazingira magumu, basi ndugu wa karibu, wajomba, mathalani baba wadogo na wengine, wachukue majukumu yao.”