Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

NSSF yazidi kuboresha huduma za Wanachama

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba akizungumza na Waandishi wa Habari. Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba akizungumza na Waandishi wa Habari.

DAR ES SALAAM

Na Alex Kachelewa

Uongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), umesema hatua ya kuboresha huduma zake kumesaidia mfuko huko kupiga hatua kubwa kimaendeleo kwa kuwa na ongezeko kubwa la mapato hadi kufikia Shilingi trilioni 8.5/- ikiwa ni ongezeko la asilimia 70% ya waajiri wapya.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, alisema hayo hivi karibuni wakati akizungumza katika Mkutano kati ya NSSF na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), uliofanyika jijini Dar es Salaam.
“NSSF imepiga hatua kubwa sana mwaka hadi mwaka na hasa wakati huu ambapo huduma zetu tumeziboresha zaidi na kumaliza kero mbalimbali kwa wanachama wetu hasa wazee ambao walikuwa wakijipanga mstari katika ofisi zetu kwa muda mrefu kusubiria huduma ya madai yao…
“Lakini kwa sasa mtu anaweza kukaa hata sebuleni kwake kwa kutumia simu yake ya mkononi anahakiki michango yake na anaweza kufanya mchakato wote wa malipo na akafanikisha akiwa huko alipo na hiyo pia hata kuomba kadi endapo itapotea,”alisema Mshomba.
Mshomba alisema kuwa mpango wa NSSF kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA, imeufanya mfuko huo kupiga hatua kubwa na kuondoa usumbufu wote uliokuwa ukijitokeza miaka iliyopita na sasa mambo ni mazuri kwa wastaafu kwani kila kitu kinafanyika kwa wakati kwa njia ya mtandao.
Mshomba alibainisha kuwa kwa sasa uongozi wake unaendelea na mikakati mbalimbali, ili hadi kufikia Desemba mwaka 2025, huduma zote zifanyike kwa kutumia TEHAMA.
“Tayari sisi NSSF tumezindua huduma ya Mwanachama wetu kuproces mafao yake kwa njia ya mtandao mfumo huu utakwenda kuondoa usumbufu wote kufika ofisini atamaliza yeye mwenyewe huko huko,”alisema Mshomba.
Kuhusu sekta Binafsi, Mshomba alisema kwamba tayari mchakato umekamilika kwa lengo la kuhakikisha watu waliojiajiri katika sekta zisizo rasmi ikiwemo, kilimo, ufugaji, uvuvi, uchimbaji madini wadogo na kadhalika watafikiwa kwa huduma ya NSSF ili nao waweze kupata mafao wakiwa wazee.
Alifafanua kuwa Wanachama wa sekta hizo wao wamewekewa utaratibu mzuri wa kuchangia kiasi cha Shilingi 30,000/- kwa mwezi au kulipa kidogo kidogo kwa kila siku, wiki ama mwezi ili nao waweze kunufaika na akiba za uzeeni.
Aidha, Mshomba alisema mpango huo unakwenda sanjari na wafanyakazi wa Sekta binafsi ambao wanapenda kujiwekea akiba zaidi wao wewenye kwa njia ya uchangiaji binafsi ili waweze kutunisha zaidi akiba zao za mafao.
Kwa mujibu wa Mshomba, kwa sasa baada ya Sheria mpya kupitishwa na Bunge Wanachama pia wanaweza kufanya kazi sehemu mbili hata tatu na waajiri hao wote wakawachangia fedha katika akiba zao za mafao, isipokuwa mwajiri moja anapaswa kuthibitisha wazi kwamba ndiye atakayehusika moja kwa moja na NSSF, kwa kukumbushwa kuwasilisha michango hiyo kisheria.
Hata hivyo, Mshomba alitumia nafasi hiyo kuwasihi wanachama kuacha tabia ya kukimbilia kuchukua mafao yao kabla ya kutimiza umri wa kustaafu, kwani kufanya hivyo ni kujinyima fursa hasa manufaa ya mafao uzeeni.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.