Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Kuandika matusi karatasi za mitihani ni fedheha kwa Taifa

DAR ES SALAAM

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mitihani ya kuhitimisha Kidato cha Nne, Tanzania (CSEE) ilifanyika Novemba 11 hadi 29, 2024.
Matokeo yakatangazwa rasimi Januari 23, 2025 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (National Examinations Council of Tanzania: NECTA) Dk. Said Mohammed kupitia hafla na Waandishi wa Habari.
Taarifa iliyotolewa na Mtendaji Mkuu wa NECTA, ilionyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia tatu (3) kutokana na watahiniwa wengi kufaulu.
Hiyo inamaanisha kuwa kati ya watahimiwa 516,695, kati ya hao watahiniwa 477,262 wamefauli kwa madaraja: I, II, III na IV; ikiwa ni ufaulu wa asilimia 92.37 kulinganisha na matokeo ya mitihani ya 2023 yenye ufaulu wa asilimia 89.36 tu.
Kadhalika, ufaulu kwa madaraja ya I, II na III ni watahiniwa 221,952 sawa na asilimia 43, wakati mwaka 2023 walikuwa watahiniwa 197,426 sawa na asilimia 37.4 tu.
Vile vile, matokeo yameonyesha kuwa waliopata daraja la nne (iv) pamoja na waliopata alama (sufuri) wamepungua kulinganisha na matokeo ya mwaka 2023; hivyo kuashiria ongezeko la asilimia 5.6 wa ubora wa kufaulu.
Hata hivyo, Katibu Mtendaji, NECTA alibainisha kuwa kwa matokeo ya mwaka 2024, watahiniwa 67, NECTA imelazimika kufuta matokeo yao kutokana na udanganyifu wakati wakifanya mitihani.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.