Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Pro-Life: Wanawake pokeeni zawadi ya Uzao

Mkurugezi wa Shirika la Kutetea Uhai Tanzania (Pro-Life Tanzania),Emil Hagamu akitoa semina kwa wanawake kuhusu uzazi. Mkurugezi wa Shirika la Kutetea Uhai Tanzania (Pro-Life Tanzania),Emil Hagamu akitoa semina kwa wanawake kuhusu uzazi.

DAR ES SALAAM

Na Gaudence Hyera

Wanawake wameaswa kupokea kwa ukarimu, furaha na upendo zawadi ya uzao wanayojaliwa na Mungu, hata kama uzao huo  umepatikana katika mazingira magumu.
Wosia huo ulitolewa na Mkurugezi wa Shirika la Kutetea Uhai Tanzania (Pro-Life Tanzania), Emil Hagamu, katika Kipindi cha Pro-Life juu ya Familia na Hifadhi ya Uhai kilichorushwa na Radio Tumaini, na kuwataka wanawake wasikatae heshima kuwa mama.
Alisema kuwa wanawake wanapaswa kuhifadhi, kupokea mimba katika hali ya furaha, iwe ni katika ndoa, ama ni kubakwa, kwa sababu hawajui kwa nini Mungu aliruhusu jambo hilo litokee.
Hagamu alisema sifa na furaha ya mwanamke, mke ni kuwa mama, na kwamba haipendezi kuona mwanamke ambaye Mungu amemjalia baraka za mimba, anakwenda kuua mtoto aliye tumboni, eti kwa dhana ya kwamba hajawa tayari kuwa mama.
Aliwataka wanawake wanapopata mimba kupokea na wamtukuze Mungu kama ilivyokuwa kwa Bikira Maria Mama wa Mkombozi, na kwamba waache malalamiko, manung’uniko na kuona mimba kuwa ni mzigo katika safari ya maisha yao.
“Mama wa Mkombozi, Bikira Maria alipopata taarifa kutoka kwa Malaika Gabriel ya kwamba atachukua mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, alipokea taarifa hiyo kwa furaha na kumtukuza Mungu, wala hakuogopa, licha ya kwamba alizifahamu Sheria za Kiyahudi juu ya adhabu ambayo ingemkabili,” alisema Hagamu.
Alisema kwamba hata sasa kuna baadhi ya wanawake ambao kwa bahati mbaya wanapata mimba katika mazingira ya kubakwa na kuchukua uamuzi wa kuua mtoto aliye tumboni kwa hofu ya familia na jamii kuwa itawatazama vipi, ama atalea vipi mtoto bila baba, na kusahau kwamba Mungu ana kusudi katika jambo hilo.
“Nawaalika wanandoa katika mwaka huu mpya kutafakari ikiwa wanatimiza kiapo walichopata wakati wa Sakramenti ya Ndoa, kutafakari juu ya Maneno Matakatifu ambayo yanasema ‘mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao watoto wengi.’ Je, ni kweli wale waliobarikiwa wanatimiza maandiko hayo? au wamekuwa wakishiriki Utamaduni wa Kifo kwa kutumia vithibiti mimba” alisema Mkurugenzi wa Pro-Life, Hagamu.
Alisema kwamba watoto wengi ni baraka ya Mungu katika kiapo cha ndoa, hivyo amewataka wanandoa kutimiza ahadi ya kiapo hicho, na kuwa tayari kupokea watoto ambao Mungu atawajalia kwa furaha.
Kwa mujibu wa Hagamu, kitendo cha wanandoa kutumia vithibiti mimba, kunazifanya ndoa hizo kuwa batili, kwani zinakiuka kiapo cha kupokea watoto watakaojaliwa na Mungu.
Katika suala la malezi, Hagamu aliwataka wazazi kuwakabidhi watoto wao kwa Mungu, ili wapate baraka siku kadhaa  baada ya kujifungua, kama ilivyokuwa kwa wazazi wa Yesu, ambapo walimpeleka Yerusalemu kupata baraka kwa Simeoni.
Alisema pia kwa kufanya hivyo watoto watakua na kuongezeka nguvu, huku wakiwa wamejaa hekima na neema ya Mungu zikiwa juu yao, kama ilivyokuwa kwa Mtoto Yesu.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.