Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Vijana wa Kiume wanaovaa hereni wanyooshewa kidole

Waimarishwa wa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Mtakatifu Fransisko Ksaveri – Chang’ombe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salam, wakiwa kwenye maandamano ya kuingia kanisani kwa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo. (Picha na Mathayo Kijazi) Waimarishwa wa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Mtakatifu Fransisko Ksaveri – Chang’ombe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salam, wakiwa kwenye maandamano ya kuingia kanisani kwa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti hiyo. (Picha na Mathayo Kijazi)

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Vijana wameonywa kuacha kuiga tamaduni zisizofaa, ikiwemo wanaume kuvaa hereni na kusuka nywele zao.
Aidha, wametakiwa kudumu katika imani, wakitambua kwamba tamaduni hizo zinaweza kuwaingiza  kwenye dhambi.
Kauli hiyo ilitolewa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 98 katika Parokia ya Mtakatifu Fransisko Ksaveri – Chang’ombe, jimboni humo.
“Mnapopokea Sakramenti hii ya Kipaimara na mnatakiwa muendelee kudumu katika imani yenu, hivyo mnatakiwa kuepuka kuiga tamaduni zisizofaa, mfano, unamkuta mwanaume anavaa suruali anaweka mlegezo, anavaa hereni, anasuka nywele kichwani kama mwanamke. Epukeni kuiga tamaduni za namna hiyo,” alisema Askofu Mchamungu.
Pia, aliwasisitiza kujiepusha na tabia za udokozi pamoja na kutumia mali zisizokuwa za kwao, bali wahakikishe kwamba pale wanapookota vitu, wavirudishe kwa wenyewe.
Aliwasisitiza pia kuwajibika katika usafi pamoja na kutunza mazingira, akisema kuwa suala la usafi wa mazingira wao kama vijana, linatakiwa kuwa kipaumbele kwao.
Wakati huo huo Askofu Mchamungu aliwakumbusha Wasimamizi wa Waimarishwa hao kwamba miongoni mwa majukumu yao, ni pamoja na kusaidiana na Wazazi katika malezi, ili kujenga maadili ya vijana hao.
Kwa upande wake Paroko wa Parokia hiyo, Padri Novatus Mbaula alimshukuru Askofu Mchamungu kwa kufika parokiani hapo pamoja na kuwaimarisha vijana 98 wa Parokia hiyo.
Aidha, Padri Mbaula aliwasihi vijana hao kuendelea kuyazingatia yale yote waliyoambiwa na Askofu wakati wa homilia yake, kwani mafundisho hayo yatawasaidia kukua katika misingi iliyo bora.
Naye Katibu wa Parokia hiyo, Simon Sangawe alivishukuru vyombo vya habari vya Kanisa vilivyoshiriki katika Adhimisho hilo, ikiwemo Tumaini Media, akisema kuwa vyombo hivyo vinafanya kazi kubwa katika suala la uinjilishaji.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.